Tuesday, November 6, 2012

CHOZI LA FUKARA



Alistaajabu alipofungua nakuingia kwani hakukuta nguo zake yaani begi lake la nguo halikuwepo Jordan alijiuliza maswali mengi sana bila kupata jibu hakupata usingizi kwa usiku huo alitoka nje akichunguliachungulia labda angemuona au alichelewa kurudi lakini alikumbuka hata begi lake halikuwako. Jordan alisononeka sana moyoni mwake roho ilimuuma sana kwani alijua tayari amempoteza mpenzi wake ila hakutambua wapi amekwenda  hivyo alikaa tu ndani akilala akiwaza na kulia kwani alimpenda sana.


 Wiki mbili zilipita bila ya kumwona mpenzi wake ndipo akapata barua, aliichukua Na kuifungua haraka haraka Ili ajue kilichopo ndani ya barua hiyo ghafla machozi yakaanza kumtoka alilia Sana, alisononeka moyoni Na aliwaza kupita maelezo, alikumbuka alivyomwimbia siku akiondoka pia alikumbuka promise waliyowekeana ndipo moyo ulizidi kumuuma. Mchana kutwa hakula wala kufanya kazi bali alishinda nyumbani tu akiwa na mawazo pia majonzi ndipo rafiki yake ambaye walifanya kazi pamoja ya kuzoa taka alikuja kumsalimia baada ya kuona aonekani kijiweni “aha vipi mshikaji mbona upo hivi unaonekana kama moyoni unamajonzi niambie mbona huonekani kijiweni, niambie basi au kunakitu kimekugasi” rafiki yake alimuuliza baada ya kumkuta akiwa ameshika tama “aha we acha tu ndugu yangu kwa mkasa ulionikuta kwani ahaahh” Jordan alimueleza tangu alivyo ondoka na kwenda kijiji kuwataarifu wazazi juu ya kwenda kumtambulisha mpenzi wake na alivyo rudi hali aliyoikuta pia alimpatia barua iliasome iliyotoka kwa mpenzi wake wa rohoni ambayo aliipokea baada ya wiki kadhaa kupita. Ndipo rafiki yake huyo aitwaye Juma alichukuana kuanza kuisoma na ilikuwa imeandikwa hivi “ikufikie wangu mpenzi wa enzi mie kiafyai ni mzima natumaini nawe u mzima, dhumuni la barua hii ni kutaka nawe kujua ni nini hasa kisa na mkasa kilicho nishawishi mbali nawe kwenda kuishi siyo siri sikupenda kuishi hali ya umasikini ya chini sana kumbuka ufukara ndiyo umechangia hivyo ninatarajia kufunga pingu za maisha ili niishi maisha bora mazuri kama almasi na nimeweka kadi ya mualiko niyako fanya ima harusini uhudhurie ukipata nafasi”
 Juma alisoma barua hiyo naye machozi yalimlenga lenga kwa huzuni kwani aliumia sana moyoni akijihisi ni yeye, alimfariji rafiki yake akimuondoa mawazo lakini Jordan akuacha kuwaza juu ya tukio hilo lililotekea katika maisha yake. Siku zilisonga mbele na na hatimaye siku ya harusi ikawadia, Mercy and Moses wakiwa mbele ya kanisa Pembeni Mchungaji na watumishi pamoja na wapambe wa maharusi ambao ni Maria na Maico. Jordan alihudhuria bila kukosa Kwa uchungu alilia Sana alipomuona Mercy akimvisha Pete mwanaume huyo ambaye alionekana kigogo yaani tajiri Wakutupa, roho yake ilimuuma Sana alitoka nje Na kuzunguka nyuma ya kanisa kisha akaanza kulia, alijikaza kiume asitoe chozi lakini wapi alijikuta akilia kama mtoto mdogo. Baada ya ibada watu walitoka wakishangilia na kuanza kuelekea ukumbini, ndipo Jordani alipata muda wa