Thursday, April 11, 2013

FACEBOOK CHATTIN (SEASON TWO) -------------1



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.
MAHALI: DAR ES SALAAM.
SIMU: 0718 069 269

...
Unaikumbuka ile Season One niliyoandika kuhusiana mimi na msichana yule wa kishua? Leo hii nakuja na Season two ambayo itakuwa kali zaidi ya ile season one iliyopita. TWENDE PAMOJA.

Najisikia nimechoka sana huku laptop ikiwa mapajani mwangu na nimeunganisha na internet nikicheki updates za facebook, macho yangu yanakuwa mazito, natamani kulala lakini ghafla naliona jina, jina zuri la msichana mmoja hivi, jina la msichana ambaye nilikuwa namtaka kila siku toka kipindi kile alichokuwa akikaa mtaani kwetu. Ghafla uchovu wote ukanitoka, naanza kumwangalia, ndiye yeye, ndiye yeye kabisa kwani nilikuwa nimemtumia friend request jana tu, leo kanikubali kuwa rafiki yake, halafu yupo online.

Kwanza nasita kumpa hi, hii ni kwa sababu katika kipindi ambacho alikuwa akiishi mtaani kwetu, alikuwa akiringa sana kutokana na urembo wake, nilikuwa nimemtaka mahusiano ya kimapenzi zaidi ya mara saba, zote alinipiga mbavuni. Leo hii, huyu msichana Dorcas kanikubalia urafiki, lazima nianze upya mpaka anikubalie bila kujua mimi ndiye yule yule ambaye alikuwa akinikataa sana. Kwa kuwa katika kipindi hicho nilikuwa ninatumia a.k.a ya jina langu kama BROTHER PRINCE, hakuweza kunitambua. Ninamfuata na kumpa hi

MIMI: Mambo mrembo! (Nilimsalimia kwa kujiamini)
DORCAS: Poa. Mzima Brother?
MIMI: Nipo poa sana. Asante sana.
DORCAS: Asante ya nini tena? (Aliuliza huku nikiona kabisa swali lake dizaini kama lilikuja na tabasamu pana)
MIMI: Kwa kunikubalia urafiki. Nimefurahi sana.
DORCAS: Usijali Brother.

Kwanza hapo nikakaa kimya, sikujua ilitakiwa niendelee vipi na mawasiliano nae, kwa dakika kadhaa, vidole vyangu vikabaki kwenye keyboard ya laptop bila kuandika chochote kile. Kuna kitu nikatokea kukikumbuka, nikaona ngoja kwanza niende kuangalia picha zake.
Asikwambie mtu, alikuwa Dorcas yule yule, msichana ambaye alinifanya niwe kama chizi mtaani kwetu, msichana ambaye alinifanya niumwe na mbu sana vichochoroni, msichana ambaye alinifanya niwe namsubiria sana kumsindikiza shuleni kwao huku nikiwa radhi nichelewe shuleni kwetu.

MIMI: Dorcas......! (Niliita kwa mwandiko wa kioga)
DORCAS (Baada ya dakika mbili): Abeeee.
MIMI: Upo bize sana?
DORCAS: Sio sana. Ila kwa nini umeuliza hivyo?
MIMI: Nimeona nimekuandikia meseji halafu unanijibu baada ya dakika mbili kupita. Kweli haki hii jamani?
DORCAS:Samahani. Unajua ninachati na watu wengi ndio maana.
MIMI: Au kwa sababu mimi ni mgeni kwako?
DORCAS: Hapana jamaniiiii. Nisamehe basi.
MIMI: Usijali. Naweza kukuuliza swali moja la kizushi?
DORCAS: Swali gani?
MIMI: Lakini haujanijibu.
DORCAS: Sawa. Uliza.
MIMI: Unaishi wapi?
DORCAS: Jamani ndio swali gani tena hilo. Si kila kitu nimeandika kwenye profile langu uangalie.
MIMI: Ninatamani sana kufanya hivyo. Mtu anapouliza swali hili si kwamba siwezi kuangalia, hapana. Internet zetu kwa sisi tunaotumia simu huwa hazina kasi kabisa na ndio maana nimeona bora nikuulize tu.
DORCAS: Kwa hiyo hapo unatumia simu?
MIMI: Yeah! (Nilidanganya)
DORCAS: Mmmh!
MIMI: Mbona unaguna?
DORCAS:Nakuona online.
MIMI: Hilo si tatizo. Natumia Opera Min mpya. Naomba unijibu.
DORCAS: Naishi Magomeni.
MIMI: Ila si unafahamu kama ni kubwa sana.
DORCAS: Nipo Mapipa.
MIMI: Sawa. Nashukuru kwa kukufahamu. Naomba tuwe tunachati kila tunapokutana online.
DORCAS: Usijali. Karibu sana.
MIMI: Poa.
DORCAS: Na wewe unaishi wapi?
MIMI: Naishi Manzese Midizini (Nilidanganya kwani ningesema kweli, angehisi kitu).
DORCAS: Owkey. Unasoma?
MIMI: Nimekwishamaliza kidato cha sita (Nilidanganya tena)
DORCAS: Shule gani?”
MIMI: Makongo.
DORCAS: Hongera.
MIMI: Asante. Wewe unasoma?
DORCAS: Nasoma kidato cha tano ila mwezi wa pili mwishoni naingia kidato cha sita.
MIMI: Nawe hongera sana.
DORCAS: Asante. Naomba nikuulize swali jingine.
MIMI: Uliza tu.
DORCAS: Mbona haujaweka picha yoyote ile?

Swali hilo likanifanya kukaa kimya kwa muda fulani, halikuwa swali gumu kabisa na pia nilikuwa na picha nyingi sana kwenye mashine yangu ila yeye ndiye alikuwa miongoni mwa watu ambao sikutaka waone picha yangu yoyote ile. Kumbuka kwamba Dorcas nilikuwa nikimtaka toka alipokuwa akiishi mtaani kwetu Tandale, tena katika mara zote ambazo nilikuwa nikimtaka, alinikataa sana kiasi ambacho mpaka nikachoka. Leo hii Dorcas alikuwa hapa, ninachati nae moja kwa moja kupitia inbox. Sikuwa tayari kwa kipindi hicho kuweka picha zangu, nilitaka zibaki zile zile za wasanii wa Wamarekani.

DORCAS: Mbona kimya Brother?
MIMI: Sina picha. Ninatamani sana niweke picha ila tatizo simu yangu haina kamera. Ila usijali, ndani ya siku mbili, utaziona picha zangu.
DORCAS: Sawa. Nakwenda kulala. Tutachati kesho Brother Mungu akipenda.
MIMI: Mungu anapenda labda wewe usipende tu.
DORCAS: Hahaha!
MIMI: Huo ndio ukweli.
DORCAS: Basi sawa mimi nakwenda kulala.
MIMI: Usijali. Wape hi wote.
DORCAS: Wa kina nani?
MIMI: Utakaowaota.
DORCAS: Na kama nikikuota wewe?
MIMI: Nipe Hi tu. Ila kumbuka kwamba ukiniota, nami nitakuota, na kama tukiotana basi hiyo inamaanisha tumemisiana.
DORCAS: Hahaha! Una maneno Brother.
MIMI: Napenda kuongea tu. Ila usijali. Usiku mwema Dory.
DORCAS: Nawe pia (Akaenda offline)

Kuanzia hapo nikawa na amani. Muda wote nilikuwa nikishukuru sana kwa Mungu kwa sababu alikuwa amenipa uwezo mkubwa sana wa kuandika kiasi ambacho uwezo ule nilikuwa nautumia kwenye chatting kiasi ambacho ulionekana kuwa mzuri sana.
Huyu Dorcas nilikuwa namtaka sana, tena nilikuwa namtaka kuliko wasichana wote. Japokuwa zamani alikuwa akinikataa lakini nilikuwa nimekwishaapa kwa marafiki zangu kwamba ilikuwa ni lazima nimpate. Wengi walinicheka kidharau kwa kuniona najisumbua, hata alipohama nilichekwa sana kwa kuonwa kwamba sikuwa nimekamilisha lengo langu.
Leo hii, vita vya chini chini vimeanza, vita ambavyo sitotaka kuwaambia marafiki zangu mpaka pale ambapo ningekamilisha ‘mission’ yangu na kuwa nae. Hebu jifikirie kwanza, Dorcas angetoka vipi? Angeweza kuanzia wapi kunikataa na wakati nilikuwa na maneno mengi ya kuandika? Sikuona angetokea wapi, ila kama atanikubali, siku ya kuonana sijui ingekuaje kama atagundua kwamba ni mimi atafanyaje? Ila hiyo sio ishu, ishu kubwa ni kumfanya aangukie kimapenzi kwenye mikono yangu iliyo salama juu ya maisha yake......thats all.

MIMI: (Nikalog out na kulala huku nikisubiri kesho nianze pale nilipoishia)


Itaendelea kesho.

Tuesday, April 9, 2013

FACEBOOK CHATTING============== 5

 

 MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269




MSICHANA: Ndio najiandaa mpenzi. Unataka nivae mavazi gani?
MIMI: Vyovyote tu. Ila sipendelei kukuona ukivaa suruali.
MSICHANA: Kwa nini?
MIMI: Sina sababu.
MSICHANA: Basi usijali. Nitavaa gauni moja zuri sana ambazlo nilinunuliwa na baba katika moja ya maduka makubwa jijini New York. Nitakuja nalo huko.
MIMI: Poa. Wewe njoo tu mpenzi.
MSICHANA: Ili uwahi, naomba ufanye kitu kimoja.
MIMI: Kipi?
MSICHANA: Kodi bajaji na hela nitalipia mimi huku.
MIMI: Poa. Ila usiniingize choo cha kike.
MSICHANA: Usijali mpenzi.

Nikaanza kujiandaa kwa haraka sana, japokuwa toka nizaliwe sikuwahi kufika mapema sehemu ya appointment ila siku hiyo nilitaka kufika mapema sana. Nilipomaliza kujiandaa, nikaanza kwenda kwenye maegesho ya madereva wa mabajaji ambako nikamuita rafiki yangu ambaye alikuwa akiendesha bajaji moja.

MIMI: Sikiliza Moody, nataka unipeleke Slipway. Kiasi gani?
MOODY: Du! Unakwenda kufanya nini tena?
MIMI: Achana na hayo. Kiasi gani?
MOODY: Elfu kumi.
MIMI: Poa. Ila naomba tufanye kitu kimoja.
MOODY: Kitu gani?
MIMI: Tukifika kule, sema gharama ni shilingi elfu ishirini na tano. Umesikia?
MOODY: Poa. Kwani kuna mtu anakulipia?
MIMI: Yeah! Mtoto fulani wa kishua.
MOODY: Poa jembe. Ingia twende.

Nikaingia ndani ya bajaji na safari ya kuelekea Slipway kuanza. Ndani ya bajaji bado nilikuwa nikiendelea kuchati nae huku akiniambia kwamba amekwishafika na ni mimi tu ndiye nilikuwa nikisubiriwa.

MIMI: Sasa hiyo elfu ishirini na tano, yako elfu kumi na yangu elfu kumi na tano. Nitaifuata baadae nikitoka kuonana nae. Umenielewa?
MOODY: Du! Yaani hata hauniongezi kwa mchongo ninaoucheza?
MIMI: Nikuongeze nini hapo? Kwanza bei yenyewe tu umenibamiza. Halafu kama ningetaka si ningechukua daladala kwa nauli ya shilingi mia tatu na ningefika Msasani ningepiga kwa mguu mpaka Slipway.
MOODY: Dah! Poa bwana. Mara ya kwanza nilitaka kushangaa eti unakodi bajaji. Mtoto wa uswahilini akodi bajaji!
MIMI: Ndio hivyo bwana. Yaani hapa najiona kupata zali sana.

Safari ilikuwa ikiendelea zaidi na zaidi mpaka tulipofika Slipway. Gari nzuri na ya kifahari ilikuwa imepaki nje. Mara msichana yule akateremka. Nikajikuta nikianza kutetemeka kupita kawaida, sikuamini, sikuamini kama duniani kulikuwa na msichana mzuri namna ile. Nilibaki kimya nikimwangalia kwa mshangao. SI mimi tu, hata Moody alikuwa akionekana kushangaa. Uzuri wa msichana yule ulinishtua kupita kawaida.

MSICHANA: Vipi mpenzi?
MIMI: Poa
MSICHANA: Ngoja nimlipe dereva.

Akaanza kuisogeea bajaji na kisha kumlipa Moody gharama zake. Sikutaka kuzubaa, nami nikaelekea pale pale kuona anamlipa kiasi gani ili baadae Moody asije akanigeuka. Nikaona wekundu wawili na elfu tano wakitoka kwenye pochi yake, nikaona kwa ushahidi ule Moody asingeweza kunizika.
Tukatoka hapo na kuelekea ndani. Ingawa mule ndani kulikuwa na warembo wengi lakini mbele ya msichana yule wote walionekana kuwa si kitu. Tukatafuta sehemu na kukaa. Vinywaji na chakula vikaagizwa na kuanza kula.

MSICHANA: Tukitoka hapa nataka twende tukapumzike kwenye chumba chochote kile.
MIMI: Sawa. Ila jina lako hasa ni nani manake naona kwenye facebook unatumia jina la Precious Angel.
MSICHANA: Naitwa Angeline.
MIMI: Ok!

