Monday, October 29, 2012

CHOZI LA FUKARA

  

 
                   NA  DEARNA MAROTA
2
ILIPOISHIA>>>>>>>>

 Ilikuwa ni jumapili jioni ambapo jordani siku hiyo hakufanya kazi yoyote kwani ilikuwa siku ya kumcha bwana hivyo aliiheshimu. Baada ya kutoka katika ibada ya jioni alikuwa ameketi tu barabarani ambapo kulikuwa na kijiwe chake alichopumzikia pindi atokapo kwenye miangaiko ya hapa na pale, ndipo alikiwa kwenye dibwi la mawazo jinsi ya kukabiliana na hali ngumu ya maisha alishtushwa na sauti nyororo ya mrembo kwa nyuma yake “za jumapili kaka”


SASA ENDELEA

“aha salama tu Karibu dada yangu” aliitikia na kumkaribisha kisha aliketi “mbona una mawazo sana kaka yangu” dada huyo alihoji “aha ni maisha tu dada sijui unaitwa nani?” alijibu kisha alimuuliza swali “naitwa Mercy na wewe je waitwaje? Mrembo alihoji “naitwa Jordan ukiniita fukara haukosei” “ahaa usiseme hivyo Jordan kwanini unajiita fukara na umejaaliwa nguvu na uwezo wa kuifanya kazi  so usijali ipo siku mungu atakupa uwezo” Mercy alimfariji nao walibadilishana mawazo ya hapa na pale kwa na hapo ndipo ukawa mwanzo wa mahusiano yao na mwanadada huyo. Kwa uzuri Mercy alijaaliwa na mwenyezi kitu ambacho Jordan aliwaza moyoni kuwa ataweza kumtunza. Siku zilizidi kwenda na Mercy alishapajua nyumbani kwa jordani ambapo alikuwa amepangisha na mara kwa mara alilala hapo na Jordan. Kadri siku zilivyozidi kwenda ndipo mapenzi ya wawili hao yalishamiri na walipendana kupita maelezo. Lakini kwa upande wa Jordan hakuacha kumkumbuka mama yake kwani ndiye alimpenda kuliko kitu chochote. Waliishi hivyo hivyo kwa kubangaiza kwa chakula, na matumizi madogo madogo na siku nyingine walikosa na waliishia kunywa maji.

Jordan:  mpenzi wangu maisha yangu ni ya shida sana tuvumilie naamini ipo siku mungu atatujalia moyo wangu umekuchangua wewe angalia usije kunisaliti, ukaniacha nikateseka katika nafsi yangu kwani ni wewe tu uliyemoyoni mwangu, vumilia mpenzi kwa leo tulale hivihivi ila kesho nitajitahidi tupate kitu japo cha kutafuna.
Mercy:  usijali mpenzi wangu hatakama nisipokula nikiwa na wewe najihisi nimeshiba ala tu nahitaji upendo wako kutoka moyoni mwako  nami naamini Mungu ndiye aliyekuchagua uwe mume wangu wa ndoa na endapo utanisaliti sitaona umuhimu wa kuishi katika dunia hii ya sasa kwani bila wewe najihisi bado sijakamilika hivyo promise me kama hutaniacha na niwe wako wa milele mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha
Jordan: I promise mpenzi wangu nitakupenda milele daima katika maisha yangu
Mercy: I promise
       Maisha yao yalizidi kusonga mbele na upendo wao ulizidi kipimo kwani walipendana kupita maelezo siku walipokosa nao walilala na njaa na siku waliyo pata nao walimshukuru Mungu kwa alicho wapatia. Jordan aliangaika mno ili kujikimu na ugumu huo wa maisha na kwa kipindi hivyo fedha ilimsaliti kabisa hadi alikosa kodi ya nyumba na walijikuta wakifukuza wasijue pa kwenda
Jordan: mpenzi wangu angalia hali tuliyo nayo tutakwenda wapi sasa” Jordan aliongea kwa unyonge akiwa amemkumbatia mpenzi wake wakiwa nje na mizigo ilikuwa imewazunguka wakishauriana wataelekea wapi. Walishauriana na wakaamua kwenda mjini kutafuta maisha yao nako walifikia kwa rafiki yake Mercy aitwaye Maria
  Walikaa hapo kwa wiki moja huku Jordan akijitafutia vibarua vya hapa na pale na baada ya wiki moja tayari alikuwa ameshapata fedha kidigo hivyo walipangisha chumba chao kama ilivyokuwa awali.
          Waliendelea kuishi kwa upendo usio na kifani na kila aliye waona mjini hapo aliwaonea vivu. Kwa kipindi chote hiki jordani hakuwahi kumtambulisha Mercy kwa mama yake wala ndugu yeyote kwani bado alikuwa hajajipanga na wakati anaondoka alimuaga mama yake kuwa hatamtupa bali kumkumbuka daima na angerudi kila mara kuangalia hali yake kwani kaka yake (Kelvin) alikuwa bize na miangaiko yake hivyo alimkumbuka kwa nadra sana. Waliishi kwa muda mrefu na hali yao kimaisha ilikuwa palepale. Wakati Jordan alienda kwenye miangaiko yake na Mercy alibaki nyumbani kwa usafi wa mazingira na shughuli ndogondogo za nyumbani hapo lakini siku ya jumamosi aliamua kwenda kwa rafiki yake Maria kumtembelea. Maria alikuwa na uwezo kiasi fulani “aha Karibu shostito wangu” maria alimkaribisha “asante yaani nimekumisi shost” “aha wewe si utaki kuja kunitembelea na unakaa hapahapa mjini, utadhani tumegombana” maria aliongea na kisha kwenda kumchukulia juice ya matunda “ehe nipe mastory” maria aliongea kisha kuketi kwenye kochi “nina story gani bwana zaidi ya kuja kukusalimia na unipe ela ya mboga maana leo hata sijui nita kula nini” aliongea Mercy
“Mhh!! Ahaa, hivi Mercy rafiki yangu mbona hujielewi elewi” Maria aliongea kwa kejeli “kwanini” mercy alihoji

Je Rafiki yake Mercy anamshangaa nini Mecry?? fuatiolia .............

No comments:

Post a Comment

Recent Posts