Tuesday, November 27, 2012

HATIA------- 15


MTUNZI: George Iron

CONTACTS: 0655 727325


SEHEMU YA KUMI NA TATU


Matha bila kujua kuwa anafuatiliwa alielekea barabarani akaangaza hapa na pale akanyanyua mkono wake wa kuume akaita taksi, haraka haraka dereva aliyekuwa amemuona Matha aliifikisha gari yake Matha akaingia ndani.

John akasubiri ile teksi ilivyoanza kuondoka naye akaingia katika teksi aliyokuwa amekodi.

“Fuata gari hiyo!!” alitoa maelekezo hayo John, dereva akafuata maelekezo. Gari mbili zikawa zinafuatana bila gari ya mbele kuwa na habari juu ya hilo, John alikuwa amevaa miwani nyekundu kuziba macho yake yaliyokuwa mekundu sana, hakutaka kumtisha dereva.


*****

Adrian alikuwa amekaa nje ya duka kubwa la kuuza nguo maeneo ya Makoroboi, umeme ulikuwa umekatika na biashara haikuwa nzuri sana siku hiyo. Adrian alikuwa anaperuzi katika gazeti la michezo alilokuwa amenunua muda mrefu uliopita.
Ubovu wa biashara wa siku hiyo haukumshtua sana Adrian kwani alikuwa na uhakika kuwa maduka mengine matano yaliyokuwa yamezagaa jijini Mwanza yangekuwa na biashara nzuri siku hiyo.
Mzee Mhina Mboje alikuwa amemuamini sana kijana wake huyu wa pili kuzaliwa, japo aliwahi kuikataa shule alipokuwa kidato cha tatu lakini akili yake katika kutafuta maisha ilikuwa inavutia wengi sana na kuwapa wivu. Adrian sasa alikuwa anasimamia maduka yote ya baba yake huku lile la Makoroboi likiwa mali yake binafsi. Adrian aliwahi sana kujipanga kimaisha kwani tayari alikuwa ameondoka nyumbani miaka mingi iliyopita na kuamua kufanya maisha ya kupanga.
Mwanzoni alikuwa anakaa na mdogo wake wa kiume lakini baada ya kuingia katika mahusiano ya kimapenzi aliamua kumrudisha mdogo wake nyumbani kwa wazazi ili aupate uhuru zaidi wa kujivinjari na binti huyu. Kwa kuwa ulikuwa upendo wake wa kwanza alikuwa akimsikiliza sana binti huyo ambaye alikuwa bado ni bikra, mapenzi yao ya kitoto toto waliyajua wao wenyewe. Adrian hakuruhusiwa kufanya lolote katika mwili wa huyu binti zaidi ya kumbusu shavuni tu na kuishia kucheza cheza.
Adrian hakuruhusiwa pia kutangaza kwa mtu yeyote juu ya uhusiano huu eti kisa tu baba yake binti alikuwa mkali sana. Upendo wa dhati ukawa umejijenga.
Ile hali ya Adrian kuukana uhusiano wake mbele ya watu ili kumfurahisha mpenzi wake huyo ilikuja kumgharimu sana. Akatokea mwanaume aliyekubuhu akamlaghai huyu binti ambaye ni Matha, alikuwa ni John Mapulu aliyemnyang’anya Adrian Mhina tonge mdomoni. Matha akahamishia upendo wake kwa John ambaye alikuwa ameitoa bikra yake. Adrian akabaki kama zezeta asijue la kufanya lakini hatimaye akazoea baada ya wawili hawa kuhamia sehemu nyingine kabisa mbali na yeye.
