Tuesday, December 18, 2012

SITAISAHAU facebook-------------- 22

 

 

MTUNZI: Emmy John P.

CONTACTS: 0654 960040

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

...
Joka lilijinyanyua juu. Sote tukawa chini yake. Joka lenye rangi ya dhahabu!! Sasa ikawa patashika kila mtu analazimisha kujificha nyuma ya mwenzake. Hakuna aliyetaka kufa. Mimi, Jenipher na wale wengine waliokuwa wanatambua yule nyoka amekuja kufanya nini pale tulijiweka mbali na vile vipande vya zile nya
ma zenye namba 666.
Joka likavimba kama linataka kutema sumu. Likavimba zaidi kama linataka kupasuka. Hatimaye likautoa ulimi nje. Likatanua mdomo kama linataka kutumeza sote. Kisu chan gu bado kilikuwa mkononi.
Mara likajirusha na kujizungusha kama pangaboi. Hapa hakuna kitu kilichosalia. Kila mmoja wetu alirushwa mbali kabisa. Mimi sikuumia lakini wenzangu waliumizwa.
Nilipogeuka nilimwona kiumbe akiwa amelowa damu akiwa na jambia mkononi. Alikuwa akikimbia mahali ambapo joka lipo. Alikuwa ni Samson yule jasiri wa kisukuma.
Macho yako yalifumba kisha yalipofumbua alikuwa ameingia mzimamzima katika kinywa cha yule nyoka. Jambia na yeye wakawa wamemezwa.
Hali ya hatari!! Nilijitahadharisha.
Joka lilikuwa linameza vile vipande vya mabaki ya nyama yenye chapa ya 666. Ndipo hapa nilimuona tena yule Osmani aliyetambuliwa kama waziri wa miundombinu. Nikakumbuka kuwa ni huyu bwana nimeambiwa kuwa anazijua njia zote za kutoka katika mji huu wa kishetani. Nikamnyemelea huku nikiwa makini na yule joka na pia nikiwa makini asiweze kuhisi chochote kile.
Nikamfikia nikamkaba shingoni. Nilikuwa na nguvu za ajabu sana. Nikamvuta hadi katika kichaka nilichokuwa nimejihifadhi hapo.
Hakuwa ananiona!! Jambo hilo lilinipa nafasi nzuri ya kumtawala. Kwa ukombozi wa wengi na kujitoa katika adha ya kufia katika mji huo. Nikanyanyua kisu changu nikazamisha katika paja lake. Akatoa kilio kikubwa sana. Kilio kile kikasababisha lile joka linyanyuke mara moja. Likaanza kuangaza huku na huko. Nami nikatulia tulii kuangalia nini kinatokea. Joka likanyanyuka kisha likatanua midomo yake. Kisha likionekana dhahiri kuwa na hasira lilitapika. Maajabu!! Samson yule jasiri katika vita hiyo akatangulia kisha jambia lake likafuata.
“Njia ya kutoka hapa ni ipi?” nilimuuliza Osman huku bado akiwa katika himaya yangu.
“Sijui.” Akanijibu kwa jeuri. Nikamchoma tena kisu katika sehemu ileile kilipopitia awali.
“Nasemaaaaa!” akapiga kelele.
“Dakika moja tu nakupa sema upesi.”
Osman akaanza kutoa maelekezo ya namna gani ya kutoka katika kijiji hicho cha maajabu!!
Maelezo yalikuwa yamenyooka!! Japo yalikuwa na masharti. Sikuwa na budi kuendelea kumshikilia. Ni huyu angetuwezesha kutoka.
Joka lilizidi kuhangaika.
Sasa lilitazama mahali alipokuwa Osmani na mimi. Likatambaa kwa hasira kali sana likawa linatufuata. Nikajikuta namuiachia Osmani. Nikaanza kukimbia. Joka likawa linaufuata uelekeo wangu.
Mungu wangu!! Kumbe linaniona sasa hivi. Nimekwisha.
Nilizidi kutimua mbio. Hatimaye mbio za sakafuni zikaishia ukingoni! Nikaanguka chini. Joka nalo hilo likanifikia.
Likaachama mdomo wake mkubwa.
Sasa nakufa! Nilikubali yaishe.
Achaaaaaa!! Nilipiga kelele za mwisho za kutokwa na roho. Huku nikitegemea zitakuwa kelele za mwisho. Haikuwa hivyo. Niliweza kuwa hai tena. Joka lilikuwa limeufumba mdomo wake. Likatulia tuli.
Nikaduwaa kulikoni nyoka huyu hajanimeza. Au! Au! …nikakosa majibu.
Joka likaendelea kutulia kama lina urafiki na mimi. Kwa uoga nikasimama na kuanza kutambaa taratibu. Joka limetulia halina habari. Nikasimama. Bado tuli! Nikaanza kuondoka hadi nikatokomea! Nyoka ametulia.
Maajabu makubwa sana haya!!

