Friday, October 26, 2012

CHOZI LA FUKARA

NA  DEARNA MAROTA

Mungu mwenyezi ni mkuu aliyeweza kuwaumba binadamu kwa mfano wake lakini kwa wepesi na ugumu wa nafsi tofauti tofauti. Mwanadamu huweza kutoa chozi lake kwa hisia tofauti: - machozi ya furaha na machozi ya uchungu. Chozi litokalo kwa uchungu wa jambo fulani huwa ni pigo lililo na pengo ndani ya moyo wa mwanadamu, CHOZI LA FUKARA ni story ambayo inaelezea jinsi masikini anavyo nyanyaswa na penzi kutokana na UFUKARA wake, na kujihisi hana nafasi ya kueleza hisia zake kwa mtu ampendaye kutokana na umasikini wake.
   “mwanzo wa mapenzi huwa matamu zaidi ya asali na mwisho wa kulishamirisha huwa kama shubiri iliyotiwa pilipili kichaa iliyo mbichi haswaaaa, kwa fukara kama mimi kwani penzi limeweza kunitoa chozi na pia kuninyanyasa katika nafsi yangu pia nikatambua fukara hana sauti” maneno haya yalitoka kinywani mwa Jordan ambaye ni kijana apatae miaka 30 kwa sasa na anafamilia hivyo ameamua kuelezea mikasa ya maisha yake na misukosuko ya mapenzi aliyopitia pindi alipokuwa masikini lakini mungu alikuwa pamoja nae mpaka kufikia hapo alipo sasa ndipo anaelezea kwa uchungu huku akivuta hisia na kumbukumbu ya mapito yake
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@------------------------- na mtunzi wako -----------------------------------
***************** ############################### %%%%%%%%%%%%%
 “Subira huvuta heri na Baraka kwa kila asubirie kwa heri kwani mungu hamtupi mja wake hata siku moja bali ukimtendea mwanadamu ubaya na mungu hukurudishia, malipo ni hapa duniani”
    Jordani ni kijana wa pili katika familia ya kimasikini aliyeishi na mzazi wake katika kijiji cha Bariadi mkoani mwanza. Kutokana na ugumu wa maisha ulipelekea Jordan na kaka yake aitwaye Kelvin kutokupata elimu ya mwangaza wa maisha yao ya baadaye kwani katika familia yao mlo wa siku tu waliupata kwa manati. Baba yao aliwatelekeza tangu wakiwa wadogo hivyo mama ndiye alikuwa na jukumu la kifamilia hiyo kwa muda huu Jordan alikuwa ni mwenye umri wa miaka 18 na Kelvin alikuwa na miaka 20. walifanya vibarua vya hapa na pale ili kupata fedha kwa ajili ya matumizi madogo madogo kama chakula, nguo za kubadili na vitu vinginevyo ili kumsaidia mama yao pia  ambaye alikuwa amedhoofika kiafya kutokana na mawazo aliyokuwa nayo kwa kipindi chote na misukosuko aliyopitia pindi alipokuwa akitafuta riziki kwa ajili ya watoto wake “kweli mama ni mama na hakuna mwingine kama mama” Jordan aliongea kisha aliendelea. Miaka ilizidi kusogea ndipo jordani alikuwa ni mwenye miaka 20 na alikuwa akifanya kazi ya kubeba taka na kupeleka katika dampo kuu la jijini mwaza pia alipokuwa na nafasi alichukua vibarua vya kuosha magari pindi alipoitajika na kazi hiyo ilimfanya apate vijisent kwa chakula chake mwenyewe na kidogo alimpelekea mama yake. Kwa kipindi hichi Jordan tayari alikuwa amepangisha chumba na alianza kujitegemea lakini kila siku alimwendea mama yake ili kumjulia hali. Mama yake aliwapenda sana tangu wakiwa wadogo lakini alizidisha upendo kwa Jordan kwani ndiye aliyemjali kuliko Kelvin lakini wote walimpenda mama yao sana kuliko kitu kingine.
Kwa upande wa Kelvin alipata marafiki ambao walikuwa wakifanya biashara za hapa na pale ili kujikomboa kimaisha.
       Ilikuwa ni jumapili jioni ambapo jordani siku hiyo hakufanya kazi yoyote kwani ilikuwa siku ya kumcha bwana hivyo aliiheshimu. Baada ya kutoka katika ibada ya jioni alikuwa ameketi tu barabarani ambapo kulikuwa na kijiwe chake alichopumzikia pindi atokapo kwenye miangaiko ya hapa na pale, ndipo alikiwa kwenye dibwi la mawazo jinsi ya kukabiliana na hali ngumu ya maisha alishtushwa na sauti nyororo ya mrembo kwa nyuma yake “za jumapili kaka” 
 
JE MREMBO HUYU NI NANI?? NA ANATAKA NINI??? ungana na mtunzi wako jumapili hii

No comments:

Post a Comment

Recent Posts