Kumbukumbu juu ya Matha zikasahaulika pia kutokana na mchumba wake ambaye walikuwa wanatarajia kuoana baada ya mwezi mmoja kwani walikuwa na mwaka mzima tangu waishi maisha ya uchumba huyu alikuwa ni Monica Lewis, dada zake walikuwa wakimpenda sana na hii ndio ilikuwa chachu ya kumshawishi Adrian kuoa.
Mara kwa mara Monica alikuwa analala nyumbani kwa Adrian, na hata kabla ya kutambulishana kwa wazazi tayari Monica alikuwa ameshiriki katika tendo la ndoa na Adrian, ujanja aliofanyiwa na Matha miaka iliyopita hakutaka tena kumwamini mwanamke.
Mwezi mmoja kabla ya ndoa tayari Monica alikuwa mjamzito, jambo hilo walilitambua wao peke yao, hawakutaka wazazi watambue hali hiyo ya wao kupata mtoto nje ya ndoa.
“Mambo vipi kaka” alisalimiwa Adrian akiwa bado ameinamia gazeti lake.
“Poa karibu!!” alijibu huku akiunyanyua uso wake. Hakutaka sana kumuangalia mtu aliyekuwa mbele yake kwa sababu alikuwa ameficha uso wake.
“Unanikaribisha unanijua kwani??” aliuliza yule binti ndani ya baibui, Adrian akacheka.
“Adrian!!! Za siku!!”
“Mh!! Kwani we nani”
“Matha!!! Jamani” alijitambulisha. Kumbukumbu ya sauti ile ya kupendeza ikarejea katika kichwa cha Adrian. Kabla hajajua la kufanya, Matha alimsogelea na kumkumbatia. Adrian hakuamini alichokuwa anakiona mbele yake, Matha akasikika kama analia, kilio hicho kikafuta hasira zote alizokuwanazo Adrian, joto lililopenya katika baibui na kumuingia Adrian likaibua hisia za upendo.
Walikumbatiana kwa dakika nzima. Kisha baada ya kuachiana Matha alijifunua kidogo, Adrian akaona vishimo katika mashavu ya Matha.
Upendo maradufu ukamvaa!!!
Matha akawa katika majuto ya hatia iliyokuwa inamkabili kwa yote aliyomtendea Adrian miaka iliyopita. Kwa mbaali akausikia mguso wa kimapenzi kutoka kwa Adrian. Akaanza kupatwa na hofu huenda Adrian bado ana hasira, lakini haikuwa hivyo!!!!
Walizungumza kwa dakika kadhaa kisha Matha akamwachia namba yake kijana huyu mwenyeji wa Tanga aliyekulia jijini Mwanza.
Yote hayo yaliyokuwa yanatokea yalishuhudiwa na jicho kali lililokuwa nyuma ya miwani, jicho la John Mapulu. Alitamani kumfyatua palepale yule mwanaume lakini alijikaza, akauzuia wivu usipitilize. Akawa amemtambua mwizi wake akapanda teksi na kuondoka, wakati huo na wawili hawa walikuwa wameagana.
Laiti kama angesubiri kidogo tu angepata kufahamu kuwa mpenzi wake huyo anakwenda kukutana na Minja anayeaminika kuwa alikufa usiku uliopita.
Lakini John Mapulu hakuwa na subira.