Tukala na kuanza kwenda katika sehemu iliyokuwa na vyumba na kuchukua chumba kimoja. Tulipoingia ndani, akaanza kuvua nguo zake na mimi kuvua zangu. Akajilaza kitandani huku akiniangalia kwa macho ya kurembua. Nami sikutaka kuchelewa, ninaanza kumsogelea. Nikaanza kumwangalia usoni.

GIDEON: Nyemo....Nyemo...Nyemo...amka.

Ilikuwa ni sauti ya kaka yangu ambayo ilikuwa ikisikika kwa mbali huku akiugonga mlango wa chumbani kwangu. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo nilivyozidi kuisikia sauti ile. Ghafla nikaamka kutoka usingizini. Mungu wangu! Kumbe matukio yote yale ambayo yalikuwa yakiendelea ilikuwa ni ndoto. Nikaamka, nikabaki kimya kitandani, sikuamini.

MIMI: Ndoto! Mungu wangu! Kumbe ilikuwa ndoto! Damn!

Nikasimama na kwenda kuufungua mlango wa chumbani kwangu, kaka yangu, Gideon alikuwa amesimama mlangoni. Nilikuwa nimechukia kupita kawaida.

GIDEON: Rafiki yako amekuja kukuulizia.
MIMI: Nani?
GIDEON: George Iron Mosenya
MIMI: Aaaggghhh! Kwa nini usingengoja hata kwa dakika moja.
GIDEON: Kuna nini?
MIMI: Dah! Nilikuwa chumbani. Tena kila kitu kikiwa kwenye hatua ya mwisho kaka.
GIDEON: Mbona sikuelewi.
MIMI: Naomba modem yangu kwanza.

Gideon akanipa modem yangu na kisha kuanza kurudi chumbani. Nikachukua laptop ambayo ilikuwa juu ya dressing table, nikaiwasha na kisha kuchomeka modem ile, nikaoganisha na internet na kufungua mtandao wa Facebook.

MIMI: Anaitwa Angeline.

Nikaanza kuwaangalia marafiki zangu wote huku nikimtafuta huyo msichana mwenye jina la Angeline. Sikuwa na rafiki huyo kabisa kitu kilichonipelekea kuanza kulitafuta. Majina yote yalikuja lakini hakukuwa na msichana yule, sura zao zilionekana kuwa tofauti kabisa na msichana yule mrembo. Sikutaka kuishia hapo, nikaanza kwenda kwenye akaunti zangu zote, twitter, myspace, beareshare, yahoo messenger lakini kote huko hakukuwa na msichana huyo.

MIMI: Mungu wangu! Kumbe alikuwa msichana wa ndoto! Kumbe nilikuwa nikiota. Ndoto....Ndoto! Kumbe ilikuwa ni ndoto! Nazichukia ndoto.

Nilijisemea huku nikionekana kukata tamaa. Sura ya msichana huyo bado itaendelea kubaki katika akili yangu, alikuwa ni msichana mzuri ambaye kila ninapowaangalia wasichana wote, hakukuwa na msichana ambaye alikuwa mzuri kama yeye. Miaka miwili imepita tangu niote ndoto hiyo lakini kamwe sura ya msichana huyo haikuweza kuondoka kichwani mwangu, nilikuwa namkumbuka kwa kila kitu. Nimejaribu kwa muda mrefu sana kumtafuta kwenye mtandao wa facebook lakini wala sijafanikiwa kumuona. Angeline....Angeline ataendelea kubaki kwenye akili yangu, nitaendelea kumkumbuka kila siku.

N:B. Hadithi hii ni ya kutunga, haihusiani na tukio lolote. Asanteni kwa kunifuatilia kutoka mwanzo hadi mwisho. Kama kweli ulitokea kuipenda hadithi hii, naomba uniambie kwa kutumia LIKE yako na kama una chochote cha kusema, unaweza kucomment pia.

MWISHO

Je umeifurahia na mwisho kukuchekesha?
Basi LIKE.

LIKE zikiwa nyingi kama 300. Kesho naanza na CACEBOOK CHATTING SEASON 2.

Monday, April 8, 2013

RIWAYA: PAINFUL TRUTH (UKWELI WENYE KUUMA)

 MTUNZI: Nyemo Chilongani

MAWASILIANO: 0718 06 92 69


SEHEMU YA TANO

Happy alionekana kuchanganyikiwa, hakuamini kama kweli Wayne alikuwa akitoka chumbani kwake huku akionekana kuwa na hasira mara tu alipothubutu kumwambia kuhusiana na ule ujauzito ambao alikuwa nao. Mshtuko mkubwa ukampata moyoni mwake hali iliyompelekea kuinuka pale kitandani na kuanza kumfuata Wayne.
Wayne alikuwa akitembea kwa mwendo wa haraka haraka, Happy akajitahidi kukimbia kumfuata huku akiita lakini Wayne hakugeuka nyuma. Happy hakutaka kuendelea kumfuata Wayne, akasimama na kisha kuanza kulia.
Tukio lile ambalo lilikuwa limetokea lilikuwa limemuumiza moyoni mwake zaidi ya tukio lolote ambalo liliwahi kutokea maishani mwake. Akaanza kupiga hatua kurudi nyumbani kwao, macho yake yalikuwa yakitoa machozi mfululizo.
Mama yake na shangazi yake wakaonekana kushangaa, hawakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea mpaka Wayne kutoka chumbani mule na kuondoka huku akionekana kubadilika. Hapo ndipo Happy alipoamua kuwaambia kile ambacho kilikuwa kimetokea.
“Yaani amekataa mimba yake?” Bi Vanessa aliuliza huku akionekana kushtuka.
Happy hakujibu kitu, bado alikuwa akiendelea kulia mfululizo. Alihisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa na ncha kali ambacho kilikuwa kimeuchoma moyo wake. Hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya ili siku moja Wayne aamini kwamba mtoto yule alikuwa wake.
Happy akarudi chumbani na kujifungia, siku hiyo wala hakutaka kuongea na mtu yeyote yule, alikuwa akilia kwa uchungu. Kuna wakati alikuwa akinyamaza, ila kila alipokuwa akiliangalia tumbo lake, akaanza kulia zaidi na zaidi.
Mpaka katika kipindi ambacho mzee Lyimo alikuwa akitoka shambani na kuingia hapo nyumbani, bado Happy alikuwa amejifungia chumbani kwake. Alipopewa taarifa juu ya kilichoendelea, mzee Lyimo akaanza kupiga hatua kuufuata mlango wa kuingia chumbani kwa Happy.
Mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani, akaanza kugonga lakini wala haukufunguliwa kitu ambacho kilimfanya kuanza kuliita jina la Happy huku akiendelea kugonga. Hazikupita hata dakika nyingi, Happy akafungua mlango na mzee Lyimo kuingia.
Macho ya Happy yalikuwa mekundu huku yakiwa yamevimba hali iliyoonyesha kwamba alikuwa amelia kwa muda mrefu sana. Mzee Lyimo akakaa kitandani na kuanza kuongea nae. Moyo wa mzee Lyimo ulimuuma zaidi, kamwe hakutarajia kama mzungu Wayne angeweza kuikataa mimba ile.
“Haiwezekani. Ameikataa?” Mzee Lyimo aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio. Ameikataa” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akasimama na kutoka nje ya chumba kile. Akauona mwili wake ukiwa umekufa ganzi kabisa. Hakuaamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Happy, alitamani akutane na Wayne na kuongea nae ili aone kama alikuwa na ujasiri wa kuukataa ule ujauzito mbele ya macho yake.
Baada ya hapo, maisha ya Happy yakaendelea kama kawaida ingawa muda mwingi alikuwa akitawaliwa na huzuni. Alikuwa akijitahidi kula vyakula vizuri ambavyo vilikuwa vikimpa afya bora yeye pamoja na mtoto.
Mara kwa mara alikuwa akihudhuria kliniki kama ambavyo madaktari walivyotaka afanye. Kamwe hakulala katika kitanda kisichokuwa na neti, alikuwa akiyalinda maisha yake na ya mtoto wake ambaye alikuwa tumboni.
Ingawa ilikuwa ni vigumu sana lakini akaamua kujisahaulisha kuhusu Wayne, akaamua kuishi maisha yake peke yake, hakutamani kabisa kumuona Wayne mbele ya macho yake, alionekana kumchukia kuliko kiumbe chochote duniani.
Miezi tisa ikatimia na ndipo Happy akajifungulia shambani katika kipindi ambacho alikuwa akilima pamoja na wazazi wake hatua iliyowapelekea kumpeleka hospitalini.
Happy alikuwa amelala juu ya kitanda ndani ya chumba kimoja katika hospitali ya KCMC iliyokuwa Moshi mjini. Bado hakuwa ameongea kitu chochote kile. Dripu moja baada ya nyingine zilikuwa zikiingiza maji katika mishipa yake.
Happy alikuja kufumbua macho yake baada ya masaa nane kupita. Akayapeleka macho yake huku na kule, yakatua katika nyuso za wazazi wake. Tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakaanza kupiga hata kumfuata.
“Mtoto wangu yuko wapi?” Happy aliuliza kwa sauti ya chini.
“Kimaro. Tulikuja nae hapa. Amewekwa katika chumba maalumu” Mzee Lyimo alijibu.
“Silitaki jina hilo baba. Sitaki mtoto wangu aitwe Kimaro” Happy alisema kwa sauti ya chini.
“Sawa binti yangu. Unataka aitwe nani?”
“Aitwe Andy” Happy alijibu.
“Kwa hiyo aitwe Andy Wayne?”
“Hapana. Aitwe Andy Ryn. Hili ni jina la babu yake. Sitaki achukue jina la baba yake” Happy alisema.
Hicho ndicho kilichoamuliwa. Jina likawa limekwishapatikana. Baada ya siku mbili, Happy akaruhusiwa kurudi nyumbani. Kila wakati alikuwa pembeni ya mtoto wake, watu mitaani walikuwa wakishangaa namna mtoto yule alivyokuwa mweupe.
Afya yake ilikuwa bora hata zaidi ya watoto wengine ambao walikuwa wamezaliwa mitaani hapo. Happy alimthamini sana mtoto wake hata zaidi ya alivyojithamini yeye mwenye. Miezi ikakatika, Andy Ryn akaanza kujifunza kutembea.
Katika kila hatua ambayo alikuwa akiifikia, Happy alionekana kuwa na furaha. Ila kamwe hakuweza kumsahau Wayne kwani kadri alivyokuwa akimwangalia Andy, alifanana sana na baba yake. Mpaka katika kipindi hicho hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea katika maisha ya Wayne katika kipindi ambacho alikuwa ameondoka na kuelekea nchini Marekani.
Mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia na kupita, Wayne hakuwa ameonekana kabisa mbele ya macho yake. Mwaka wa tatu ukaingia na kupita na mwaka wa nne kuingia. Hapo ndipo Happy akaamua kumuanzisha Andy katika shule ya chekechea iliyokuwa hapo Machame.
“Atakuwa na akili kama za mama yake” Happy alijisemea huku akimvarisha Andy nguo tayari kwa kumuanzisha shule.
Katika kipindi ambacho Happy alikuwa akiingia shuleni hapo pamoja na mtoto wake, walimu wote wakaonekana kushangaa, mtoto wa Happy alionekana kuwa tofauti kabisa. Alikuwa ni mzungu kwa asilimia themanini huku ishirini zilizobaki akiwa amechukua asili ya mama yake.
Andy akaanza kusoma katika shule hiyo. Kwa siku ya kwanza tu aliyofika shuleni hapo, uwezo wake ulijionyesha wazi. Ingawa alikuwa na umri mdogo lakini alikuwa na uwezo mkubwa sana kiasi ambacho kila mwalimu alikuwa akishangaa.
“Mmmh! Huyu mtoto ni wa maajabu nini?” Mwalimu Nuru alimuuliza mwalimu Leonila ambaye nae alikuwa akishangaa tu.
“Wala sijui. Ila uwezo wake unanishangaza sana. Nimewahi kufundisha watoto zaidi ya elfu tano katika shule hii, lakini mtoto huyu ameonekana kuwa wa kipekee sana” Mwalimu Leonila alimjibu mwalimu Nuru.
Mwaka wa tano na wa sita ukaingia. Andy akaanzishwa darasa la kwanza katika shule ya Machame Primary School. Kila mwanafunzi alikuwa akimshangaa, hawakuwahi kumuona mtoto wa kizungu akiwa anasoma katika shule kama ile.
Maswali mengi yalikuwa yakimiminika vichwani mwa walimu wa shule hiyo asili halisi ya mtoto huyo. Kila mmoja alikuwa akiongea lake. Mpaka amefikisha miaka sita, hakukuwa na mtu ambaye alikuwa akifahamu kama Andy alikuwa mtoto wa Wayne ambaye alikuwa ameikataa mimba yake kipindi cha miaka sita iliyopita.
****
Ilikuwa ni taarifa mbaya ambayo ilikuwa imesikika masikioni mwa Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia. Waliiangalia simu ile ya mezani ambayo ilikuwa imepigwa na kupewa taarifa ile ya ajali mbaya huku wakionekana kutokuyaamini masikio yao.
Wakaonekana kuchanganyikiwa, wote walijiona kuwa kwenye ndoto iliyojaa huzuni ambapo baada ya muda wangeshtuka kutoka usingizini na kumuona Wayne akiendelea kujiandaa na harusi pamoja na mchumba wake, Kristen.
Hiyo haikuwa ndoto, lilikuwa ni tukio halisi ambalo lilikuwa limetokea katika maisha yao. Walichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika hospitali ya Jackson Heights ambayo walikuwa wameelekezwa iliyokuwa katika mji wa Albertson hapo hapo jijini New York.
Gari likafunga breki ndani ya eneo la hospitali ile, wote wakateremka na kuanza kuelekea ndani ya hospitali hiyo kubwa. Waandishi wengi wa habari walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kupiga picha na kuandika kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea kwani tukio lile la ajaili lilikuwa limegusa hisia za watu wengi nchini Marekani.
Bwana Brown na mkewe wakaingia ndani ya jengo lile huku wakipigwa picha na waandishi wale waliokusanyika katika eneo la hospitali ile. Breki ya kwanza ilikuwa ni nje ya chumba cha wagonjwa mahututi ambacho alikuwa amelazwa Wayne.
Wote wawili wakajikuta wakitokwa na machozi hasa mara baada ya kuuangalia mlango wa chumba kile kilichoonekana kutisha. Wakakaa vitini huku bado machozi yakiendelea kuwatoka. Walitakiwa kusubiri mahali hapo mpaka pale ambapo wangeruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho kwa ajili ya kumuona mtoto wao.
Masaa yalikatika lakini hakukuwa na yeyote ambaye alikuwa ameruhusiwa kuingia, nao hawakutaka kuondoka mahali hapo, waliendelea kusubiri zaidi na zaidi. Usiku ukaingia na hata asubuhi kufika lakini bado hawakuruhusiwa zaidi ya madaktari kupishana mlangoni.
Hali ya Wayne ilionekana kuwa mbaya kiasi ambacho akatolewa chumbani akiwa juu ya machela na kisha kuanza kupelekwa katika hospitali ya St’ Albert ambayo ilikuwa kubwa sana nchini Marekani. Hawakutaka kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kuanza kuifuatilia machela ile huku Bi Lydia akilia kama mtoto.
Katika maisha yao walikuwa wamepitia katika hali ngumu sana lakini kwa wakati huo, hali hiyo ndio ilikuwa ikionekana kuwa ngumu zaidi katika maisha yao. Wayne akapakizwa ndani ya helkopta ya hospitali ile na kisha kuanza kupelekwa katika hospitali ya St’ Albert huku dripu zikining’inia.
Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia wakaingia katika gari lao na kisha kuanza kuelekea katika hospitali hiyo iliyokuwa katika mji wa RockVile uliokuwa karibu na uwanja wa ndege wa Kimataifa wa John F Kennedy.
Ni ndani ya dakika mia moja wakawa wamekwishafika katika eneo la hospitali hiyo. Wakateremka na kuanza kuingia ndani ya jengo la hospital hiyo. Kama kulia walikuwa wamelia sana na kama macho yao kuvimba yalikuwa yamevimba sana.
Miili yao ilikuwa ikitetemeka kupita kawaida, tayari hali ya wasiwasi ilikuwa imewashika, walikuwa wakiogopa kupita kawaida, waliona kwamba muda wowote ule wangeweza kumpoteza mtoto wao ambaye walikuwa wakimpenda sana hata zaidi ya walivyokuwa wakimpenda mtoto wao mwingine, Esther.
Mara baada ya oparesheni ya kuwekewa ngozi nyingine kufanyika ndani ya chumba maalumu na ndipo wakaruhusiwa kuingia ndani ya chumba kile. Hawakutakiwa kupiga kelele zozote zile kwa kuhofia kuleta matatizo mengine zaidi.
Wayne alikuwa kitandani kimya, dripu zilikuwa zikiendelea kuingiza maji mwilini mwake huku mashine ya hewa ya Oksijeni ikiwa imeziba mdomo na pua yake. Wote wakashindwa kuvumilia, hali ambayo ilionekana kwa mtoto wao ikaonekana kuwatisha, wakaanza kulia.
Hayo ndio yalikuwa maisha ya Wayne. Ajali ilionekana kubadili maisha yake kabisa. Ila kila siku wazazi wake walikuwa wakimshukuru Mungu kwa kumnusuru mtoto wao kutokana na Kristen kufariki pale pale. Wayne akaonekana kuwa na bahati katika maisha yake.
Miezi ilikatika lakini Wayne hakufumbua macho yake. Mwaka wa kwanza ukakatika, wa pili ukafuata. Mwaka wa tatu ukaingia, wa nne na hata wa tano ukaingia, bado alikuwa amefumba macho yake vile vile.
Mishipa yake ya fahamu ilikuwa imelegea sana kutokana na ajali ile kumletea matatizo na ilikuwa imechukua muda mrefu sana mpaka kukaa sawa. Waliamini kwamba ni lazima kuna siku Wayne angekuja kufumbua macho iwapo tu kama mishipa ile ya fahamu ingekaa sawa.
Kama kulia, wazazi wake walilia sana. Katika kipindi cha miaka mitano, kila siku walikuwa wakifika hospitali hapo huku wakiwa na mtoto wao, Esther ambaye alikuwa na majonzi zaidi ya wote. Maisha ya kitandani bado yalikuwa yakiendelea kwa Wayne.
Mwaka wa sita ukaingia na siku kumi na mbili, Wayne akayafumbua macho yake. Manesi hawakuamini kile ambacho walikuwa wamekiona, walichokifanya ni kwenda kumuita daktari ambaye alifika mahali hapo na kumwangalia Wayne.
“Glory to Almight God (Utukufu kwa Mungu Mkuu)” Dokta Carthebert alisema huku akiinyoosha mikono yake juu.
Walichokifanya ni kuwapigia simu wazazi wake ambao walifika mahali hapo huku wakiwa na furaha kupita kawaida. Kitendo cha mtoto wao kufumbua macho kilionekana kuwafurahisha kupita kawaida. Wakaanza kumshukuru Mungu kwa jambo kuu ambalo alikuwa amelifanya katika maisha ya mtoto wao, Wayne.
Japokuwa Wayne alikuwa amefumbua macho lakini hakuweza kuongea kitu chochote kile kitandani pale. Kumbukumbu zake zikaanza kurudi upya, akaanza kukumbuka kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea siku ile alipopata ajali.
Alitamani kuongea kitu lakini hakuweza kuufumbua mdomo wake kabisa. Miezi sita ikakatika na ndipo Wayne alipoanza kufumbua mdomo wake na kuanza kuongea. Madaktari wakaonekana kuwa na furaha, walichokifanya ni kuwapigia simu wazazi wake na kuwapa taarifa.
Bwana Brown na Bi Lydia wakafika hospitalini hapo huku wakionekana kuwa na furaha kupita kawaida. Taarifa walizoambiwa kwamba Wayne alikuwa amefumbua mdomo wake na kuongea zilikuwa zimewapa faraja.
Wakaingia ndani ya chumba kile na macho yao kutua kwa mtoto wao, Wayne. Wote wakajikuta wakitoa tabasamu pana. Wayne alikuwa akiongea vitu fulani kwa sauti ya chini kabisa hali iliyomfanya Bwana Brown kumsogelea na kulipeleka sikio lake karibu na mdomo wa Wayne.
“Say something my son (Ongea kitu chochote kijana wangu)” Bwana Brown alisema huku akitabasamu.
“I want my kid....I want to see my kid (Ninamtaka mtoto wangu.... Ninataka kumuona mtoto wangu)” Wayne alisema maneno yaliyomfanya Bwana Brown kushangaa.


