Sunday, April 7, 2013

FACEBOOK CHATTING--------- 3



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269



MSICHANA: Mbona kimya?
MIMI: Unajua internet connection inazingua sana. Yaani mara ikate, mara irudi. Yaani tabu tupu.
MSICHANA: Poleee. Naomba unijibu basi.
MIMI: Ninae kwa sasa.
MSICHANA: Unae?
MIMI: Ndio. Ila hanionyeshei mapenzi ya dhati. Mara nyingi najitahidi kumtumia meseji, hanijibu, nikimpigia simu usiku, ipo bize tu. Tena si hivyo tu, hadi usiku wa manane ipo bize. Unahisi nini hapo?
MSICHANA: Unaibiwa.
MIMI: Kama naibiwa, nawe upo tayari kumuibia?
MSICHANA: Una maana gani?
MIMI: Hahahaha! Acha utani. Usitake nianze kutoa maana moja kwa moja hadi watu wa facebook washtukie.
MSICHANA: Kama yeye mwizi, sina budi nami kuwa mwizi.
MIMI: hauoni dhambi kuiba?
MSICHANA: Kwenye mapenzi sidhani kama kuna dhambi kuiba. Anayeua kwa upanga nae atauawa kwa upanga.
MIMI: Mmmhh! Sawa. Ila samahani kidogo. Kuna swali nataka kukuliza.
MSICHANA: Kuwa huru
MIMI: Unaonekana kuwa msichana wa tofauti sana. Yaani sio aina ya msichana ambaye amekulia hapa.
MSICHANA: Yeah! Nimeishi sana nchini Marekani ambako huko nilikaa kwa muda mrefu sana na ndipo nikalilia kuja Tanzania.
MIMI: Mmmh!
MSICHANA: Mbona unaguna tena?
MIMI: Hakuna bhana.
MSICHANA: Vipi kuhusu namba ya simu.
MIMI: Kwani unaitaka leo?
MSICHANA: Ndio. Nataka tuongee leo kama nilivyokwambia.
MIMI: Hivi unajua leo lini?
MSICHANA: Jumatatu.
MIMI: Hatutoweza kuongea kwa leo. Kesho inatakiwa niwe chuoni saa tatu.
MSICHANA: Chuo gain?
MIMI: Ninaposoma.
MSICHANA: Kwa hiyo tutaongea lini?. Nina hamu sana ya kusikia sauti yako.
MIMI: Labda Ijumaa.
MSICHANA: Kuanzia saa ngapi?
MIMI: Saa tano.
MSICHANA: Ok! Kadri tunavyoendelea kuongea na ndivyo ambavyo ninazidi kufall inlove zaidi.
MIMI: Hahahahaha
MSICHANA: Unazicheka hisia zangu?
MIMI: Hapana. Umekuwa mwepesi sana kufall inlove.
MSICHANA: Yeah! Sijui kwa sababu gani.
MIMI: Labda kwa sababu una hamu ya kuniumiza hapo baadae.
MSICHANA: Haiwezekani kabisa. Labda wewe ndio uniumize.
MIMI: Kwangu haitowezekana kabisa. Niamini.
MSICHANA: Sawa. Ila naomba unipe namba ya simu ili niwe na amani.
MIMI: Usijali. Nipe yako ili nikupigie.
MSICHANA: Yangu ni 0719 878 ……
MIMI: Poa.

Sikutaka kuchelewa, nilichokifanya ni kumpigia na kuanza kuongea kwa dakika chache na kisha kurudi tena kwenye meseji ndani ya mtandao wa Facebook. Sauti yake ilikuwa nzuri sana, yaani ilifanana na jinsi alivyokuwa. Mara nikashtukia meseji kutoka kwake ikiingia kwenye akaunti yangu ya facebook.

MSICHANA: Mmmh! Una sauti nzuri mpenzi.
MIMI: Hahaha! Acha kunizingua bhana. Mbona sauti yangu mbaya sana.
MSICHANA: Nzuri, nimeipeda sana.
MIMI: Asante. Hata yako nzuri pia. Ulikuwa muimba kwaya nini?
MSICHANA: Yeah! Ila nilipokuwa nchini Marekani.
MIMI: Basi ndio maana.
MSICHANA: Naomba tuendelee kuchati baadae mpenzi. Mama amenipigia simu na kuniambia anataka twende Mlimani City kufanya shopping ya vyakula na mavazi.
MIMI: Poa. Ila kama ukichelewa sana, unaweza kunikuta nimelala.
MSICHANA: Usijali, nitawahi.
MIMI: Ok.
MSICHANA: Nakupenda mpenzi.
MIMI: Nakupenda pia.

Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kuanza mahusiano na msichana ambaye sikuwahi kukutana nae. Nikajiona kikizama kwenye mapenzi kwa asilimia mia moja, moyo wangu ukaonekana kumhitaji kupita kawaida.

MIMI: (Mawazoni: Dah! Nimeshachanganyikiwa sasa. Ngoja nilale then nichati nae hiyo usiku).

Akili yangu ilikuwa imechoka sana na hivyo nilihitaji muda wa kulala. Nililala kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka saa mbili usiku. Nilipoamka, nikaelekea kuoga, nikala na kisha kuwasha laptop. Nilipojiunga na mtandao wa facebook, msichana yule alikuwa miongoni mwa marafiki zangu waliokuwa online.

MSICHANA: Waaaoooo! Karibu mpenzi.
MIMI: Asante.
MSICHANA: Nimekumiss mpenzi.
MIMI: Nami pia baby. Kuna jipya?
MSICHANA: Mengi tu.
MIMI: Kama yapi?
MSICHANA: Nilitaka kumwambia mama kuhusu wewe. Ameniona kuwa wa tofauti sana leo, muda wote alikuwa akiniona kuwa na furaha.
MIMI: Naomba usifanye hivyo.
MSICHANA: Kwa nini?
MIMI: Muda bado wa kufanya hivyo.
MSICHANA: Lakini ni kitu cha kawaida baby. Unafikiri atanigombeza? Wala hatoweza kufanya hivyo.
MIMI: Najua ila naomba usifanye hivyo kwa sasa.
MSICHANA: Sasa unataka nimwambie lini?
MIMI: Siku yoyote ile lakini sio wiki hii.
MSICHANA: Sawa. Ninauheshimu uamuzi wako.
MIMI: Nashukuru kwa kunisikiliza mpenzi.
MSICHANA: Kuna kitu nataka kufanya.
MIMI: Kitu gani?
MSICHANA: Nimemwambia rafiki yangu kuhusu wewe.
MIMI: Rafiki yupi?
MSICHANA: Rafiki yangu, Lydia.
MIMI: Ndiye nani huyo?
MSICHANA: Ninasoma nae shule. Amefurahia sana. Naweza kumuonganisha tuchati pamoja nae?
MIMI: Kwani yupo online kwa sasa?
MSICHANA: Ndio. Tena amenitumia meseji na kuniambia kuwa tuchati wote watatu.
MIMI: Poa. Tengeneza kundi la watu watatu.
MSICHANA: Sawa

Nikabaki kimya, msichana huyu alionekana kuchanganyikiwa zaidi yangu, mapenzi yalikuwa yakionekana kumchanganya akili yake kupita kiasi. Kwa jinsi alivyokuwa na furaha, nilimuona kuwa na kiu ya kutaka kumfahamisha kila mtu kuhusu uhusiano wetu.

MSICHANA: Tayari.
MIMI: Mambo Lydia.
LYDIA: Poa. Mzima shemeji
MIMI: Mzima tu. Maisha yanasemaje?
LYDIA: Safi tu. Mbona umemchanganya sana rafiki yangu?
MIMI: Nimemchanganya au kajichanganya?
MSICHANA: Umenichanganya.
MIMI: Hapana bwana. Umejichanganya wewe mwenyewe.
LYDIA: Kwa hiyo amejichanganya yeye mwenyewe?
MIMI: Ndio. Au kama nimekosea sana, acha niseme kwamba mapenzi ndio yaliyomchanganya.
LYDIA: Hahahaha
MSICHANA: Sasa unacheka nini na wewe.
LYDIA: Case closed. Wewe umeniambia amekuchanganya kumbe umejichanganya wewe mwenyewe. Hahahaha
MSICHANA: Unacheka unaona mazuri Lydia? Nimejaribu kusoma lakini nashindwa kabisa, yaani kila nikijaribu, nakuwa sina hamu kabisa. Si unaona hata kukupigia simu nimeshindwa siku ya leo.
LYDIA: Acha utoto wewe. Unajifunza kupenda nini?.
MIMI: Ajifunze wapi huyo. Anaonekana mzoefu tu wa mapenzi.
MSICHANA: Nani kakwambia kama mimi mzoefu? Au kwa sababu ya picha?
LYDIA: Picha gani tena?
MSICHANA: Hayakuhusu na wewe.
LYDIA: Sasa kama hayanihusu kwa nini umeniambia niongee nae?
MSICHANA: Nimekwambia uongee nae lakini si kumuuliza kuhusu picha. Hilo niachie mimi na Nyemo wangu.
MIMI: Mbona mnakuwa kama hamueleweki? Tatizo nini tena?.
MSICHANA: Hakuna tatizo mpenzi. Naomba turudi kwenye chartin yetu kama kawaida. Achana na huyu Lydia.
MIMI: Mbona umebadilika ghafla mpenzi?
MSICHANA: Kawaida tu.
LYDIA: Ok! Usikasirike rafiki yangu. Nyemo naomba unitumie friend request.
MSICHANA: Hapana. Sitaki. Usimtumie mpenzi.
MIMI: Kwa nini?
MSICHANA: Basi tu.
LYDIA: Acha wivu shosti. Haujiamini?
MSICHANA: Najiamini ila naogopa udhaifu wa mwanaume.
MIMI: Hahahaha
MSICHANA: Unacheka kwani uongo? Nyie wadhaifu sana. Huyu Lydia anaweza akaleta matatizo katika mahusiano yetu. Mahusiano yenyewe bado machanga sana.
MIMI: Aya. Umeshinda wewe mpenzi. Kama vipi usiku mwema Lydia, naona dogo ameshakasirika bhana.
MSICHANA: Nani dogo?
MIMI: Wewe. Kwani unajiona mkubwa? Bado mdogo.
MSICHANA: Sawa. Wewe si mkubwa! Usiku mwema Lydia.
LYIDA: Nanyi pia.