John alirejea nyumbani kwake, hakutaka tena kwenda kwenye tukio la ujambazi akili yake ilikuwa imechanganyikiwa kabisa. Uchungu alioupata Adrian miaka mitatu iliyopita sasa ulikuwa umemgeukia yeye.
Wakati anamnyakua Matha mikononi mwa Adrian alijiona kidume sasa na yeye alikuwa katika majaribu ya namna ya kipekee.
“Kama mwanzoni nilimchukulia Matha wake sasa wakati huu naitwaa roho yake, mshamba kama yule hawezi kumchukua Matha kirahisi hivyo, nitamuua!!!” aliapa John kwa sauti ya juu.
Alikuwa kama amechanganyikiwa!!!
Wivu ukawa unamtesa!!!


******


“Tukutane hapo nje ya chuo cha biashara (CBE)”
“Sawa dada” alijibu Minja. Matha akapiga hatua kadhaa akawa amefika hapo chuoni. Minja alikuwa ameanza kukasirika baada ya kuwa anapiga simu ya Matha halafu haipokelewi.
“Ingia ndani!!!” Matha alimuamrisha Minja bila kumuangalia usoni. Hiyo ilikuwa ni mbinu ya kuepusha kama yupo mtu anawafuatilia asiweze kugundua lolote. Laiti kama angejua aliyekuwa anawafatilia tayari amepata jibu na kuondoka hata asingeweza kujihangaisha hivyo.
Minja aliingia akaa katika meza moja, baada ya dakika mbili Matha naye akafika.
“Samahani kaka naweza kukaa hapa?” alizuga, Minja akashangaa. Matha akajiongeza akakaa.
“Chooni wapi kaka samahani” aliuliza kwa sauti ya juu ili majirani waweze kumsikia.
Minja akashangaa tena.
Matha akamuuliza mtu mwingine akaelekezwa akaenda uani.
Aliporejea alikaa alipokuwa Minja. Aliamini kuwa tayari amewapoteza baadhi ya watu.
“Ehee!! Kuna tatizo gani?”
“Yaani sijui nisemeje”
“Umeniita kufanya nini kama hujui la kusema” aliunguruma Matha, Minja akaogopa.
“Usiku kuna mtu ameuwawa ndani kwangu” alijitutumua na kumueleza kila kitu kilivyokuwa. Matha akawa ameelewa kuwa dhumuni lilikuwa ni kuuwawa kwa Minja.
“Laiti kama John angempata jana basi najua mambo yangekuwa mabaya……” aliwaza Matha huku walau hofu ya John kugundua tatizo hilo ikianza kupungua, lakini uwepo wa Minja jijini Mwanza ungekuwa bado ni tatizo. Matha hakuona tena haja ya kumuua Minja kwani alimuona kama hana hatia yoyote ile tena.
“Unatakiwa uondoke haraka hapa Mwanza”
“Sasa naenda wapi dadangu nisaidie”
“Hujui pa kwenda, basi utaenda jela” alisema Matha, Minja akatetemeka kusikia hivyo.
“Chukua hii, kesho uondoke!!!” Matha alimkabidhi Minja shilingi laki moja.
Laiti kama angejua kuwa Minja kuna jambo zito analifahamu wala asingekubali aondoke hai jijini Mwanza.
Asubuhi iliyofuata Minja akaondoka kuelekea Singida, alitegemea kufikia kwa rafiki yake ambaye waliwahi kufanya shughuli za udalali pamoja jijini Dar es salaam. Amani ikarejea moyoni mwake, akajihisi kuwa hana hatia tena. Akawa amesahau kuwa hatia humfuata muhusika popote atakapoenda.
Hatia ilipanda naye katika basi kuelekea Singida!!!!
Hatia haimuachi muhusika mpaka mwisho wa uhai wake, hatia huingia na mtu wake kaburini!!!


******


Adrian aliwahi sana kufunga duka siku hiyo, aliikatisha ahadi aliyokuwa nayo ya kutoka jioni ya siku hiyo na mpenzi wake (Monica). Kitendo cha kumuona Matha kwa mara nyingine tena kilikuwa kimeamsha ari fulani katika nafsi yake.
Alifika nyumbani kwake akaoga na kisha akaingia kitandani. Aliyawaza maisha yake na Matha miaka ya nyuma katika nyumba hiyohiyo hadi siku alipomsaliti na kuondoka na John. Zilikuwa ni hisia za kipekee zilizojawa na historia ambayo Monica hakuwa nayo kwani walikutana ukubwani.
Ile hali ya kukosa nafasi ya kuitoa bikra ya Matha ilimtesa sana lakini bado aliona si bure anaweza kuthubutu kumtoroka Monica kisha walau afanye mapenzi na Matha kama njia ya kupunguza machungu aliyoyapata wakati ule.
Adrian akaamua kumpigia simu Matha. Simu iliita kidogo ikapokelewa, alikuwa ni Matha katika sauti iliyochangamka sana. Adrian alilitambua hilo akajijengea kujiamini sana. Walizungumza mengi sana, na kuishia katika mazungumzo yaliyohusisha penzi lao la wakati ule. Mazungumzo hayo yaliibua hisia kwa kila mmoja, Matha akawa wa kwanza kulia, Adrian Mhina akaligundua hilo akajaribu kumbembeleza sana lakini kwa kuwa alikuwa yupo kwenye simu ilikuwa ni kazi bure.
“Adrian nahitaji kukuona!!!!” Matha alijikuta akitamka kwa hisia kali. Adrian hakuamini alijua kuwa Matha anatania. Lakini kadri alivyorudia mara kwa mara ndipo aliamini kuwa alikuwa anamaanisha mpenzi huyu wa zamani.
Kwa kuwa alikuwa ameoga tayari, alivaa pensi ambayo hupendelea kuivaa jioni, juu akavaa fulana iliyokuwa inambana na kuonyesha kifua chake jinsi kilivyokuwa kimejigawanya katikati, chini akavaa viatu vya wazi.
Akachukua pochi yake, akatazama ndani yake palikuwa na kadi ya benki (ATM) na noti kadhaa za shilingi elfu kumi na elfu tano.
Hizo zilimtosha kwa ajili ya kuchukua teksi iliyomfikisha maeneo ya PPF Tower, akazama katika mashine ya kutoa pesa akajitwalia kiasi alichotaka, kisha akapanda tena hiyo teksi iliyokuwa inamsubiri.
“Tunaelekea wapi bosi!!!” alitamka yule dereva, Adrian akatabasamu kusikia anaitwa bosi, tabasamu lake likaruhusu meno yake yaliyoathiriwa na utafunaji wa vitu vyenye sukari kuonekana.
“Millenium Hotel Nyegezi” alijibu kwa sauti nzito na tulivu.
Safari ikaanza!!!

