Monday, November 19, 2012

SABABU ZINAZOSABABISHA WASICHANA KUINGIA KWENYE MAPENZI NA MTU ASIYEMPENDA

mara nyingi watu huwa wanajiuliza ni kwanini wasichana wengi ni rahisi kuingia kwenye mahusiano bila hata ya wao binafsi kupenda kuingia katika mahusiano hayo.

kwa uchunguzi wangu binafsi nimegundua sababu kuu nne ambazo wasichana hujikuta kwenye mahusiano ya mapenzi hata kama hawakupenda kuwa na huyo mtu aliyeko naye. katika sababu hizi haziaendani na sababu za kijamii, kiuchumi wala utamaduni wa eneo fulani bali ni sababu ambazo mara nyingi huwakuta wasichana wa rika na uwezo tofauti bila kujali kama ni masikini ama tajiri. Kwanza kabisa tuone sababu za msichana kutotaka kuwa kwenye mapenzi na mtu asiye mpenda.

1. UJASIRI

Msichana anaweza kuwa jasiri kuingia kwenye mahusiano ama kutoingia kwenye mahusiano. mara nyingi wasichana wanavaa ujasiri pale wanapokuwa wapo mbali na mvulana na kujiaminisha yakuwa akifika kwa mvulana na atamwambia kuwa sikutaki. Na mara nyingi kwa mtu ambaye hampendi na hatamani kuwa naye hata kidogo. hivyo anauvaa ujasiri wa kuongea kwa mvulana. kitendo cha msichana kuvaa ujasiri akiwa kwake I mean kabla ya kuonana na mvulana humpa sababu ya pili ambayo ni

2. KUJIAMINI

Msichana akiwa jasiri anaweza kujiamini ya kuwa akifika atamwambia ukweli na hivyo akiwa anaenda kukutana na huyo mvulana basi njia nzima anakuwa anajiamini kuwa akiwa jasri na kumweleza kuwa hampendi na hamtaki basi yule mvulana lazima atamwelewa. na sababu hiyo hata akiitwa kuwa aonane naye anakuwa anajiamini kuwa hiyo vita ataishinda.

Lakini tofauti na mategemeo, msichana hujikuta anaondokewa na ujasiri na kujikuta yupo mikononi mwa mtu ambaye alidhani hapo mwanzo hatakuwa naye na hii ni kwa sababu zifuatazo:

1. woga/fear

Msichana anakuwa anaingiwa na dalili za kuogopa kusema kile alichokipanga kukisema kwa mvulana na mara nyingi anapokutana naye uso kwa uso, tofauti na hata angemtumia sms ama kumpigia simu. anapatwa na wasiwasi mkubwa wa wapi aanzie kumweleza ya kuwa hampendi na hataki kuwa naye. na hali mara nyingi hutokea pale mvulana anapomnyima nafasi ya kujieleza msichana na kwa hiyo sababu huzaa zababu kubwa ambayo mara nyingi imekuwa tatizo kwa watoto wa kike. sababu hiyo ni

2. HURUMA


Msichana anapopatwa na woga anajikuta katika hali kumhurimia yule mvulana au mwanume ambaye amejieleza kwake kwa kiasi gani anaumia kadri ambavyo yeye msichana anavyoendelea kumkatalia ombi lake. na hii mara nyingi hutokea pale mwanaume/mvulana anapotumia maneno yakuuchoma moyo wa masichana. na point ya kuumia moyoni na kujiona ni mkosaji, msichana hujikuta akiwa katika majaribu makubwa, ujasiri na kujiamini unaondoka na woga na huruma huchukua nafasi na kujikuta yupo kwenye mikono ambayo mwanzoni alifikiri si salama na hawezi kuwa na mtu kama yule ila sasa tayri kazama.

MWISHO

kama kweli msichana huhitaji kuwa na mvulana fulani basi SIMAMIA HILO na usiruhusu woga wala huruma kuingia katikati.

No comments:

Post a Comment

Recent Posts