Mawasiliano ya watu watatu yakakatika muda huo, kundi la kuchati la watu watatu likafutwa na kurudi katika mawasiliano ya kawaida. Kuna hali nikaanza kuigundua, msichana huyu alikuwa akionekana kuwa na wivu sana, alitaka mimi niwe wake kama wake tena peke yake, hakutaka mtu yeyote amuingilie kwenye mapenzi yake. Tukaanza kuchati kama kawaida yetu.

MSICHANA: Unataka niibiwe mali yangu.
MIMI: Hahahaha! Wasiwasi wako tu. Mwizi hawezi kukuibia kama sijampa nafasi ya kukuibia.
MSICHANA: Sawa bwana.
MSICHANA: Naomba kitu kimoja mpenzi.
MIMI: Kitu gani?
MSICHANA: Nimeshindwa kuvumilia kabisa.
MIMI: Kuvumilia nini?
MSICHANA: Nimeshndwa tu. Naomba tufanye mapenzi kwa njia ya simu.
MIMI: Mbona unakuwa na haraka hivyo?
MSICHANA: Ndio maana nimesema naomba. Naomba unisaidie katika hilo mpenzi. Pleaaseee
MIMI: Sawa.
MSICHANA: Nashukuru kwa kunisikiliza.
MIMI: Usijali. Ila mchezo huu una sheria zake ili uchangamke.
MSICHANA: Sheria gani?
MIMI: Moja, Utatakiwa kufanya kila kitu nitakachokwambia. Usipofanya tu, umeharibu mchezo.
MSICHANA: Nitafanya.
MIMI: Mbili, Unatakiwa kunipa nafasi mwilini mwako. Wewe kuwa kila sehemu ya mwili wako, ila mikono yako acha niwe mimi.
MSICHANA: Sawa. Hakuna tatizo.
MIMI: Simu yako inatumia hearphone?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Basi kwa leo tumia hizo.
MSICHANA: Sawa. Kuna kingine mpenzi?
MIMI: Ndio. Nitumie namba yako ya vodacom. Nataka tutumie mtandao huo leo. Tigo network yao inazingua sana, wanaweza kutukatisha mara kwa mara.
MSICHANA: Sawa.

Wala hakutaka kuchelewa, hapo hapo akanitumia namba yake ya Vodacom japokuwa alikuwa akitaka yeye kunipigia. Muda ulizidi kwenda, msichana yule alionekana kuwa na kiu kubwa ya kufanya mapenzi kwa kutumia njia ya simu. Kila wakati alikuwa akiniambia wazi kwamba muda ulikuwa hauendi kabisa. Ilipofika saa tano, nikampigia kwa kutumia laini ya Vodacom, akakata simu na kisha kunipigia. Hakujua kama mimi ndiye nilikuwa mkali wa kufanya mapenzi kwa njia ya simu. Nilikuwa nikiufahamu sana mchezo ule ambao ulikuwa unachezwa sana na vijana kama sisi ambao tulikuwa tumekulia uswahilini, hasa huku Tandale.

MIMI: Upo tayari?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Uko peke yako chumbani?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Unaikumbuka sheria yetu ya kwanza?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Ilikuwa inasemaje?
MSICHANA: Nifanye kila utakachoniambia.
MIMI: Safi sana. Naomba uzime taa.

Nikaanza kumsikia akiinuka kitandani, baada ya muda, nikaisikia switch ikilia kuona kwamba tayari alikuwa amezima taa ya chumbani kwake na kisha kurudi kitandani.

Itaendelea

No comments:

Post a Comment

Recent Posts