Matha alikuwa anamaanisha alichokuwa anamwambia Adrian kwenye simu, picha za Michael na John Mapulu zilitokea mara kwa mara lakini hazikuweza kukizuia kivuli cha Adrian Mhina. Alijua ni kweli anafanya usaliti lakini, ile hatia ya kumtenda Adrian miaka kadhaa iliyopita ikawa inamuadhibu. Matha akajikuta anafanya maamuzi ya ajabu!! Maamuzi ya kuificha na kuifuta hatia hiyo kwa kumpa penzi Adrian.
“John alimdhulumu Adrian, Michael amemwibia John, na Adrian anachukua kwa Michael….ah!! wote weziiii” alisema Matha wakati akiikaribia hoteli ya Millenium iliyopo maeneo ya Nyegezi jijini Mwanza.
Matha alianguka kifuani mwa Adrian baada ya kuwa wameingia chumbani, Adrian alimpokea kwa kumbatizi lenye huba ndani yake. Machozi yakamtoka Matha na kukilowanisha kifua cha Adrian, Adrian hakuwa jasiri na yeye akatokwa machozi. Walikuwa wanavuta fikra za miaka iliyopita.
Baada ya kuachiana, kila mmoja alimtazama mwenzake, halafu kwa pamoja wakautazama mlango kumbe ulikuwa unapiga kengele ya kuwapa taarifa ya kuwa upo wazi, wakatabasamu Matha akaenda kuufunga vizuri.
Wakati anaenda mlangoni Adrian alipata fursa ya kumwangalia vizuri jinsi alivyokuwa ameumbika, hakuwa na shaka hata kidogo kuwa alikuwa na haki ya kumtoroka Monica siku hiyo na kuzini nje. Matha alikuwa ni mrembo haswaa, wakati anaufunga mlango aliinama kidogo, kikaonekana kicheni kinang’ara katika kiuno chake.
Macho yakamtoka Adrian, alijua kuwa Matha alifanya maksudi kwani tangu zamani hizo alikuwa anafahamu ni kwa jinsi gani yeye (Adrian) ni mfuasi wa kiurembo hicho.
Wakati Matha anarejea katika mwendo wa kunyata na yeye Adrian alielekea Matha alipotoka, akachomoa kikadi kilichokuwa pembeni kidogo ya mlango. Taa zote zikazima!!! Kiyoyozi kikawaka!!!
Teknolojia ina mambo!!!!
Akarudi kwa hisia za kupapasa akafika na kumkuta Matha bado amesimama. Akamkumbatia tena na kumbusu.
“Asante Adrian!!!” alishukuru Matha kwa sauti ya kimahaba.
Katika chumba hicho hakuongelewa Michael, John wala Monica.
Kila mmoja alijua kuwa alikuwa anaiba!!!!