Je ni nini kitaendelea?
Je Wayne ataweza kumuona mtoto wake?
Je wazazi wataweza kufahamu Andy anamzungumzia mtoto yupi?
Itaendelea

RIWAYA: WASALIMIE KUZIMU---------------- 5


MTUNZI: Hussein Wamaywa

SIMU: 0755 697335


SEHEMU YA TANO

Kwa yakini hakuna, hakuna kwa maana ya watu wanaojua kupenda, natumai ushujua naongelea nini!” Akahitimisha. Nasra akatikisa kichwa kukubaliana nae. Akasema.
“Ni kweli uyasemayo baba. Saadan ana moyo wa peke yake! Lakini mimi…..” Akasita na kumtupia jicho baba yake. Alitaka kusema ‘simpendi kabisa!’ macho ya Alwatan Dafu ndiyo yaliyombadilihia uelekeo wa maongezi.
“Lakini mimi simjui fika! Nahitaji kumjua kwanza baba pengine inawezekana yeye akawa mbaya zaidi kuliko wote uliowataja. Inawezekana anajifanya Simba mwenda pole ili ale nyama! Huwezi kujua baba!”
“Inawezekana wala sio uongo, wala sikatai utabiri wako. Lakini pamoja na yote bado sijaelewa unataka kuniambia nini? Ujue sitaki kabisa kuusikia upuuzi wa Halfan!”
“Swali zuri Daddy! Nataka kwenda Oman kwa Saadan. Nikakae walau mwezi mmoja, miwili au miattu! Nione hali halisi ya maisha ya kule, nimjue vilivyo, naamini nikirudi hapa nitakuwa nimerejea na tarehe ya harusi!”
“Good Nasra. Ndio sababu nakupenda Nasra. Wewe ni msichana wa ajabu. Ninajivunia hilo, I love you Nasra!” Baba Nasra akishangilia kwa vigelegele “Sasa umeamua jambo la busara kuliko yote uliyowahi kuamua katika maisha yako!” Akainuka na kuingia ndani, akarudi na vitabu vitatu vyenye majalada ya plastiki.
“Hizi ni Passport zenu aliniachia Saadan siku chache kabla ya kuondoka. Ni wewe tu kuamua uondoke lini! Sawa mwanangu? Juu ya nauli usiofu aliacha fedha za kutosha tu.
“Sawa baba, lakini naomba kitu kimoja tu ukifanya hicho utanihakikishia ni kiasi gani unanipenda na kunithamini.
“Kuwa huru na usema unachotaka.”
“Ni juu ya Halfan!” Alwatan akakunja uso.
“Najua ni kiasi gani ninakukera na kukuudhi kila ninapotaja jina hili. Lakini baba wewe ni mtu mzima sasa. Na ugomvi wako na yeye ulishamiri wakati ule nilipomkataa Saadan, lakini sasa nimeshamkubali! Sioni kama kuna haja ya ugomvi tena. Halafu ujue hata kama mimba ile iliingia kwa bahati mbaya, lakini ndo tayari watoto wameshazaliwa na hatuwezi kuwaangamiza au kumsusIa!
Hivyo tutake tusitake tumeshaunga undugu na Halfan, ingawa ninaolewa kwingine! Ingawa nitakuwa nimeolewa tayari; Halfan kama Halfan ataendelea kuwa mzazi mwenzangu forever! Na wewe lazima umuheshimu kama mkweo! Kama Saadan.
Naomba upunguze chuki dhidi yake na ikiwezekana muondoleane uhasama baina yenu. Please baba, temeni mate chini Shetani apite!
Alwatan Dafu akafikiria kwa muda na kushusha pumzi. “Nitafikiria ‘I mean’ nitajitahidi kufanya uliyoinambia. Hakuna haja ya uhasama, aghalabu maelewano huwa ni bora zaidi kuliko mifarakano. Nitajitahidi mwanangu!”
“Good baba! Very Good!” Ikawa zamu ya Nasra kufurahi.
“Sasa unaweza kwenda kazini baba, nakutakia kazi njema yenye afya, furaha na bashasha!” Nasra akahitimisha kwa kumkumbatia na kumbusu baba yake.
“Na wewe pia, nakutakia mapumziko mema hapa nyumabni unatarajia kuondoka lini?”
“Nafikiri wiki ijayo, lakini natarajia kushauriana na mama juu ya siku nzuri ya kuondoka!” Akajibu wakiachiana. Alwatan Dafu akienda kazini. Nasra akirudi chumbani kwake!”
Kwisha kazi yake! Kila mmoja kwa upande wake aliwaza hivyo. Walikuwa wamewezana! Hawakurofautiana sana na ile hadithi ya mjanja mjanjuzi.
Chumbani hakukukalika. Nasra akatoka mbio mpaka kwa mama yake, akafika anamkumbatia kwa nguvu huku machozi ya furaha yakimtoka “Thank you mama, Thank you. Nashukuru sana kwa ushauri wako mzuri”
“Enhe nipe habari mwanangu, mambo yamekwendaje?”
“Imekuwa rahisi nisivyotegemea, yaani kama kumsukuma Mlevi vile!” akamueleza mama yake kila kitu. Mama mtu akabaki mdomo wazi kwa ujasiri wa mwanae.
“Sasa …?” Alikuwa mama Nasra “Sasa unaweza kufanya mambo yako taratibu kabisa bila usumbufu wowote ule!” Baadae walipanga tarehe ya safari kuwa ingekuwa wiki mbili zijazo.
Jioni Dafu aliporudi akapewa habari hizo na kuzidi kufurahia. Siku zikasogea. Na kadiri muda ulivyozidi ndivyo hali ya Romota, mtoto mdogo wa Nasra ; pacha wa Promota ilivyozidi kuwa mbaya kiafya.
Walimpeleka hospitali hii na ile bila mafanikio. Siku ya safari ilipowadia bado hali ya Romota ilikuwa haijakaa sawa. Wakaiahirisha na kumpigia simu Saadan na kumueleza sababu za kuiahirisha safari ya Nasra.
Miezi michache baadae hali ya Romota ilizorota zaidi, ikawa mbaya kupindukia, hatimaye akafariki dunia. Nasra alilia mno kumlilia mwanae kiasi cha kupoteza fahamu mara kadhaa.
Habari za msiba wa mototo wa Nasra zilitambaa na kufika mbali zaidi. Siku mbili baadae watu walikuwa wamefurika nyumbani kwao. Saadan nae alikuwepo.
Wakazika na kumaliza matanga. Siku chache za kumfariji mfiwa zikakatika. Hatimaye Nasra akakubali kuwa kazi ya mungu haina makosa. Miezi michache baadae waliondoka na Saadan pamoja na Promota na kuelekea Omani!
Ilikuwa safari ndefu na ya ajabu kwa Nasra ambaye hakuwahi kupanda ndege kabla. Alijifunza mengi na vingi njiani. Mpaka wanafika Oman, tayari alishaelimika vya kutosha!