*****

Nilirejea hadi kule walipokuwa wanakijiji wenzangu. Osmani alikuwa amehitisha mkutano tena. Alionekana mwenye furaha sana na ni kama alikuwa anatoa karipio kali.
Samson niliyedhani amekufa kumbe alikuwa amezimia tu baada ya kutemwa na yule nyoka. Nilimkuta akiwa amefungwa kamba nyingi sana. Bila shaka adhabu yake ilikuwa imewadia.
Nilimuona Jesca pia. Lakini John pekee ndio nilikuwa sijamuona.
Nilikuwa na hasira. Nikatumia ule mwanya wa joka kutulia. Nikamvamia Osmani. Nikamkaba tena. Safari hii sikutaka mambo mengi sana, nilihitaji njia ya kutokea.
“Wakati wa kuwa watumwa wa shetani umekwisha. Tunatakiwa kusihi maisha yetu tuliyoshi awali. Manyanyaso haya yote na yasiendelee. Tusikubali kabisa uonevu huu. Sasa tunatoka humu. Kila mwenye nia na aungane nami sasa. Tunatokaa!!” niliunguruma kwa sauti kuu. Wale wasiokuwa na Chapa walinisikia na kuniona. Wale waliokuwanayo waliduwaa wasijue kinachoendelea.
Samson alifunguliwa kamba alizokuwa amefungwa. Sasa Osmani akawa anatuongoza kuielekea njia ya kutokea.
Chapa ya 666 ilikuwa katika mkono wake wa kuume.
Kijiji kilikuwa kikubwa sana. Tulipenyeza njia hadi njia bado hatukufika tulipokuwa tunahitaji.
Sasa tulifika mahali palipokuwa na majani makavu lakini laini sana. Tulipokuwa pale. Osmani akaniponyoka. Kisha akapiga mluzi fulani hivi. Wakatokeza kenge wa ajabu. Wakubwa kama mamba. Walikuwa wanne. Na dhahiri walikuwa na njaa. Walishambulia katika namna yha ajabu na upesi sana.
Waliua! Watu kumi wakaanguka chini. Mamba wale badala ya kula nyama wakawa wananyonya damu.
Ilikuwa zamu yangu sasa. Osmani alikuwa pembeni akitucheka. Kuna unga fulani alijipaka usoni, sasa aliweza kuniona vizuri.
“Achaaaa!!” nilijikuta natamka neno lililoniokoa midomoni mwa joka lile kuu. Kenge hawa wa ajabu wakatulia palepale wakafunga vinywa vyao. Osmani akashangaa na mimi pia nikashangaa.
Samson ambaye naye alikuwa amekata tamaa alishangaa.
Nikawahi kuipoteza hali yangu ya kushangaa. Nikamwendea Osmani. Nikamkaba tena. Nikampiga makofi mawili akaanza kutema damu.
“Njia ya kutokea!!” niliamuru.
Akageuka, akatunyooshea mkono. Palikuwa na mlango mdogo wa mbao zilizooza. Nikawaamuru wanakijiji wsaliosalia wapite. Wakapita!!
Hadi walipomalizika ndipo mimi na Osmani tulipita. Kabla hatujamaliza kupitia nilisikia kilio kikubwa. Kuna mtu alikuwa akiniita.
Sauti ile ilikuwa ya John!
Nikasita kutoka. Nikarejea nyuma niweze kuchungulia.
John alikuwa anagalagazwa na lile joka kubwa.
Huruma ya mapenzi yangu kwa John ikanijia. Nikaweka kando yote aliyowahi kunitendea. Nikarudi kwa kasi. Neno acha likiwa mdomoni mwangu. N ilipofika nikaamuru kwa sauti kuu. Joka lile likatii kwa nidhamu. Nikaduwaa. Nikamchukua John na kuanza tena kuitafuta njia ya kutokea.
Kosa kubwa! Nilimuacha mbali waziri wa miundombinu!
Osmani akawa amepotea! Sikujua ni wapi pa kupita.
John hakuwa akiniona wala kunisikia. Nilitamani ajue ni mimi nipo naye. Lakini haikuwa hivyo.
Nilifanikiwa kukipata kisu. Nikaamini sasa nitaiondoa alama ya 666 katika mwili wake na ataweza tena kuona.\
Hofu! Na kukata tamaa. John alikuwa na alama ile shingoni mwake. Mwili ukafadhaika.
Siwezi kumchinja John!! Siwezi!! Niliapa.
Lakini nitafanya nini sasa.
Kitu kama tetemeko la ardhi likatwaa mawazo yangu. Nikamvuta John asiyejielewa nikamkumbatia. Tetemeko hilo lilivyopita hapakuwa tena na lile joka.
Lakini kitu kipya kikajitokeza. Ulikuwa mwanga mkali kama jua vile!! Nikatafakari ni kitu gani hicho. Sikuweza kutambua.
Mara ule mwanga ukapotea. Nikasja kushtuka nimepigwa kibao katika shavu langu. Nikaanguka.
Niliposimama nikapigwa tena, na sikumjuona kiumbe aliyekuwa ananifanyia hivyo.
Mapigo yakaongezeka. Nikawa navuja damu.
Sikuweza kusimama tena.

