Thursday, December 13, 2012

SITAISAHAU facebook------- 17

 

 

MTUNZI: Emmy John P.

MAWASILIANO: 0654 960040

SEHEMU YA KUMI NA SABA

...

Haya yote niliyataka mwenyewe!! Sasa nikaanza kuhisi kuwa Davis hakuwa mtu mzuri kwangu!!

Davis ni MCHAWI!!!

Naenda kufanya mapenzi na mchawi!!

Ghafla nikaijiwa na kumbukumbuku za chapa ya shetani 666, niulipokumbuka hili nikakumbuka na mshahara wangu ulikuwa una hizi namba, hata simu ya Osmani nayo ina 666, Davis aliwahi kunitumia nauli nayo ilikuwa na 666 na sasa nipo katika chumba namba 66 namsubiri huyu mfalme wa 666

Hapana! Hapana! Niliipinga nafsi yangu. Na sasa nilikuwa nimeamua kumkimbia mchawi huyu. Kuikimbia chapa ya shetani!!!

Nikiwa najiandaa kukimbia

.Mlango ukafunguliwa!!!

NANI AMEUFUNGUA MLANGO!!!

JE ISABELA ATAIKIMBIA CHAPA HII 666.

Kama akiikimbia je ndo anaruhusu MAMA YAKE afe!! NANI KAMA MAMA???