* * *
Husemwa na kuimbwa kwamba mtaka cha uvunguni sharti ainame, mwombaji sharti mikono iwe nyuma na pengine haraka haraka haina baraka.
Misemo nahau na methali zinazokwenda sambamba na ile ya subra yavuta kheri huleta kilicho mbali, ilitumika haswa kutekeleza matakwa ya Nasra Alwatan Dafu.
Badala ya mwezi mmoja au miwili aliyokuwa ameipangilia, aliishi miezi mingi zaidi. Na ili kuweka mazingira mazuri ya kuondoa mizengwe, kauzibe na ukuta katika mioyo ya ndugu wa Saadan, Nasra na Saadan walikubaliana kumfanya Promota kuwa mtoto wa Saadan.
Ingawa rangi na matendo ya Promota vilikuwa beni beni na hali ya Saadan, Nasra na Saadan walijitia hawalioni hilo. Ndugu nao hali kadhalika, wengine wakadai kitanda hakizai haramu!
Saadan aliyekuwa mcha-Mungu kupindukia, aliwasha ngaza daadhi ya ndugu zake pale alipokubali kuwa ‘alimuingilia’ Nasra bila kufunga ndoa. Na mara zote alipoulizwa ni kwa nini alifanya hivyo, jibu lake lilikuwa moja tu, “Ibilisi jamani!”
Wengi kama siyo wote walimpokea Nasra vizuri. Na baadhi walikuwa wacheshi kama yeye mwenyewe. Na vile lugha ya kiarabu Nasra aliifahamu vizuri, hakuwa na shida katika mawasiliano.
Ajabu ni kwamba kwa kipindi chote alichokuwa Oman, Nasra hakumruhusu Saadan kuukurubia katika mwili wake.
Lakini vitendo vidogo vidogo kama kuiruhusu miili yao ikaribiane, kukumbatiana na pia kubusiana; Nasra alishindwa kuvizuia na kumruhusu Saadan afanye hivyo mara nyingi tu katika mwili wake.
Noor, mtoto wa kiume anayemfuata Saadan ndiye kidogo aliyeonekana kutokubaliana na ulaghai kwamba Promota alikuwa mtoto wa kaka yake. Yeye alitamka wazi kuwa Saadan amepigwa bao la kisigino na wabongo!
Huyu alikuwa kero kwao lakini kwa kuwa familia nzima ilimuona kama ambaye hajatulia, hakuna aliyezitilia maanani kauli zake ambazo zilikuwa kama msumari wa moto katika donda bichi la moyo wa Saadan.
Hali hii na lile la kupigwa marufuku asiusogelee mkate wa siagi wa Nasra, vilimuathiri sana. Lakini kwa vile moyo wake ulishatua kwa Nasra, na wenyewe wanasema ‘muhitaji ni khanithi;’ Saadan aliyameza haya kwa machungu makali na maumivu yasiyo na mfano.
Hatimaye siku ilifika, siku ya kuondoka kwa Nasra. Ilikuwa siku ngumu kwa Saadan ambaye moyo wake ulikuwa ukipata faraja kumuona Nasra pembeni yake kila wakati.
Wakiwa Air port pamwe na ndugu zao, Saadan alishindwa kabisa kuyazuia machozi yaliyotiririka mashavuni baada ya kufanya vurugu za mwaka katika macho yake. Hili likamgusa Nasra.
Akamchukua Saadan na kusogea nae pembeni. Huku naye machozi ambayo nilishindwa kung’amua mara moja kuwa ni ya furaha au uchungu yakimtoka;
Akamkumbatia kwa nguvu na kwa mara ya kwanza akampiga busu la kinywa. “Saadan! Naamini unanipenda mimi kuliko kitu kingine chochote. Na ninataka kukuahidi kitu kimoja. Kwamba amini sasa Nasra bint Dafu ataolewa na Saadan peke yake!
Kujizuia na kuzizuia tamaa za mwili wako kwangu ingawa mara nyingi tumeondakea kupewa ‘one room’, juu ya kitanda kimoja tukiwa kama bibi na bwana harusi mtarajiwa, kumenifanya niamini kwamba upendo wako kwangu haumaananishi tamaa za kimwili tu;
Bali umekwenda mbali zaidi. Ndivyo mapenzi ya kweli yanavyotakiwa kuwa! Umenionyesha kwamba unanipenda kwa dhati. Sioni kwa nini nisikupe tumaini. Nakupenda Saadan!” Nasra alinong’ona taratibu akiwa juu ya kifua cha Saadan. Saadan akafarijika. Kwa kila hali ilikuwa habari njema kwake.
Akafaulu kufuta machozi na kubaki akimtazama Nasra kwa matamanio. “Sasa kama unalitambua hilo ni kwa nini basi unasita nisilete washenga kwenu waje kuulipa mahari uwe wangu wa milele, tutenganishwe na kifo?”
“Sisiti kwa nia mbaya dia, mambo mazuri hayataki haraka. Fanya taratibu, pole pole. Utaona matokeo yake na unaweza kuona mambo yanakuwa vipi!
Mara ya kwanza nilikwambia nitakuja Oman. Na tayari nimetiza ahadi! Hiyo pekee inatosha kukuonyesha kwamba Nasra sio mtu wa kupoteza miadi! Ni mtu ambaye akiahidi anatimiza.
Naelewa kwamba ahadi ni deni na shuruti uitimize. Amini ahadi niliyotoa kwako itatimia. Jambo la muhimu ni subira tu hata hivyo nataka unihakikishie kwamba mdogo wako Noor hatambughudhi mwanangu endapo tutafunga ndoa!”
“Nakuahidi hatombughuddhi! Tone moja la damu kamwe haliwezi kuchafua maji ya mto au bahari. Nitamdhibiti istoshe ndugu wote wanamjua kuwa hajatulia.”
“No! tena hao wasiotulia ndio wabaya kwa kuumbuana. Maana akishtukia ishu tu, hakai kimya. Bahati nzuri au mbaya watu hawa wasiotulia hufikia wakati wakatoa mawazo ambayo waliotulia hushindwa hata kuyafikilia wachilia mbali kuyatoa. Mfano kama hili sio siri kanifanya nionekane Malaya na tapeli!”
“Usifadhaike mpenzi! Nakuahidi tutaishi raha mustarehe!”
Wakaachana pale wasafiri waliposikia tangazo lililowahitaji kuingia ndani ya ndege upesi Nasra akawaaga ‘wifi’ zake, ‘shemeji zake’ ‘wakwe zake’ na hata marafiki zake.
Akawaacha na nyuso zilizojaa simanzi na huzuri, akavuta hatua kuijongelea ndege mwanae Promota akiwa kifuani mwake Naam! Dakika kumi baadae alikuwa hewani.

* * *
Watu waliojitokeza kumpokea nyumbani Tanzania walikuwa wachache sana. Baba yake, mama yake na wafanyakazi wao kadhaa wa ndani. Pengine waliokuwa wageni ni washiriki wenzake wa Miss Temeke Academia ambao walishika nafasi ya pili na ya tatu.
Labda kilichomfurahisha ni kile kitendo cha wazazi wake kuja kumpokea na gari yake ya ushindi Caddilac. Wakajipakia garini na msafara wa kuelekea nyumbani kwa Alwatan Dafu ikaanza.
Nyumbani kwao kulikuwa na sherehe kubwa ikimsubiri. Nusura Nasra aanguke kwa Mshutuko alioupata. Akajumuika na wenzake wakasherehekea kurudi kwake. Wakala kunywa na kucheza muziki.
Sherehe ilipokwisha washiriki wenzake wa urembo waliondoka na kumuacha jioni akiteta na wazazi wake, ambao walikuwa wanahitaji kusikia mengi kutoka kwake.
Kwanza aliwaoongopea mengi kuhusu Saadan na Oman na mipango yao ya ndoa ambayo ilipangwa kufanyika mwaka mmoja baadae. Halafu akahitimisha kwa kuwapa zawadi zao alizotoka nazo ukweni.
Alwatan Dafu alikaribia kupasua kwa furaha. “Kwa nini mipango yenu ya ndoa mmeiweka mbali hivyo?” Alwatan akashindwa kujizuia.
“Kusomana baba, unajua Kusomana tabia sio kazi ndogo. Ni kazi isiyohitaji papara ili maamuzi yatakayofikiwa yasijekuwa na majuto baadae. Ni vizuri kufikiri kabla ya kutenda.”
“Sasa mnasomanaje na hali mko beni beni kama mbingu na ardhi? Mmoja Afrika, mwingine Asia! Inawezekana kweli?!”
Kwa nini isiwezekane baba? Huu ni mwanzo tu kuna wakati yeye atakuja huku na tutaishi kwa kipindi furani. Na kuna wakati tunaweza kusafiri na kwenda kuishi nje. Tutafanya mambo kadiri tutavyoona. Subira tu ndiyo inayohitajika.
“Oke! Whatever you like, I’m ready to listen you! (vyovyote mpendavyo ninawasikiliza nyie!)
“Good Baba! Ninajivunia kuwa wewe ni baba yangu!” kauli hii ilimuacha Alwatan Dafu akitabasamu, kabla hajambusu mwanae na kumtakia usiku mwema. Kisha akaingia ndani kulala.
Akawaacha mtu na mama yake wakiteta kwa nafasi. Hapo ndipo Nasra alipomueleza mama yake ukweli halisi ulivyo, vile alivyohisi na mipango yake ya baadae ambayo ilikuwa tofauti na mbali kabisa na Saadan.
“Mh! Mtoto una hatari wewe! Haki ya Mungu sijaona!” Mama yake akasema kwa kicheko mwisho wa maelezo ya Nasra. “Nataka kumuonyesha baba kuwa yeye akiujua huu, wenzie tunaujua ule.
Naomba nikushukuru tu kwa vile wazo lako la kwenda Oman limeniweka huru. Na tena ninaamini kuwa sasa nitaweza kuitumia Caddilac yangu. Naomba unifanye mpango wa kuipata kadi yake! Akaomba.
“Nitakufanyia mwanangu! Iko katika droo ya baba yako. Kumbuka furaha yangu inakuja pale unapokuwa na furaha nitakupatia!“ Na kweli alimpatia siku mbili zilizofuata.
“Thanks mama! I won’t stop loving you!” Nasra akashukuru wakati akiipokea kadi hiyo. Akiwa na funguo na kadi ile tena sasa akiwa na uhuru wa kufanya atakalo na kwenda atakako tena katika wakati atakao (isipokuwa usiku) Nasra alijihisi kama aliyetua mzigo mzito baada ya kazi ngumu! Alifurahia kuona akimiliki gari yake mwenyewe.
Ni hapo alipoamua kumpeleka mwanae katika shule za awali. Na taratibu ubongo wa Promota, mwanae pekee aliyesalia, ukaanza kunolewa…


***NASRA anaendelea na mkakati wake babkubwa....kimya kimya bila mzee wake kujua...SAADAN amedanganyika anahisi anapendwa kweli....
nini kitafuata???

ITAENDELEA KESHO

FACEBOOK CHATTING------- 4

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269




MSICHANA: Tayari.
MIMI: Safi sana. Itegeshe mike ya Hearphone yako karibu na mdomo. Ipe mikono yako uhuru. Wakati mwingine, unaweza kufumba macho. Itulize akili yako kabisa, achana na kufikiri mambo mengine. Isikilize sauti yangu kwa makini, nitakwenda kuongea maneno mengi, yanayotakiwa kufanya na wewe, fanya kama nitakavyokwambia. Hakikisha umelala chali. Umesikia mpenzi.
MSICHANA: (Huku sauti yake ikianza kubadilika na kuwa ya chini) Sawa.
MIMI: Tunakwenda kuanza mchezo huu. Mchezo huu utaanzia mwilini mwako, nitakwenda kuitembelea kila sehemu yako ya mwili. Kumbuka kwamba mikono yako ndio mimi kwa sasa. Hakuna maswali, tulia na niache nifanye kazi yangu.
MSICHANA: Sawa mpenzi.
MIMI: Tunakwenda kuanza mchezo wetu. Tunaanzia kifuani kushuka chini.
MSICHANA; Sawa.