*****


Monica alikuwa anampenda sana Adrian sio tu kwa kuwa alikuwa na pesa na pia anatoka familia ya kitajiri la!! Moyo wa kujali aliokuwanao Adrian ulimvutia zaidi. Japo wasichana wengi walidhani kuwa Monica amefuata pesa kwa Adrian.
Siku hii Monica alikuwa anataka kuzungumza na Adrian juu ya ndoa yao ambayo ilikuwa imekaribia na huo ujauzito aliokuwanao.
Suala la kuitunza siri ya ujauzito huo ilikuwa imemchosha hivyo alihitaji kumshauri Adrian kuwa wawe wawazi.
Adrian aliporejea tu kutoka Nairobi alipokuwa amefuata mzigo wa nguo mpya. Monica alimuomba waonane, Adrian akawa amempangia Monica siku hii ambayo alikutana na Matha. Ile hali ya Adrian kuhairisha ghafla miadi hiyo wakati yeye Monica akiwa amejipanga na kuwaaga wazazi wake ilimshtua na kumkera sana, alijiuliza maswali mengi.
“Mara anaumwa!!! Sijui hajisikii vizuri!!!...kuna ukweli hapa au mume wangu amenichoka!!!” alijiuliza. Hakutaka kumwambia mtu yeyote kuwa Adrian amehairisha ahadi yake. Aliona aibu kwa wadogo zake wa kike ambao kila siku walikuwa wakimwonea wivu.
Monica akawaza sana mwishowe akaamua kwenda kwa Adrian bila taarifa.
“Isijekuwa ana kasichana leo hapo kwake….yaani sijui nitamfanyaje!!!” aliwaza Monica, wakati huo ilikuwa saa nne usiku.
Kimya kimya huku mapigo yake ya moyo yakimwenda mbio aliifikia nyumba ya Adrian. Akanyata hadi mlangoni.
Akatega sikio hakusikia lolote lakini pumzi zikipishana hapa na pale. Kabla ya kugonga mlango akaiondoa kanga yake aliyokuwa amevaa akabakia na kisketi kifupi sana, lengo likiwa kumtega Adrian.
Akaikunja kanga na kuitia katika mkoba, akajaribu kufungua mlango ukawa haujafungwa, akausukuma taratibu ndani taa ilikuwa imezimwa, akapiga hatua mpaka ndani.
“koh….koh….koh…” akakohoa baada ya kukutana harufu ya sigara, wakati anaiendea taa akasikia kitu cha baridi kabisa kikimgusa shingoni.
“We Adrian wewe!!! Hebu acha ujinga…ina maana kumbe…..” kabla hajamaliza alisikia kitu kizito kikitua mgongoni mwake, hakikuwa chuma lakini mkono wa mtu, viatu virefu alivyokuwa amevaa vikamtegua mguu wakati anajaribu kutafuta balansi. Akapiga ukelele wa nguvu ukelele wa maumivu.
Mara taa ikawashwa, hakuwa Adrian!!! Ilikuwa sura ngeni kabisa machoni mwake.
“Shkamoo” alisalimia kwa uoga, akajibiwa kwa tabasamu feki, macho mekundu.
“Wewe ni nani yake Ady” aliulizwa.
“Nani mimi?” aliuliza na yeye il-hali wapo wawili tu hapo ndani. Akapokea pigo jingine usoni akatoa kelele tena. Kelele hazikuwa na msaada wowote kwani nyumba ya Adrian ilikuwa imejitenga sana.
“Mke wake…naniii mchumba” alijibu Monica. Uso wake tayari ulikuwa mwekundu na alikuwa anajitahidi kuizuia damu inayomtoka isiendelee kutoka kwa kujilamba midomo.
Jibu hilo lilikuwa baya sana mbele ya mtu aliyekuwa mbele yake. Mwanzoni alikuwa ameishikilia bunduki lakini sasa akaiweka kando akamvagaa yule msichana akamchania chania nguo zake, kisketi, bikini, sidiria na blauzi Monica akawa uchi wa mnyama. Lakini mbele yake alikuwepo mnyama mwingine John Mapulu. Kama vile simba anavyomvagaa swala ndivyo John alifanya akamvagaa na kuanza kumbaka Monica kwa kulazimisha, nguvu alizokuwanazo zilimshinda Monica ambaye alikuwa hajaandaliwa, maumivu yakamzidi damu nazo zikamvuja sana.
“Nisamehe!!!”
“Akusamehe nani?? Unajua Adrian yupo wapi na anafanya nini??” aliuliza John huku akiendelea kumbaka Monica.
Baada ya kumbaka alimtembezea mwaliko wa kipigo kikali sana. Monica akapasuka pasuka.
John hakuwa na huruma!!! Tayari alijua kuwa yu hatiani hivyo ongezeko la hatia nyingine kwake halikuwa tatizo. Maana hatia moja ukiongeza nyingine jibu bado ni HATIA.
Alitambua kuwa ameua tayari!! Akavaa nguo zake na kutoweka bila kizuizi chochote, akimwacha Monica nusu mfu nusu hai.