kuongea na Mercy kwani alikuwa hajaingia bado kwenye gari. “Why Mercy? Ok ni uamuzi wako, basi naomba unipatie pete yangu niliyokuvisha wakati wa uchumba wetu” jordani aliongea kwa uchungu sana “ehee wewe usinitie majonzi saa hizi kaitafute mule ndani kwenye maboksi” alimjibu kwa dharau kisha alipanda gari na kuondoka zake. Jordan alirudi nyumbani akiwa na mawazo sana hivyo alipanda kitandani na kulala lakini hakupata usingizi kwa ajili ya mawazo aliyokuwa nayo aliwaza mengi sana ila alimuomba mungu ampatie roho ya kumsahau mwanamke huyo lakini pia aliwaza kuwa asingeweza kumsahau maisha yake yote. Aliendele na kazi zake za hapa na pale ndipo alijipati fedha kidogo na kuamua aende kumsalimu mama yake kipenzi. Hivyo siku iliyofuata alikuwa tayari amekwishafika jijini mwanza alipo mama yake kwani alikuwa amemmis sana. Alipofika alimkumbatia mama yake kwa furaha kisha kumpatia zawadia alizo mpelekea na alikaribishwa pia mama yake alifurahi sana. Baada ya kuabdili nguo na kupata msosi ndipo waliendelea na maongezi “yaani tulisubiri utuambie utakuja lini kutuletea mkwe maana si unajua nimekwisha zeeka tena nahitaji mjukuu haya mbona umekuja mwenyewe tena vipi?” “Yaliyo nisibu mama nayo makubwa kuliko, yalinisababisha nikawa sili silali ila namuomba mungu anifanye niwe msahaulifu, Mercy nilimpenda toka moyoni mwangu na naamini alinipenda ila jua mama tama ya pesa ndiyo inayoharibu mapenzi ya watu na samaki mdogo mkunje kabla hajakuwa chatu, pia nimeamini kuwa fukara hana sauti hana uwezo wa kueleza hisia zake tokana na umasikini wake.  Baada ya maongezi Jordan alikwenda kujipumzisha kwani alikuwa amechoka kwa safari ya aliyokuwa ametoka. Siku iliyofuata kaka Kelvin alikuja kuwasalimu na kwa bahati alimkuta Jordan naye alikuwa amefika “ahha my young brother upo” “mie nipo tu kaka yangu nitaenda wapi na maisha yenyewe ndo haya, Karibu tu kaka yangu” Jordan alimkaribisha “vipi tena kaka si uliniambia utakuwa umerekebisha mambo baada ya mwezi” “ahha nipe siku hizi mbili nitayakamata mapene kama sina akili nzuri” Kelvin alimjibu. Siku iliyofuata Kelvin aliondoka asubuhi Na mapema kwani alikuwa Na appointment Na rafiki yake ambapo waliongoza wote mpaka mahali ambapo palijulikana Kama Kwa MTEMA NYOKA ambaye alikuwa Ni mganga, mchawi aliyetokea Nigeria. Waliingia hapo kwani walikuwa waeagiziwa kurudi siku hiyo “ahaaa!!! Kelvin Na Joshua karibuni Sana ahaaa ahaaa shiiiii ahhaaa, siku ndiyo hii unataka pesa, ahaaa utajiri ni wako ahhaaa Kelvin pesa sasa ni yako
Alisema mganga huyo ambaye alikuwa ameshika njiwa mweupe mkononi na kitambaa cheupe na chekundu mkononi mwake na sufuria nyenye maji yaliotiwa dawa kisha alimwambia Kelvin atenganishe kichwa na kiwiliwili cha mnyama huyo na kelvini alifanya kama alivyoambiwa na mganga huyo baada ya kutenganisha ndipo tone la damu lilidondokea juu ya maji na ghafla Kelvin aliona sura ya mama yake kwenye sufuria ile “what???? 

ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment

Recent Posts