Kuanzia hapo, mchezo ulivyochezwa hautoweza kuelezwa sana kwa sababu ya matumizi ya facebook kutumiwa hadi na watoto walio chini ya miaka 18. Usiulize maswali wala usibishe. Kuna watoto wengi huku mtaani kwetu ambao ni marafiki zangu na wote wanaisoma post hii. Sitoelezea sana mchezo huu kwani sitotaka kuiharibu saikolojia yao, ufahamu nilio nao kwenye mchezo huu acha ubaki kuwa wangu tu, sitaki kuibiwa maujuzi kabisa. Kila mtu anatakiwa kuucheza mchezo huu kwa kutumia ujuzi wake na si kuiba ujuzi kutoka kwangu kwani unaweza kumuua hata binti wa watu na kuniletea matatizo.

NB: Watoto wengi, sehemu hiyo inakatishwa kidogo na wala haitoelezewa kwa kina.


Mchezo uliendelea zaidi na zaidi, kila wakati nilikuwa namsikia akipumua kwa nguvu huku akilalamikalalamika. Bado nilikuwa nikiendelea kama kawaida. Dakika kumi zikapita, niliendelea kuongea nae, dakika ishirini zikapita, nusu saa na hadi saa moja, bado alikuwa akilalamikalalamika tu.

MSICHANA: Stooooooooooopppppp (Aliitoa sauti yake kimahaba)
MIMI: Nini tena?
MSICHANA: Stooooooopppp mpenzi. Aaaaggggghhhhh! Naomba nipumzike.
MIMI: Mbona unaomba kupumzika tena na wakati bado masaa kama matatu hivi?
MSICHANA: Utaniua. Nimeshindwa kujizuia mpenzi.
MIMI: Poleeeee
MSICHANA: Asante. Ngoja nikaoge kwanza.
MIMI: Vipi tena?
MSICHANA: Umenichafua.
MIMI: Hahahaha! Nimekuchafua au umejichafua?
MSICHANA: Umenichafua. Haukumbuki ulisema uwe mikono yangu?
MIMI: Ok! Nimekuelewa. Ukitoka huko naomba ulale. Mimi mwenyewe nimejichafua pia. Nakwenda kuoga, sitokuwa na nguvu ya kuendelea. Acha nilale kwanza mpaka kesho. Usiku mwema.
MSICHANA: Nawe mpia mpenzi (Bado sauti yake ilikuwa ikisikika kimahaba)

Nikabaki nikicheka sana, sikuamini kama msichana yule hakutaka kuendelea kuucheza mchezo ule na wakati ndio kwanza tulikuwa tumetumia dakika sitini tu. Nikaenda kuoga na kisha kurudi kitandani. Sikutaka kuwasha simu yangu kwani nilijua kwa namna moja au nyingine angenitafuta tu.
Kesho, nikaanza kuelekea chuoni. Akili yangu nikaituliza huku ikionekana kama kutokukumbuka kitu chote kilichotokea. Saa tano na nusu nikawasha simu yangu na kukutana na meseji zake tano.

MSICHANA: *Usiku wa jana umekuwa usiku wa kukumbuka sana kwangu.
*Nilikuwa nikilalamika mpaka mama akasikia na kuamua kuja chumbani kwangu. Sijui amejua nilichokuwa nimekifanya kwani asubuhi alikuwa akiniangalia kwa jicho la wasiwasi sana.
* Kama mchezo wenyewe upo vile, sijui itakuwaje. Unaonekana kuwa mchezo mzuri lakini uliojaa hatari.
* Ingawa niliwahi kuucheza mchezo ule lakini jana ilikuwa balaa. Yaani kama ni mpira basi nimekutana na timu inayokimbiza muda wote.
* Mbona upo kimya mpenzi? Naomba ukizipokea meseji hizi nijibu chochote ili niwe na furaha. Leo sijaenda shule kabisa kwa kuogopa kutokuelewa darasani. Nimesingizia naumwa. Yote kwa ajili yako. Nakupenda mpenzi. Nakupenda My Only Nyemo.

Nilibaki nikicheka sana. Msichana ambaye ilikuwa imepita siku moja tu tangu tuanze uhusiano wa kimapenzi alikuwa amechanganyikiwa sana. Mahusiano yetu yakawa yamechangamka sana kana kwamba yalikuwa yameanza miezi sita iliyopita.

MIMI: Usijali mpenzi. Mchezo ule unahitaji sana maandalizi. Wengi wanashindwa kuucheza kwa sababu tu huwa wanakurupuka. Mimi kama mimi huwa ninakwenda hatua kwa hatua mpaka mwisho. Najiamini, ninafanya kazi zangu kwa uhakika mpenzi.
MSICHANA: Una tabia mbaya sana. Mbona haukunijibu toka asubuhi nilipokutumia meseji zile?
MIMI: Nilikuwa darasani baby. Hadi hapa bado nipo darasani.
MSICHANA: Umejifunza wapi mchezo ule?
MIMI: Nyumbani.
MSICHANA: Mmmh! Una hatari wewe!
MIMI: Hatari ya nini tena?
MSICHANA: Ungeweza kuniua last night. Yaani kuna kipindi nilikuwa naona viungo vyote vikiishiwa nguvu.
MIMI: Poleeeee
MSICHANA: Asante mpenzi.
MIMI: Naomba leo tucheze tena.
MSICHANA: Sitaki. Sitaki tena kucheza, utaniua jamani. Jana nilikuwa nahema juu juu kama nakata roho vile.
MIMI: Polee sana. Ila ndio ukubwa huo.
MSICHANA: Au ulitaka kunitoa usichana wangu?
MIMI: Kwani unao?
MSICHANA: Ndio
MIMI: Mmmh! Kweli hatari. Unanishangaza sana.
MSICHANA: Kwa nini?
MIMI: Ulidumu na mpenzi wako kwa muda gani?
MSICHANA: Kwa miaka miwili.
MIMI: Hamkufanya kitu chochote kile?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Alikuwa na chembechembe za ushoga nini?
MSICHANA: Hahahaha! Kwa nini unasema hivyo?
MIMI: Inawezekana. Miaka miwili halafu kimya. Haiwezekani, kuna jambo hapo nyuma ya pazia.
MSICHANA: Inawezekana.
MIMI: Hivi una miaka mingapi?
MSICHANA: Kumi na nane.
MIMI: Hahahaha! Unafaa kuliwa wewe. Umeshaiva mpenzi. Inabidi nikutungue kutoka mtini. Umeiva vizuri kabisa.
MSICHANA: Hahahaha! Una maneno wewe
MIMI: Hayo ndio maneno tunayopenda kuyatumia huku kwetu. Miaka kumi na nane mkubwa sana, tena sana. Kama ungekuwa huku kwetu ungekuwa unatafutiwa mume.
MSICHANA: Ningekuwa natafutiwa mume?
MIMI: Ndio. Tungekuwa tunakula pilau sasa hivi.
MSICHANA: Hahahaha! Sawa bwana. Ila inakubidi uwe na shabaha ya kulitungua tunda lililoiva.
MIMI: Shabaha ninayo tena kubwa sana. Nikiona kama nakukosa, nitakupandia uko uko mtini. Hahahaha!
MSICHANA: Una visa sana Mpenzi.
MIMI: Usijali. Lecturer anaingia. Kama vipi tutaendelea kuchati baadae.
MSICHANA: Poa. Nakupenda mpenzi.
MIMI: Nakupenda pia.

Msichana yule alionekana kuwa msumbufu sana, muda wote alikuwa akinitumia meseji za mapenzi lakini sikumjibu hata moja, muda wote nilikuwa nikimfuatilia lecturer alivyokuwa akifundisha. Muda wa kutoka ulipofika, sikutaka kumshtua, nikarudi nyumbani na kujilaza kitandani.

MIMI: Nipo nyumbani.
MSICHANA: Namshukuru Mungu umerudi nyumbani salama. Kuna kitu nilikuwa nakifikiria mpenzi.
MIMI: Kitu gani?
MSICHANA: Unaonaje tukionana somewhere?
MIMI: Lini?
MSICHANA: kesho.
MIMI: Haitowezekana kabisa.
MSICHANA: Kwa nini mpenzi?
MIMI: Labda tufanye weekend.
MSICHANA: Okey! Ila naomba tuonane mpenzi.
MIMI: Usijali.

Baada ya hapo, mawasiliano yalikuwa yakiendelea kila siku, alitamani sana kuonana nami lakini nilikuwa bize sana mpaka pale ilipofika weekeend ambapo tulipanga sehemu ya kukutania.

MIMI: Umesema wapi?
MSICHANA: Slipway.
MIMI: Du! Sipajui bwana.
MSICHANA: Acha kunitania mpenzi. Ila usijali, nitakuelekeza.
MIMI: Poa.

Baada ya hapo akaanza kunielekeza. Si kwamba nilikuwa sipajui kweli Slipway ila kwa wakati huu nilikuwa nikitaka kucheza na akili yake tu. Nilitaka afahamu kwamba mimi nilikuwa mtoto wa uswahilini na hata sehemu nyingi za kuenjoy hasa za watu waliokuwa na uwezo fulani nilikuwa sina uhitaji wa kupafahamu.
Nikafikiria kwa haraka haraka, sehemu ile ilikuwa haiendeki kwa daladala hivyo kama ningependa daladala ya Msasani na kwenda huko, ungekuwa mwendo mrefu kidogo. Sikuonekana kujali, kukutana na msichana wangu ndicho kitu pekee ambacho nilikuwa nikikihitaji.
Asubuhi ya Jumamosi tukaanza kuchati kwa sms hata kabla hatujaonana.



Itaendelea

Sunday, April 7, 2013

RIWAYA: PAINFUL TRUTH (UKWELI WENYE KUUMA)============ 4

 