*****


Matha na Adrian waliamka kwa ajili ya kujiandaa majira ya saa kumi na moja alfajiri.
Wote walikuwa hawawezi kutazamana usoni. Hakuna aliyeweza kuzungumzia kuhusu usiku uliopita. Kila mmoja alijidai hajui kinachoendelea.
Adrian aliwahi bafuni akabonyeza kitufe katika moja ya kona ya bafu maji yakaanza kupata joto, alipohakikisha joto hilo ni sahihi akaenda na kumchukua Matha wakaingia kuoga wote. Huko walikuwa kama watoto wadogo, mara wafinyane wamwagiane maji wabebane waogeshane ilimradi tu burudani.
Walitumia saa zima bafuni na wote walitoka wakiwa na furaha.
“Twende ukapaone kwangu najua umepasahau tayari, maana lile ghorofa la mzee Kimaro limevunjwa tayari yaani huwezi kupakumbuka”
“Siwezi kupotea hata iweje, sasa nitakuja peke yangu kesho!!” aliahidi Matha katika hali ya kubishana. Adrian akakubaliana naye kwamba kesho ataenda mwenyewe. Waliagana kwa kukumbatiana pale chumbani kisha wakateremka na kwenda kupata kifungua kinywa halafu wakapanda teksi iliyomfikisha Matha hadi Buzuluga stendi na kisha kuondoka na Adrian kuelekea Isamilo.
Wakapungiana mikono ya heri.
Adrian alipoagana na Matha ndipo alipata upenyo kidogo wa kumfikiria Monica, kwanza alimchukulia kama msichana ambaye ameingilia mapenzi yake na Matha. Aliamini Monica ndiye alipaswa kuwa mpenzi wa John halafu yeye na Matha waendelee kama zamani.
Suala la Matha kuwa bado hajazaa lilizidi kumtia hamasa Adrian na kuamini kabisa kuwa alipangwa kwa ajili yake kiumbe huyu. Uchungu wa bikra ya Matha kutolewa na mtu mwingine tayari ulikuwa umepoozwa usiku uliyopita, penzi alilopata kwa Matha lilikuwa limekifuta kidonda kile, wazo la kuendelea kuwa na Matha katika mapenzi lilivamia kichwa chake, likamyumbisha kimsimamo akaanza kuziona siku za kufunga ndoa na Monica zikizidi kusogea. Adrian akaanza kumuona Monica kuwa si mwanamke sahihi tena kwake.
Adrian alitaka kumkwapua Matha, jumla jumla.
Akiwa katika mawazo hayo akaikumbuka mimba aliyokuwa nayo Monica. Jambo hilo likamfadhaisha sana alijua hicho ndio kilikuwa kiunganishi baina yao.
Naenda kumshauri aitoe!!!! Aliijiwa na wazo hilo la kishetani.
Lakini kabla ya kumwambia aitoe hebu ngoja kwanza nikazungumze na mzee juu ya kuhairisha ndoa hii kwanza. Adrian aliwaza hivyo kwani alikuwa anaamini mzee wake alikuwa anampenda sana hivyo atamsikiliza na kumsaidia.
“Hebu ingia huku Kirumba kwanza” Adrian alimwamuru dereva aende upande alioutaka. Huko ndipo alikuwa anakaa mzee Mhina na familia yake, hapo hapo nyumbani mzee Mhina alikuwa na ofisi yake ndogo.
Adrian alifika na kuingia moja kwa moja ndani akawasalimia ndugu zake kisha akaenda kidogo kudeka kwa mama yake kabla ya kuingia ofisini kwa baba yake.
“Simba hilooo!!!” alikoroma mzee Mhina akimsifia mtoto wake. Adrian alizipokea zile sifa kwa kicheko kidogo kisha akamsalimia mzee wake kwa kumshika mkono halafu akakaa.