ENDELEA

Nilipokishika kitasa ili kuufungua nitoke nikakumbwa na kihoro! Mlango ukafunguka kama vile ulikuwa katika kungojea amri yangu!!
Niliamini kabisa si muhudumu anayeweza kuingia katika chumba cha mteja bila ruhusa. Kwa hiyo kama sio muhudumu basi angekuwa Dokta.
Hakika. Alikuwa ni yeye! Nikatazamana naye ana kwa ana, akapiga hatua mbili akawa ameingia vyema ndani ya chumba. Akaufunga mlango.
Alitaka kuongea jambo lakini mlango ukagongwa tena, akasita kisha akaufungua! Alikuwa muhudumu.
"Barcadi, na Sprite!" aliagiza Davis bila kutoa malipo ya awali. Vinywaji alivyoagiza nilijua fika ni kwa ajili yangu na yeye!
Mlango ukafungwa tena.
Sasa aliufunga na funguo kisha akaziacha pale mlangoni zikining'inia.
Mimi nilikuwa wima mkoba begani nikitetemeka.
Davis akaliendea kochi kubwa hapo chumbani akaketi.
Kisha kwa ishara akaniita!
Naitwa na shetani! Nilihamaki. Nikasita kwenda.
"Hautaki?" aliuliza, sikumjibu!
Akaitwaa simu yake kubwa ya kisasa.
"Tabasamu kidogo nikupige picha Bela?" alinishawishi. Sikushawishika.
Alipochoka kunichekesha nisiyecheka akatoweka na kwenda bafuni. Nikabaki chumbani peke yangu! Hapo likanivamia ghafla wazo la kutoroka! Funguo zilikuwa mlangoni! Kwanini nisikimbie? Nilijiuliza. Hapo sasa ndipo nikagundua kwanini sina ubavu wa kukimbia. Huyu bwana alikuwa anahodhi maisha ya mama yangu! Mwalimu Nchimbi.
Nilipotambua hilo nikafadhaika. Nikakiendea kitanda nikajitupa, nikautupa na mkoba wangu!
Ilikuwa lazima nifanye mapenzi na Davis ili kuokoa maisha yake.
Nilifadhaika bila kujua nini la kufanya.
Mlango wa maliwatoni ukafunguliwa. Kichwa kilikuwa kizito hata kunyanyuka kushuhudia ni kimbwanga gani kipya atakizua Dokta huyu!
Akajikoholesha kama anayerekebisha koo. Nikaijua nia yake! Nikanyanyua kidogo! Macho wazi!! Yowe la uoga likanitoka kwa nilichokiona.
Hili lilikuwa kubwa kupita yote!
Kilichokuwa mbele yangu ni kiumbe kile kile kinachoitwa Davis.
Lakini sasa hakuwa na nguo. Maungo yake yote yakawa yananidhihaki, japo alikuwa mweusi tii. Lakini ule mwanga pale ndani uliniwezesha kutambua kuwa alikuwa amelowana damu katika viungo vyake vya uzazi, na hiyo damu ilikuwa mbichi na ni kama ilikuwa inaendelea kumtoka lakini ajabu haikuwa inadondoka katika marumaru!
Hapa sasa nilimsahau kwa muda mwalimu Nchimbi, nikauacha mkoba nikakimbilia mlangoni.
Ajabu! Ule funguo haukuwepo tena mahala pake!
Dokta akacheka sana huku akinifuata kwa hatua ndogo ndogo!
Nilitegemea huenda nitapoteza fahamu. Lakini hiyo haikutokea niliendelea kushuhudia kiumbe huyu akinifuata.
Nikawa narudi kinyumenyume hadi nikafika mwisho. Davis akazidi kunisogelea. Sasa alikuwa amenifikia!
Akanishika mkono! Kiganja chake kilikuwa cha baridi sana!! Akanitazama usoni, nami nikamtazama. Akaniachia kisha akasonya kwa dharau. Akakiendea kitanda akajirusha pale!
Bado mashuka hayakuchafuliwa na damu mbichi.
Hakika sikuwa tayari kufanya mapenzi na kiumbe kile cha ajabu!! Niliapa!
Muwasho ulianza kama wa kawaida tu katika chuchu yangu moja, nikajikuna, muwasho ukapita.Mara ile chuchu ya pili nayo ikawasha nikaikuna ikatulia.
Sasa zikawa zinawasha zote kwa pamoja, muwasho usiofanana na ule wa kumwagiwa upupu. Huu ulikuwa wa tofauti. Nikatazama kitandani yule Dokta alikuwa amesinzia. Nikaitoa Sidiria yangu ili nijikune vizuri. Nikabaki bila nguo kwa juu. Nikafanya jitihada za kujikuna!! Ile hali ya kujikuna ikautwaa uoga wangu nikahamia katika hisia za raha! Raha ya kujipapasa! Mazito!
Ni heri ningekuwa na mikono mitatu huenda ningeweza kuipinga hali hii. Maana sasa kati kati ya mapaja muwasho ukazaliwa. Niache wapi? Nikune wapi? Nikajiuliza.
Raha ikawa karaha!
Nikaanza kulia huku nagalagala chini. Nilijikunja na kujikukunjua bila mafanikio!
Nilihitaji msaada wa hali ya juu! Msaada wa kukunwa!
Mara kama ameshtuka ndotoni yule kiumbe pale kitandani aligutuka. Akasimama akanitazama kisha akachuchumaa. Akanisogelea karibu zaidi. Sikuwa na nguvu mwilini.
Hakuwa na nguo nami sikuwa na nguo!
Kama vile alijua ninapowashwa! Akaanza kunikuna kwa namna ya kupapasa! Nikahisi raha ya kipekee ambayo sijawahi kuipata duniani. Bila kujitambua nikamkumbatia Dokta Davis.
Akaendelea kunikuna! Sasa nilikuwa hoi.
Fanya unalotaka! Ndivyo ningeweza kusema kama angeniuliza.
Lakini hakuniuliza!
Nikajikuta katika ulimwengu wa mahaba mazito!
Kama kukunwa hakika nilipata mkunaji! Muwasho ukatoweka kabisa. Jasho mwili mzima.
Nikapitiwa na usingizi kutokana na uchovu.

*****

Saa kumi na moja alfajiri hapakuwa na Dokta wala nguo zake pale ndani. Nilikuwa peke yangu.
Maumivu kifuani kama niliegemezewa gogo! Maumivu haya yakanikumbusha ndoto za kuota nazini na gogo!
Nikashtuka! Mbio mbio bafuni nikatapika!
Kumbukumbu ya kufanya mapenzi na Davis usiku uliopita ilinijia kichwani!
Yupo wapi sasa shetani yule? Nilijiuliza.
Ile hali ya maungo ya Davis kuwa na damu ilinisisimua na kujiona kuwa sina thamani tena ulimwenguni.
Kama sina thamani, bora nife! Niliamua!
Nitakufa vipi sasa? Hilo likawa swali la kujiuliza.
Nikayakumbuka maneno ya dada Suzi. Kuhusu utoaji mimba na madhara yake!
Nikafikia maamuzi ya kutoa mimba! Kisha nitajua nini cha kufanya!