MTUNZI: Nyemo Chilongani

MAWASILIANO: 0718 06 92 69


SEHEMU YA NNE

Maisha ya Happy hayakuwa na furaha tena hali iliyompelekea kuondoka nyumbani kwa shangazi yake na kurudi nyumbani kwao Machame. Kichwa chake kilikuwa kikifikiria kuhusu mimba ambayo alikuwa nayo, hakujua ni kitu gani ambacho angekifanya mpaka kuanza kuwaeleza wazazi wake kuhusiana na mimba ile.
Moyo wake ulikuwa ukimuuma, akaanza kumchukia Wayne ambaye alikuwa amempa ujauzito ule na kisha kuondoka kurudi nchini Marekani. Alijiona kuwa mpweke, akakosa amani kabisa.
Mpaka katika kipindi ambacho alikuwa akiingia nyumbani kwao, Happy alikuwa akilia tu. Wazazi wake, Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakabaki wakimshangaa Happy, hawakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikimliza binti yao katika kipindi hicho.
Kila walipojaribu kumuuliza Happy kitu ambacho kilikuwa kimetokea, alikuwa kimya, hakutaka kuwaambia wazazi wake kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika kipindi ambacho alikuwa jijini Arusha. Alibaki kimya, siri ya kwamba alikuwa mjauzito ikabakia moyoni mwake.
Siku zikakatika mpaka katika kipindi ambacho matokeo ya kidato cha nne yalipotangazwa. Happy alikuwa amefanya vizuri sana zaidi ya wanafunzi wote wa Machame Girls Secondary School. Matokeo hayo yaliinua furaha kwa wazazi wake,
Kitu kilichowashangaza ni pale walipompa Happy matokeo yale. Badala ya Happy kuwa na furaha hata zaidi ya wao waliyokuwa nayo, akaanza kulia kwa uchungu. Kitendo kile kikaonekana kuwashangaza wazazi wake jambo ambalo liliwapelekea kumuuliza sababu ilikuwa nini. Happy hakutaka kuongea kitu chochote kile, tayari wazzi wake wakajua kwamba kulikuwa na tatizo limetokea.
“Kaongee nae. Nadhani ana tatizo” Mzee Lyimo alimwabia mkewe.
Bi Vanessa hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuanza kuelekea chumbani kwa Happy na kuanza kuongea nae. Alichukua saa moja kuongea nae lakini Happy hakuwa tayari kuufungua mdomo kueleza ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.
Bi Vanessa alitumia ujuzi wake wote na hatimae Happy kumwambia ukweli. Bi Vanessa akaonekana kama mtu aliyechanganyikiwa, hakuonekana kuyaamini maneno yale, alimwangalia binti yake mara mbili mbili huku akionekana kutokuamini.
“Una mimba?” Bi Vanessa aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio” Happy aijibu huku akiangalia chini.
“Ya nani?”
“Wayne”
“Ndiye nani?”
“Mvulana mmoja hivi”
“Anakaa wapi? Hapa hapa Machame au Arusha?” Bi Vanessa aliuliza.
“Anakaa Marekani”
“Marekani!”
“Ndio”
Bi Vanessa hakutaka kubaki ndani ya chumba hicho, alichokifanya ni kutoka na kisha kwenda kumwambia mumewe, mzee Lyimo.
Mzee Lyimo akaonekana kuchanganyikiwa, hasira zikaanza kumshika, akaanza kuondoka kumfuata Happy chumbani kwake. Alipoingia tu, akajikuta hasira zake zote zikipotea haa mara baada ya kuyaona machozi ya Happy ambayo yalikuwa yakimtoka mfululizo.
Mzee Lyimo akaanza kupiga hatua kumfuata Happy pale kitandani alipokuwa na kisha kukaa karibu nae. Moyo wake ukaonekana kuumia, alijua kwamba alitumia kiasi kikubwa sana cha fedha kumsomesha Happy mpaka kufikia hatua hiyo ambayo alikuwa mefikia, kupata ujauzito hata kabla hajaendelea na masomo kulionekana kumuumiza.
Alijua fika kwamba kumchapa Happy au kumfukuza nyumbani isingekuwa suluhisho la kile ambacho kilikuwa kimetokea, aliona kuwa na umuhimu wa kuwa pamoja na Happy na kumfariji katika hali ambayo alikuwa nayo katika kipindi hicho.
“Wayne ndiye nani?” Mzee Lyimo aliuliza japokuwa alikuwa ameambiwa kila kitu na mkewe.
“Mwanaume kutoka Marekani” Happy alijibu.
“Ni mzungu?”
“Ndio” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akaonekana kukosa nguvu, alichokifanya ni kuinuka mahali hapo na kwenda nje. Hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya, kupata ujauzito kwa Happy kulionekana kumnyima furaha kabisa.
Huo ndio ukawa mwisho wa Happy kusoma, hakuendelea tena na elimu, akawa msichana wa kukaa nyumbani na kuwasaidia wazazi wake kazi mbalimbali hasa shambani. Miezi ilikuwa ikiendelea kukatika, Happy alikuwa akiutunza ujauzito wake huku wazazi wake wakimpa kila msaada ambao alikuwa akiuhitaji.
Dalili zote za kuwa mjamzito zikaanza kuonekana, akaanza kutapika mfululizo huku akipoteza hamu ya kula. Muda mwingi alikuwa akijisikia uchovu hali iliyompelekea kulala. Mpaka miezi mitano inatimia, hali ya ujauzito ikaanza kuonekana waziwazi.
Happy alikuwa amelala chumbani kwake huku pembeni yake kukiwa na maembe mabichi pamoja na udongo. Hivyo ndivyo vilikuwa vitu ambavyo alikuwa akipenda sana kuvitumia kila siku. Mara mama yake akaingia chumbani humo, uso wake ulikuwa umejaa tabaamu pana.
Maswali mfululizo yakaanza kujikusanya kichwani mwa Happy, hakujua sababu iliympelekea mama yake kuwa na tabasamu namna ile. Akainuka kitandani na kukaa. Mama yake akaja na kukaa pembeni yake huku tabasamu likiendelea kuonekana usoni mwake.
“Kuna nini?” Happy aliuliza.
“Amekuja” Bi Vanessa alijibu.
“Nani?”
“Wayne. Yupo nje anakusubiri” Bi Vanessa alimwambia Happy.
Badala ya kuonyesha furaha, Happy akaanza kutokwa na machozi. Hali ile ilionekana kumshangaza mama yake ambaye akaamua kuanza kumbembeleza. Alipoona Happy amenyamaza, akatoka chumbani mule na moja kwa moja kwenda kumuita Wayne ambaye alikuwa nje ya nyumba lle.
Ni ndani ya sekunde kumi tu, mlang wa chubani ukafunguliwa na Wayne kuingia ndani. Usowa Wayne ukaonekana kuwa na furaha mara baada ya kumuona Happy kwa mara nyingine tena. Huku akionekana kuwa na tabaamu pana, akakaa kitandani pale.
Happy akashindwa kuvumilia, akajikuta akimsogelea Wayne na kumkumbatia kwa furaha huku machozi yakiendelea kumtoka. Wayne akaipitisha mikono yake na kumkumbatia. Walikaa katika hali hiyo kwa dakika mbili, Wayne akayapeleka macho yake usoni mwa Happy, akaonekana kufarijika.
“Nimekukumbuka mpenzi” Wayne alimwambia Happy.
“Nimekukumbuka pia” Happy alijibu.
Furaha ya Wayne ikaonekana kurudi moyoni mwake, tayari alikuwa amekwishasahau kama alikuwa amemuacha Kristen hotelini. Alikaa pamoja na Happy kwa muda wa masaa mawili na ndipo walipoanza kupiga stori.
“Mbona ulikimbia chumbani siku ile?” Wayne alimuuliza Happy.
“Nilikuwa nikiogopa, kuna kitu nilikuwa nimekikumbuka” Happy alijibu.
“Kitu gani?”
“Kwamba nilikuwa katika siku zangu za kupata mimba” Happy alitoa jibu ambalo likaonekana kumshtua Wayne.
“Unasemaje?”
“Nilikuwa katika siku zangu za kupata mimba. Hapa unaponiona, nina ujauzito wako” Happy alimwambia Wayne.
Wayne akaonekana kushtuka, akamwangalia vizuri Happy, akaipandisha blauzi ambayo alikuwa ameivaa na kisha kuliangalia tumbolake, aliona mabadiliko makubwa lakini cha ajabu katika kipindi ambacho alikuwa akifanya nae mapenzi hakuyaona mabadilko hayo.
Wayne akaonekana kubadilika, wasiwasi ukaanza kuonekana machoni mwake, hakuamini kama alikuwa amempa ujauzito msichana wa kiafrika, akamwangalia Happy huku dhahiri uso wake ukionekana kuukataa ujauzito ule.
Wayne akainuka, akaanza kuvaa nguo zake na kuufungua mlango, kilichoendelea mahali hapo ni kuondoka huku akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa. Hakujua ni kitu gani alitakiwa kukifanya, moyo wake haukuwa tayari kukubali kama alikuwa amempa mimba msichana wa Kiafrika.
“Haiwezekani. Ile sio mimba yangu. Siwezi kumpa mimba msichana wa Kiafrika” Wayne alisema katika kipindi ambacho alikuwa akielekea kituoni huku akiwaacha watu nyumbani pale wakiwa hawaelewi ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea ndani ya chumba kile.
Wayne alifika hotelini baada ya saa moja. Kristen alikuwa na wasiwasi akimsubiri. Japokuwa Kristen alionekana kuwa na wasiwasi lakini hakuuliza kitu chochote kile. Tayari Wayne alikuwa amebadilika, uso wake ukaonekana kuwa na hasira kupita kawaida, kitendo cha kumpa mimba msichana wa Kiafrika kilionekana kumuumiza.
“Kuna nini?” Kristen alijikuta akiuliza.
“Tuondoke. Inatupasa turudi nyumbani haraka iwezekanavyo” Wayne alimwambia Kristen.
“Unasemaje? Mbona ni maamuzi ya haraka namna hiyo?”
“Ndio hivyo. Nakuomba usiulize kitu Kristen. Nimechanganyikiwa baada ya kusikia kwamba marafiki zangu kutoka Uingereza wameelekea Marekani tayari kwa kuhudhuria harusi yetu” Wayne alidanganya.
“Harusi gani? Mbona unaonekana kama umechanganyikiwa?”
“Ni lazima tufunge harusi haraka iwezekanavyo. Huo ni uamuzi ambao nimejiwekea. Najua ni uamuzi ulioamuliwa kwa haraka sana. Haina jinsi mpenzi. Wiki ijayo ni lazima tufunge ndoa” Wayne alimwambia Kristen.
Ni kweli. Ulikuwa ni uamuzi wa haraka sana, Wayne alionekana kuchanganyikiwa. Taarifa za ujauzito ambazo alikuwa amepewa zilionekana kumchanganganya kupita kawaida. Siku mbili zilizofuata, wakasafiri na kurudi tena nchini Marekani ambako huko mipango ya harusi ikaanza kufanyika.
Kila kitu kilikuwa kimepangwa kwa haraka haraka sana hali ambayo ilikuwa ikimshangaza kila mtu. Vyombo vya habari vikaanza kutangaza harusi kubwa ambayo ilitarajiwa kufanyika wiki ijayo. Kila mtu akawa na hamu ya kuiangalia harusi hiyo kwenye televisheni.
“Ni bora nioe ili nimsahau Happy. Haiwezekani kuzaa na msichana wa Kiafrika” Wayne alisema.
Kitu walichokifanya ni kuanza safari ya kuelekea Elmon, mji mdogo uliokuwa pembeni mwa jiji la New York kwa ajili ya kuwaona babu na bibi wa mchumba wake, Kristen kwa ajili ya kuwapa taarifa kile ambacho kilikuwa kinataka kutokea.
Ndani ya gari walikuwa wawili tu, Wayne na Kristen. Wayne ndiye ambaye alikuwa ameshikilia usukani, alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi sana kwani alihitaji wafike katika mji huo haraka iwezekanavyo.
Bado kichwa chake hakikuwa sawa, muda wote alikuwa akimfikiria Happy na ujauzito ule ambao alikuwa nao. Mara kwa mara alikuwa akipiga usukani ule kuonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amechanganyikiwa.
“Happy.....haiwezekani...” Wayne alijikuta akisema kwa sauti kubwa iliyosikiwa na Kristen.
“Umesemaje?” Kristen aliuliza.
“Nini?” Wayne nae aliuliza.
“Nimekusikia umeongea kitu”
“Kitu gani?” Wayne aliuliza.
Bado Wayne alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi hadi kutokukiona kibao ambacho kilimtaka kuendesha gari kwa mwendo wa taratibu kutokana na matengenezo ya barabara. Ghafla, mbele yake akaona gari kubwa likichimba barabara ile huku mainjiania wakitoa malelekezo kwa dereva wa gari lile kubwa la kutengeneza barabara.
Kutokana na mwendo mkali ambao walikuwa nao, ikawa ngumu kufunga breki na gari kusimama. Gari lao ambalo lilikuwa katika mwendo wa kasi likalivamia gari lile kubwa lililokuwa likitengeneza barabara.
Mlio mkubwa ukasikika, Kristen akarushwa kutoka ndani ya gari mpaka nje na kukibamiza kichwa chake katika chuma kikubwa cha gari lile lililokuwa likitengeneza barabara ile. Na Wayne akarushwa mpaka nje, akaburuzika katika marabara ile, sehemu kubwa ya ngozi yake tumboni ikabaki barabarani.
Ilikuwa ni ajali kubwa ambayo wala haikuwa na moyo kuitazama. Gari lao lilikuwa limebondeka, milango ya mbele haikuwa ikionekana kabisa, yaani gari lilikuwa limebaki nusu tu kuanzia milango ya nyuma.

Je nini kitaendelea?
Je huo ndio mwisho wa Kristen na Wayne?
Je nini kitaendelea katika maisha ya Happy?
Itaendelea.

RIWAYA: PAINFUL TRUTH (UKWELI WENYE KUUMA)----------3

MTUNZI: Nyemo Chilongani

MAWASILIANO: 0718 06 92 69

SEHEMU YA TATU


“Nitachagua wa kumuoa hapo baadae. Ila hata Happy nae anafaa sana. Mmh! Wazazi watanielewa vipi kama nikimuoa? Kwanza hawamjui hata mara moja, wataweza kuniunga mkono katika maamuzi yangu? Mmh! Huo nao uamuzi mgumu” Wayne alijisemea wakati ndege ikiwa imekwishafika katika ardhi ya Morocco tayari kwa kuendelea na safari ya kuingia Ulaya na kisha kuelekea Marekani.