“Umetutenga sana simbaaaa!!!!”
“Majukumu baba!!!!” alijibu Adrian.
“Anakuja Monica tu, ana juhudi sana yule mtoto wangu” maneno hayo yaliyotoka katika kinywa cha Mzee Mhina yalimchoma sana Adrian kwani alijua ni kiasi gani familia yake ilikuwa inampenda Monica.
“Monica akija ni sawa nimekuja mimi” alijibu kwa sauti ya chini Adrian.
“Haya niambie mguu huo najua ni kwangu”
“Ndio mguu huu kwako kuna jambo nahitaji tuzungumze kidogo ni kuhusu ndoa yangu mimi na Monica” Mzee Mhina akashtuka kidogo, akaacha kazi alizokuwa anafanya akaondoa miwani yake machoni akamtazama Adrian.
“Umempiga mtoto wa watu eeh!!” alibashiri. Adrian hakujibu akatabasamu!!!
“Bora ingekuwa hivyo tungeyamaliza wawili”
“Nini sasa tatizo….”
Kabla mzee Mhina hajamaliza kuzungumza alikatishwa na simu ya Adrian.
“Ah!! Namba mpya hizi zinaniboa sana” alilalamika huku akijiweka sawa koo kwa ajili ya kupokea simu ile.
“Adrian Mhina nani mwenzangu!!!”
“Naitwa Jose kuna tatizo hapa kwako!!!”
“Tatizo tatizo gani??” alihoji kwa mshangao mkubwa Adrian, mzee Mhina alikuwa makini kana kwamba alikuwa anausikia upande wa pili unavyojieleza.
“Mkeo… ni mkeo…..hebu njoo” kauli hiyo ikamnyanyua kutoka katika kiti alichokuwa amekaa, akaanza kupambana na joto kali lililomkumba ghafla. Mzee Mhina naye akasimama wima na kumsogelea mwanaye.
“Adrian nini kimetokea kwani”
“Hata sielewi wananiambia mke wangu sijui, hebu ngoja niende baba”
“Tunaenda wote hebu ngoja” mzee Mhina aliingia ndani akachukua funguo za gari lake akamuaga mama Adrian bila kumwambia lolote linaloendelea.
Injini za gari zilizimwa mbali kidogo na nyumba aliyokuwa anaishi Adrian kwani umati ulikuwa mkubwa sana, Adrian alikuwa anatetemeka sana lakini mzee Mhina ukongwe ulimsaidia aliweza kupambana na presha ile.
“Mungu Wangu sijui kama ni mzima yule” walisikika watu wakizungumza. Adrian aliyasikia hayo, mzee Mhina akawa makini amemshika mkono kwani aliamini kuwa kuna tatizo kubwa ambalo mwanae hawezi kulihimili.
Na kweli hakuwa amewaza vibaya mzee huyu, punde tu baada ya kuuona mwili wa mpenzi wake Monica ukiwa umezungukwa na damu pande zote lakini ukiwa umesitiriwa kwa upande wa kanga Adrian alilegea na kupoteza fahamu palepale. Likaanza zoezi la kumpepea pasipo mafanikio.


****ADRIAN anaanza kunogewa na penzi lake la utotoni kwa MATHA...sasa anataka kumdhulumu JOHN MAPULU jumla....akiwa bado katika mwanzo wa harakati..linatokea tukio baya nyumbani kwake...MONICA anabakwa!!! MSHTUKO!!!

****JOHN MAPULU amebaka huku akiamini kuwa ADRIAN ndiye mwizi wake namba moja....anaapa kumwondoa duniani..je? atatimiza!!!!

****MINJA amesafiri na hatia yake kukimbilia Singida..je!! hatia imekubali kubaki Mwanza na kumwacha huru MINJA!!!!

Usikose

No comments:

Post a Comment

Recent Posts