Wakati natoka pale chumbani na kupita mapokezi nilikumbana na swali, "mwenzako bado yupo? Maana tunataka kufanya usafi". Mwenzangu? Mwenzangu nani? Wanamaamisha Dokta Davis.
Sikuwajibu nikajongea na kupotea eneo lile.
Nikaamua kurejea nyumbani kwangu. Tayari nilikuwa na taarifa kuwa mama anaendelea vizuri kiafya!

Tumbo! Tumbo! Tumbo lilianza ghafla kuniuma, upande wa kushoto!! Nililalamika sana, dereva wa teksi akaegesha pembeni akaniuliza kulikoni.
“Nipeleke hopitali!! Nipeleke nitakulipa” nilimsihi huku nikizidi kuugulia.
Kama nilivyoomba akaendesha hadi hospitali iliyokuwa jirani. Alikuwa ni kati ya masalia ya watu wakarimu waliobaki hapa duniani. Aliwahi kuwaita manesi. Japo walichelewa lakini walikuwa kunibeba kutoka ndani ya gari lile.
Moja kwa moja nikakimbizwa wodi ya wanawake!!
Nikapatiwa huduma ya kwanza!!
Baada ya muda damu ikaanza kunitoka!! Nilikuwa nimeingia katika siku zangu ama? Nilijiuliza bila kupata majibu!! Mjamzito naingia katika siku zangu!!
Kadri damu ilivyokuwa inavuja ndivyo maumivu yalizidi kupungua na hatimaye kuisha kabisa.
Majibu ya daktari yalikuwa kwamba. Ni tatizo la kawaida tu kwa mwanamke kuumwa tumbo akiwa anaingia katika siku zake. Lakini mimi nilikuwa mjamzito sasa!! Au mimba imetoka.
Sikutaka kuondoka na dukuduku. Nilimvuta daktari tukazungumza kinagaubaga.
Akafikia hatua ya kunipima ujauzito!!

Hakuchukua muda mrefu akarejea.
Alikuwa hajachangamka na ni kama alikuwa na jambo anahitaji kunieleza.
“Ina miezi miwili sasa!!.” Alinieleza.
“Ni maajabu wewe kuingia katika siku zako!!” aliendelea. Mimi nikiwa msikilizaji.
“Kwa hiyo ni nini Dokta.”
“Rudi baada ya siku saba. Kama ikiendelea hivyo. Ama la basi utakuwa mshtuko tu.” Alimaliza.
Nikaondoka zangu huku nikiitazama dunia jinsi inavyonizomea.

****

Maria hakushangazwa na hali yangu ya kuvuja damu!! Aliamini ni kawaida tu kwa msichana. Hakujua kama nina mimba!!
Siri nikabaki nayo. Mimi na daktari!!
Siku ya kwanza, ya pili, ya tatu….damu zinaendelea kuvuja tena bila kukoma!!!! Kazi ikawa ipo kwangu kila mara kubadili nguo zangu.
Siku ya nne, ya tano….bado tatizo likawa lile lile. Mateso sasa!!! Mimba gani hii!!!
Sikuingoja siku ya saba ifike. Nikarejea hospitali.
Daktari alinipokea vizuri. Nikampa kwa siri kiasi fulani cha pesa ili aweze kunihudumia kwa upendeleo.
“Hadi leo bado damu inakutoka?” alishangaa daktari. Nikamthibitishia kuwa bado zinatoka tena mfululizo.
Akakuna kichwa chake chenye mvi nyingi kasha akahamia kidevuni. Na penyewe akajikuna kwa muda.
“Hebu njoo…” akanipeleka katika chumba kingine. Akanipima tena mimba.
Daktari akashtuka!!!
“Kwa mara ya kwanza katika miaka yangu 20 ya kazi!!!” alihamaki.
“Nini? Nini dokta.” Niliuliza.
“Wiki iliyopita ilikuwa na miezi mingapi vile.”
“Mitatu ulisema.”
“Sasa imefikaje miezi sita leo???” aliniuliza. Nikahisi kuzizima. Nikakaa chini!!!
Daktari naye alikuwa ana hofu!!

***ISABELA motto wa masikini anateseka!! Baada ya kufanya mapenzi na Davis Sasa anavuja damu.
***Nini kinamtokea msichana huyu…..
***Sasa MIMBA ina miezi sita…ndani ya wiki kadhaa….

NI KISA JUU YA KISA.

No comments:

Post a Comment

Recent Posts