Jina la Brown Michael Ryn lilikuwa jina kubwa miongoni mwa matajiri ambao walikuwa wakipatikana nchini Marekani. Mzee huyu alikuwa akimiliki miladi mikubwa nchini Marekani pamoja na mingine iliyokuwa katika mataifa makubwa kama Uingereza, Urusi na Ufaransa.
Huyu ndiye alikuwa mwasisi wa shirika la ndege la American Airways, ndiye alikuwa akimiliki kiwanda kikubwa cha kutengeneza makaratasi cha Brown Paper Company Limited, huyu ndiye ambaye alikuwa akiimiliki kampuni kubwa ya kutengeneza magazeti ya Independent ambayo yalikuwa yakitoka mara mbili kwa wiki nchini Marekani.
Tofauti na vitega uchumi hivyo, pia alikuwa na kampuni nyingi pamoja na visima vya mafuta nchini Qatar. Jina lake lillikuwa kubwa na kila siku alikuwa akiingiza kiasi kikubwa cha fedha katika maisha yake.
Mpaka inafika mwaka huo wa 1990, Bwana Brown alikuwa ameingiza kiasi cha dola bilioni sabini katika mwaka huo na kumfanya kuwa tajiri namba kumi na nane duniani. Maisha yake siku zote yalikuwa yametawaliwa na fedha, alikuwa akithamini sana fedha kuliko kitu kingine chochote kile.
Miaka ya nyuma katika kipindi ambacho alikuwa na umri mdogo, alikuwa kijana masikini ambaye alifiwa na wazazi wake na kuachwa akiwa hana kitu. Mchezo wa kamari wa Pluto Game ndio ambao ulimpatia fedha kiasi cha dola elfu themanini ambazo akazifanyia biashara ambayo ikaanza kumuingizia fedha.
Maisha yake yakabadilika na kumfanya kuongeza jitihada kwa kila biashara ambayo alikuwa akiifanya. Ni ndani ya mwaka mmoja tu, akafanikiwa kumiliki hisa ya asilimia arobaini katika kampuni ya kutengeneza magari ya Mc Lloyd.
Alipofikisha miaka ishirini na mbili akaamua kumuoa mwanamke mzuri, Ruth ambaye aliishi nae kwa miaka minne na kuachana nae. Hapo ndipo alipoamua kutulia ila baada ya miaka miwili akamuoa mwanamke mmoja ambaye alikuwa akiitwa Lydia.
Huyu ndiye ambaye alikuwa amedumu nae katika ndoa mpaka kumpatia watoto wawili, Wayne na msichana Esther. Watoto hawa ndio ambao walikuwa kila kitu katika maisha yake, aliwathamini kuliko hata alivyozithamini biashara zake.
Kijana wake, Wayne alionekana kuwa tofauti sana na watoto wa matajiri wengine. Yeye alikuwa akiishi maisha ya peke yake, kamwe hakuwahi kuchangamana na watoto wa matajiri. Maisha yake yalikuwa mitaani pamoja na watoto weusi ambako alikuwa akikaa nao na jioni kurudi nyumbani.
Maisha yake yalikuwa yakimkasirisha baba yake, kila siku alikuwa akimkaripia na hata kumpiga lakini Wayne hakuonekana kubadilika. Bwana Brown akaonekana kuchoka, akaamua kumuacha Wayne kuishi maisha ambayo alikuwa akitaka kuishi.
Hata Wayne alipoamua kumleta mchumba wake, Luciana, Bwana Brown akaonekana kukasirika. Kamwe hakutaka mtoto wake awe katika uhusiano na msichana yeyote wa kimasikini, alihitaji kijana wake awe katika uhusiano na msichana yeyote kutoka katika familia ya kitajiri.
Hapo ndipo alipoanza mipango yake ya chini chini kuhakikisha kwamba Wayne anaingia katika uhusiano na msichana yeyote kutoka katika familia ya kitajiri. Akafanikiwa kumuunganisha Wayne na msichana Kristen ambaye alikuwa ametoka katika familia ya kitajiri.
Wayne na Kristen wakaanza kuzoeana na hatimae kuanzisha uhusiano ambao ulionekana kuwafurahisha wazazi wao. Mipango ya harusi ikaanza kufanyika taratibu. Kila tarehe ya harusi ilipokuwa ikikaribia, harusi ilikuwa ikihahirishwa kwa sababu ambazo hazikujulikana vizuri.
Wayne akaonekana kukasirika, na hapo ndipo alipoamua kuomba muda wa kupumzika kwenda katika nchi yoyote abayo ilikuwa na vivutio vizuri. Hapo ndipo alipoisoma Tanzania katika ramani ya dunia na kuamua kuja nchini Tanzania.
Akatamani kuziona mbuga za wanyama ambazo zilikuwa zikitangazwa sana pamoja na mlima mrefu kuliko milima yote barani Afrika. Akasafiri tena akiwa peke yake, japokuwa baba yake alikuwa akimtaka atumie ndege ya kukodi lakini akaonekana kukataa kabisa.
Kwa sasa alikuwa ndani ya ndege kurudi nchini Marekani. Kichwa chake wala hakikutulia kwa mawazo, wasichana wawili ambao walikuwa kichwani mwake walionekana kumchanganya kupita kawaida.
Ndege ikaanza kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Morocco na kuingia katika nchi za Ulaya. Kitu ambacho alikuwa akikitaka Wayne ni kufika nchini Marekani haraka iwezekanavyo ili apate kujua ni kitu gani alitakiwa kukifanya kwa wakati huo ambao mchumba wake alikuwa katika matatizo makubwa.
Kutoka nchini Morocco mpaka nchini Marekani, alitumia masaa ishirini na mbili na ndipo ndehe ikaanza kutua katika uwanja wa ndege jiji New York. Mara baada ya ndege kusimama, abiria wakaanza kuteremka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jengo la uwanja huo wa ndege ambako baada ya mizigo yao kuchunguzwa, wakaichukua na kutoka nje.
Gari aina ya BMW ilikuwa ikimsubiri nje, alipoifikia, akaingia ndani ya hiyo gari na kisha safari ya kuelekea Eastchester kuanza huku ikiwa imetimia saa tano asubuhi. Ndani ya gari Wayne hakuonekana kuwa na furaha, muda wote alikuwa akimfikiria Kristen.
Gari likasimama nje ya jengo kubwa lililojengwa katika eneo kubwa lililokuwa na ukubwa wa mita mia moja na ishirini kwa urefu na upana wa mita sabini. Geti likajifungua na gari kuingizwa ndani. Wayne akateremka na kuanza kuelekea ndani ya nyumba hiyo.
Wazazi wake hawakuwepo, ni wafanyakazi wa ndani tu ndio ambao walikuwa wakizunguka zunguka ndani ya nyumba ile. Alipoulizia mahali walipokuwa, aliambiwa kwamba walikuwa katika hospitali ya St’ Mathew ambako mchumba wake, Kristen alikuwa amelazwa.
Wayne akatoka ndani ya nyumba ile, akaanza kuelekea katika sehemu za kupakia magari na kisha kulichukua gari lake aina ya Aston Martin na kuanza safari ya kuelekea katika hospitali hiyo ambayo ilikuwa kusini mwa jiji la New York karibu kabisa na bandari ya Hamilton.
Mawazo juu ya Happy yakafutika, Kristen ndiye ambaye alikuwa akimfikiria sana kwa wakati huo. Aliendesha gari kwa mwendo wa kasi, shida yake ilikuwa ni kutaka kufika hospitalini haraka iwezekanavyo. Ni ndani ya dakika thelathini tu, akawa analipaki gari lake katika eneo la hospitali hiyo.
Kwa haraka sana akateremka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jengo la hospitali hiyo, sehemu ya kwanza kwenda ilikuwa mapokezi, akamulizia mgonjwa wake. Dada wa mapokezi akachukua kipanya cha kompyuta na kuanza kukipeleka huku na kule huku macho yake yakiwa katika kioo cha monita ya kompyuta.
Akaliandika jina la ‘Kristen’ na kisha kompyuta yenyewe kuanza kutafuta. Wayne alikuwa kimya akimwangalia yule dada wa mapokezi kwa jinsi alivyokuwa akicheza na kompyuta yake. Ni ndani ya sekunde kumi na tano tu, akaonekana kukipata kile alichokuwa akikitafuta.
“Yupo chumba namba 108 katika ghorfa ya sita” Dada yule alimwambia Wayne.
Wayne hakutaka kupoteza muda wake, alichokifanya ni kupanda lifti na kisha kuanza kuelekea katika ghorofa hiyo ambayo alikuwa ameelekezwa. Bado kichwa chake hakikutulia kabisa, mawazo juu ya Kristen yalikuwa yakimtesa kupita kawaida.
Alipofika katika ghorofa hiyo akateremka na kisha kuanza kupiga hatua kukitafuta chumba hicho. Alipokifikia, akakishika kitasa na kuanza kuufungua mlango. Kwa kuwa muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umefika, akaruhusiwa kuingia.
Macho yake yakatua kitandani, Kristen alikuwa kimya kitandani pale huku mashine ya Oksijen ikiwa imefunika pua na mdomo wake. Wayne akajikuta akiishiwa na nguvu, akaanza kupiga hatua kuelekea katika kitanda kile.
Japokuwa pembeni ya kitanda kile walikuwepo wazazi wake pamoja na wazazi wa Kristen lakini yeye wala hakuonekana kuwaona, mtu aliyekuwa akimuona kwa wakati huo alikuwa Kristen tu. Alipokifikia kitanda kile, akapiga magoti chini, akauchukua mkono wa Kristen na kuubusu.
“Usiniache mpenzi...” Wayne alisema.
Machozi yakaanza kumtoka na kutiririka mashavuni mwake, hali ambayo alikuwa nayo Kristen ilionekana kumuumiza kupita kawaida. Katika maisha yake, ugonjwa wa pumu ndio ambao alikuwa akiuchukia kuliko ugonjwa wowote kwa kuwa ulikuwa ukimkosesha amani kupita kawaida.
“Lakini kwa nini mimi? Mbona maisha yangu ya uhusiano hayana furaha kabisa? Mbona kila siku ni mimi tu. Nani ameichukua furaha yangu?” Wayne alikuwa akijiuliza.
Akashikwa bega lake kwa nyuma, alipoyageuza macho yake, alikuwa baba yake, Bwana Brown. Wayne akasimama na kisha kumkumbatia baba yake huku akilia tu. Mama yake, Bi Lydia nae akawasogelea na kisha kuwakumbatia. Wote walionekana kuumizwa na hali ile ambayo alikuwa nayo Kristen, kila siku sala zao zilikuwa ni kutaka Kristen apone kabisa ugonjwa ule.
Wazazi wa Kristen ambao walikuwa pembeni nao wakawasogelea na kuwakumbatia. Wote walionekana kuumizwa na hali ambayo alikuwa nayo Kristen, kwao waliona kwamba muda wowote ule msichana yule angepoteza uhai wake.
Walihangaika katika kila hospitali huku wakijitahidi kutumia kila aina ya dawa ambayo waliambiwa watumie lakini wala hali ya Kristen haikubadilika, kila siku alikuwa vile vile. Wote wakakata tamaa na maisha ya Kristen, sala zao ambazo kila siku walikuwa wakisali zikaonekana kukosa majibu kutoka kwa Mungu wao.
Kristen akakaa katika hospitali ile kwa muda wa wiki mbili, akaruhusiwa kurudi nyumbani huku akionekana kuwa mzima wa afya. Hatua hiyo ikaonekana kuwa ya furaha kwa Wayne ambaye alionekana kumthamini sana katika maisha yake.
Miezi mitano ikapita. Kitu alichokipanga pamoja nae ilikuwa ni kusafiri kuelekea nchini Tanzania huku sababu yake kubwa ikiwa ni kutaka kumuonyeshea mbuga mbalimbali za wanyama pamoja na kuuona mlima mkubwa kuliko wote barani Afrika.
Kristen hakutaka kupinga, kwake, matembezi ndio yalikuwa moja ya maisha yake. Akamkubalia mpenzi wake kwa moyo mmoja kusafiri nae kuelekea nchini Tanzania. Moyoni hakujua kwamba Wayne alitamani sana kuelekea nchini Tanzania kwa sababu moja tu, kumuona Happy ambaye tayari alikwishaanza kurudi kichwani mwake kwa kasi ya ajabu.
Siku tatu zilizofuata walikuwa ndani ya ndege ya Amerian Airlines wakianza safari ya kuelekea nchini Tanzania. Ndani ya ndege walikuwa wakiongea mengi lakini mudaa wote Wayne alikuwa katika mawazo mazito juu ya Happy.
Walichukua masaa ishirini na saba, ndege ikaanza kutua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Kambarage Nyerere. Wakateremka na kisha kukata tiketi ya ndege ya siku hiyo ya shirika la Precious kwa ajili ya safari ya kuelekea jijini Arusha ambako huko wangetembelea sehemu mbalimbali za mbuga za wanyama na pia kusafiri mpaka Kilimanjaro ambako wangeupanda mlima Kilimanjaro.
Ndani ya saa moja, ndege ya shirika la Precious ilikuwa ikitua katia uwanja wa ndege wa KIA ambako wakachukua teksi iliyowapeleka mpaka Arusha mjini ndani ya hoteli ya nyota tano ya Chui Chui.
Kila mmoja akaonekana kuwa na furaha, walitembea sehemu mbalimbali wakiwa pamoja huku wakinunua vinyago vingi kwa ajili ya kurudi navyo nchini Marekani. Katika vipindi vyote hivyo, Wayne alikuwa na mawazo ya kuonana na Happy tu.
Asubuhi iliyofuata, saa moja akaamka na kuanza kuvaa nguo zake. Kitu alichokuwa akikitaka ni kuondoka na kuelekea kwa shangazi yake Happy ambapo angemuulizia Happy na kuonana nae. Hata kabla Kristen hajaamka, Wayne akaamka na kuanza safari ya kuelekea huko huku akihakikisha kwamba Kristen hakumuona katika kipindi ambacho aliondoka.
Njia nzima Wayne alikuwa na mawazo juu ya Happy. Aliukumbuka uzuri ambao alikuwa nao msichana huyo, kwake alionekana kuwa msichana wa ajabu ambaye hakustahili hata siku moja kukaa nchini Tanzania.
Alifika katika nyumba hiyo, Bi Selina alikuwa nje akifagia uwanja wa nyumba hiyo kwa kutumia ufagia mkubwa. Uso wa Wayne ukajaa tabasamu, kitendo cha kumuona Bi Selina kwake kikaonekana kumfariji kupita kawaida. Wakasalimiana kwa furaha hadi kukumbatiana.
“Aliondoka kuelekea nyumbani kwao” Bi Selina alimwambia Wayne.
“Siwezi kumuona kwa siku ya leo?” Wayne aliuliza huku akionekana kuwa na kiu ya kutaka kumuona Happy.
“Inawezekana. Inabidi tuondoke hata asubuhi hii. Ni mwendo wa dakika ishirini tu hadi kufika kwao kwa daladala” Bi Selina alimwambia.
Hakukuwa na kitu cha kusubiri, alichokifanya Bi Selina ni kujiandaa na kisha kuanza safari ya kueleka, Machame, Kilimanjaro. Ingawa ndani ya gari walikuwa wakiongea lakini Wayne alionekana kuwa na mawazo. Kitu cha kwanza alikuwa akimfiria Happy lakini kitu cha pili alikuwa akifikiria kuhusu Kristen katika kipindi ambacho angeamka na kumkosa kitandani.
“Nitahitaji kumuona tu ili mladi kiu yangu ikatike na hata ikiwezekana nifanye nae tena” Wayne alikuwa akijisemea moyoni katika kipindi ambacho safari ilikuwa ikiendelea.