Sauti ya Jenipher ikanijia kichwani, “Ukinywa damu unakuwa kama wao!!”
Maneno hayo yakanifanya nipatwe na ari mpya. Nikatambaa nikamfikia John.
Badala ya kumchinja! Nitamnyonya damu walau kidogo tu.
Nikamfikia. Nikamkamata. Akaanguka chini, nikajirusha shingoni mwake. Nilipoifikia shingo yake nikamkumbuka yule mganga wa kinaijeria. Hapo sasa nikakumbuka sio mara yangu ya kwanza kunywa damu. Nikapenyeza meno yangu pale pale kwenye alama ya 666 aliyopigwa shingoni.
Damu ikaanza kutoka. Nikaimeza huku nikiwa nimeikunja sura yangu.
Nguvu za ajabu zikaniijia. Sasa niliweza kumuona adui yangu aliporejea tena. Alikuwa ni Dokta tuliyekutana katika mtandao, alikuwa ni Dokta Davis.

Alikuwa ananisogelea tena aweze kunipiga. Nikaudaka mkono wake. Akataka kujitoa hakuweza. Nikaweka sawa kisu changu nilichokuwa nimekificha kwa nyuma. Nikazamisha katika sehemu zake za siri huku nikipiga kelele.
Akaanguka chini na kuanza kujirusharusha.
Nikamkumbuka yule ninja wa kisukuma, Samson ambavyo hakuwa na huruma. Na mimi nikamuiga. Nikamrukia Davis na kuanza kumchoma visu.
Nilipoanza tu kumchoma kisu cha kwanza mambo yakawa tofauti na yule ninja wa kisukuma aliyekuwa akichoma kisu anaua hapo hapo...nikakumbwa na mfadhaiko mkubwa.
Oparesheni ukombozi ikaingia doa jingine!!

***ISABELA katika mapambano ana kwa ana na Davis. Je nini hatma!! na ni kipi kimetokea mbona amefadhaika

***Je? John ndio amekufa baada ya kung’atwa na Isabela.

No comments:

Post a Comment

Recent Posts