Je nini kitaendelea?
Je Wayne ataweza kumuona Happy?
Je nini kitatokea baada ya wawili hawa kuonana?
Itaendelea.
 


FACEBOOK CHATTING--------- 3



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269



MSICHANA: Mbona kimya?
MIMI: Unajua internet connection inazingua sana. Yaani mara ikate, mara irudi. Yaani tabu tupu.
MSICHANA: Poleee. Naomba unijibu basi.
MIMI: Ninae kwa sasa.
MSICHANA: Unae?
MIMI: Ndio. Ila hanionyeshei mapenzi ya dhati. Mara nyingi najitahidi kumtumia meseji, hanijibu, nikimpigia simu usiku, ipo bize tu. Tena si hivyo tu, hadi usiku wa manane ipo bize. Unahisi nini hapo?
MSICHANA: Unaibiwa.
MIMI: Kama naibiwa, nawe upo tayari kumuibia?
MSICHANA: Una maana gani?
MIMI: Hahahaha! Acha utani. Usitake nianze kutoa maana moja kwa moja hadi watu wa facebook washtukie.
MSICHANA: Kama yeye mwizi, sina budi nami kuwa mwizi.
MIMI: hauoni dhambi kuiba?
MSICHANA: Kwenye mapenzi sidhani kama kuna dhambi kuiba. Anayeua kwa upanga nae atauawa kwa upanga.
MIMI: Mmmhh! Sawa. Ila samahani kidogo. Kuna swali nataka kukuliza.
MSICHANA: Kuwa huru
MIMI: Unaonekana kuwa msichana wa tofauti sana. Yaani sio aina ya msichana ambaye amekulia hapa.
MSICHANA: Yeah! Nimeishi sana nchini Marekani ambako huko nilikaa kwa muda mrefu sana na ndipo nikalilia kuja Tanzania.
MIMI: Mmmh!
MSICHANA: Mbona unaguna tena?
MIMI: Hakuna bhana.
MSICHANA: Vipi kuhusu namba ya simu.
MIMI: Kwani unaitaka leo?
MSICHANA: Ndio. Nataka tuongee leo kama nilivyokwambia.
MIMI: Hivi unajua leo lini?
MSICHANA: Jumatatu.
MIMI: Hatutoweza kuongea kwa leo. Kesho inatakiwa niwe chuoni saa tatu.
MSICHANA: Chuo gain?
MIMI: Ninaposoma.
MSICHANA: Kwa hiyo tutaongea lini?. Nina hamu sana ya kusikia sauti yako.
MIMI: Labda Ijumaa.
MSICHANA: Kuanzia saa ngapi?
MIMI: Saa tano.
MSICHANA: Ok! Kadri tunavyoendelea kuongea na ndivyo ambavyo ninazidi kufall inlove zaidi.
MIMI: Hahahahaha
MSICHANA: Unazicheka hisia zangu?
MIMI: Hapana. Umekuwa mwepesi sana kufall inlove.
MSICHANA: Yeah! Sijui kwa sababu gani.
MIMI: Labda kwa sababu una hamu ya kuniumiza hapo baadae.
MSICHANA: Haiwezekani kabisa. Labda wewe ndio uniumize.
MIMI: Kwangu haitowezekana kabisa. Niamini.
MSICHANA: Sawa. Ila naomba unipe namba ya simu ili niwe na amani.
MIMI: Usijali. Nipe yako ili nikupigie.
MSICHANA: Yangu ni 0719 878 ……
MIMI: Poa.

Sikutaka kuchelewa, nilichokifanya ni kumpigia na kuanza kuongea kwa dakika chache na kisha kurudi tena kwenye meseji ndani ya mtandao wa Facebook. Sauti yake ilikuwa nzuri sana, yaani ilifanana na jinsi alivyokuwa. Mara nikashtukia meseji kutoka kwake ikiingia kwenye akaunti yangu ya facebook.

MSICHANA: Mmmh! Una sauti nzuri mpenzi.
MIMI: Hahaha! Acha kunizingua bhana. Mbona sauti yangu mbaya sana.
MSICHANA: Nzuri, nimeipeda sana.
MIMI: Asante. Hata yako nzuri pia. Ulikuwa muimba kwaya nini?
MSICHANA: Yeah! Ila nilipokuwa nchini Marekani.
MIMI: Basi ndio maana.
MSICHANA: Naomba tuendelee kuchati baadae mpenzi. Mama amenipigia simu na kuniambia anataka twende Mlimani City kufanya shopping ya vyakula na mavazi.
MIMI: Poa. Ila kama ukichelewa sana, unaweza kunikuta nimelala.
MSICHANA: Usijali, nitawahi.
MIMI: Ok.
MSICHANA: Nakupenda mpenzi.
MIMI: Nakupenda pia.

Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kuanza mahusiano na msichana ambaye sikuwahi kukutana nae. Nikajiona kikizama kwenye mapenzi kwa asilimia mia moja, moyo wangu ukaonekana kumhitaji kupita kawaida.

MIMI: (Mawazoni: Dah! Nimeshachanganyikiwa sasa. Ngoja nilale then nichati nae hiyo usiku).

Akili yangu ilikuwa imechoka sana na hivyo nilihitaji muda wa kulala. Nililala kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka saa mbili usiku. Nilipoamka, nikaelekea kuoga, nikala na kisha kuwasha laptop. Nilipojiunga na mtandao wa facebook, msichana yule alikuwa miongoni mwa marafiki zangu waliokuwa online.

MSICHANA: Waaaoooo! Karibu mpenzi.
MIMI: Asante.
MSICHANA: Nimekumiss mpenzi.
MIMI: Nami pia baby. Kuna jipya?
MSICHANA: Mengi tu.
MIMI: Kama yapi?
MSICHANA: Nilitaka kumwambia mama kuhusu wewe. Ameniona kuwa wa tofauti sana leo, muda wote alikuwa akiniona kuwa na furaha.
MIMI: Naomba usifanye hivyo.
MSICHANA: Kwa nini?
MIMI: Muda bado wa kufanya hivyo.
MSICHANA: Lakini ni kitu cha kawaida baby. Unafikiri atanigombeza? Wala hatoweza kufanya hivyo.
MIMI: Najua ila naomba usifanye hivyo kwa sasa.
MSICHANA: Sasa unataka nimwambie lini?
MIMI: Siku yoyote ile lakini sio wiki hii.
MSICHANA: Sawa. Ninauheshimu uamuzi wako.
MIMI: Nashukuru kwa kunisikiliza mpenzi.
MSICHANA: Kuna kitu nataka kufanya.
MIMI: Kitu gani?
MSICHANA: Nimemwambia rafiki yangu kuhusu wewe.
MIMI: Rafiki yupi?
MSICHANA: Rafiki yangu, Lydia.
MIMI: Ndiye nani huyo?
MSICHANA: Ninasoma nae shule. Amefurahia sana. Naweza kumuonganisha tuchati pamoja nae?
MIMI: Kwani yupo online kwa sasa?
MSICHANA: Ndio. Tena amenitumia meseji na kuniambia kuwa tuchati wote watatu.
MIMI: Poa. Tengeneza kundi la watu watatu.
MSICHANA: Sawa

Nikabaki kimya, msichana huyu alionekana kuchanganyikiwa zaidi yangu, mapenzi yalikuwa yakionekana kumchanganya akili yake kupita kiasi. Kwa jinsi alivyokuwa na furaha, nilimuona kuwa na kiu ya kutaka kumfahamisha kila mtu kuhusu uhusiano wetu.

MSICHANA: Tayari.
MIMI: Mambo Lydia.
LYDIA: Poa. Mzima shemeji
MIMI: Mzima tu. Maisha yanasemaje?
LYDIA: Safi tu. Mbona umemchanganya sana rafiki yangu?
MIMI: Nimemchanganya au kajichanganya?
MSICHANA: Umenichanganya.
MIMI: Hapana bwana. Umejichanganya wewe mwenyewe.
LYDIA: Kwa hiyo amejichanganya yeye mwenyewe?
MIMI: Ndio. Au kama nimekosea sana, acha niseme kwamba mapenzi ndio yaliyomchanganya.
LYDIA: Hahahaha
MSICHANA: Sasa unacheka nini na wewe.
LYDIA: Case closed. Wewe umeniambia amekuchanganya kumbe umejichanganya wewe mwenyewe. Hahahaha
MSICHANA: Unacheka unaona mazuri Lydia? Nimejaribu kusoma lakini nashindwa kabisa, yaani kila nikijaribu, nakuwa sina hamu kabisa. Si unaona hata kukupigia simu nimeshindwa siku ya leo.
LYDIA: Acha utoto wewe. Unajifunza kupenda nini?.
MIMI: Ajifunze wapi huyo. Anaonekana mzoefu tu wa mapenzi.
MSICHANA: Nani kakwambia kama mimi mzoefu? Au kwa sababu ya picha?
LYDIA: Picha gani tena?
MSICHANA: Hayakuhusu na wewe.
LYDIA: Sasa kama hayanihusu kwa nini umeniambia niongee nae?
MSICHANA: Nimekwambia uongee nae lakini si kumuuliza kuhusu picha. Hilo niachie mimi na Nyemo wangu.
MIMI: Mbona mnakuwa kama hamueleweki? Tatizo nini tena?.
MSICHANA: Hakuna tatizo mpenzi. Naomba turudi kwenye chartin yetu kama kawaida. Achana na huyu Lydia.
MIMI: Mbona umebadilika ghafla mpenzi?
MSICHANA: Kawaida tu.
LYDIA: Ok! Usikasirike rafiki yangu. Nyemo naomba unitumie friend request.
MSICHANA: Hapana. Sitaki. Usimtumie mpenzi.
MIMI: Kwa nini?
MSICHANA: Basi tu.
LYDIA: Acha wivu shosti. Haujiamini?
MSICHANA: Najiamini ila naogopa udhaifu wa mwanaume.
MIMI: Hahahaha
MSICHANA: Unacheka kwani uongo? Nyie wadhaifu sana. Huyu Lydia anaweza akaleta matatizo katika mahusiano yetu. Mahusiano yenyewe bado machanga sana.
MIMI: Aya. Umeshinda wewe mpenzi. Kama vipi usiku mwema Lydia, naona dogo ameshakasirika bhana.
MSICHANA: Nani dogo?
MIMI: Wewe. Kwani unajiona mkubwa? Bado mdogo.
MSICHANA: Sawa. Wewe si mkubwa! Usiku mwema Lydia.
LYIDA: Nanyi pia.

Mawasiliano ya watu watatu yakakatika muda huo, kundi la kuchati la watu watatu likafutwa na kurudi katika mawasiliano ya kawaida. Kuna hali nikaanza kuigundua, msichana huyu alikuwa akionekana kuwa na wivu sana, alitaka mimi niwe wake kama wake tena peke yake, hakutaka mtu yeyote amuingilie kwenye mapenzi yake. Tukaanza kuchati kama kawaida yetu.

MSICHANA: Unataka niibiwe mali yangu.
MIMI: Hahahaha! Wasiwasi wako tu. Mwizi hawezi kukuibia kama sijampa nafasi ya kukuibia.
MSICHANA: Sawa bwana.
MSICHANA: Naomba kitu kimoja mpenzi.
MIMI: Kitu gani?
MSICHANA: Nimeshindwa kuvumilia kabisa.
MIMI: Kuvumilia nini?
MSICHANA: Nimeshndwa tu. Naomba tufanye mapenzi kwa njia ya simu.
MIMI: Mbona unakuwa na haraka hivyo?
MSICHANA: Ndio maana nimesema naomba. Naomba unisaidie katika hilo mpenzi. Pleaaseee
MIMI: Sawa.
MSICHANA: Nashukuru kwa kunisikiliza.
MIMI: Usijali. Ila mchezo huu una sheria zake ili uchangamke.
MSICHANA: Sheria gani?
MIMI: Moja, Utatakiwa kufanya kila kitu nitakachokwambia. Usipofanya tu, umeharibu mchezo.
MSICHANA: Nitafanya.
MIMI: Mbili, Unatakiwa kunipa nafasi mwilini mwako. Wewe kuwa kila sehemu ya mwili wako, ila mikono yako acha niwe mimi.
MSICHANA: Sawa. Hakuna tatizo.
MIMI: Simu yako inatumia hearphone?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Basi kwa leo tumia hizo.
MSICHANA: Sawa. Kuna kingine mpenzi?
MIMI: Ndio. Nitumie namba yako ya vodacom. Nataka tutumie mtandao huo leo. Tigo network yao inazingua sana, wanaweza kutukatisha mara kwa mara.
MSICHANA: Sawa.

Wala hakutaka kuchelewa, hapo hapo akanitumia namba yake ya Vodacom japokuwa alikuwa akitaka yeye kunipigia. Muda ulizidi kwenda, msichana yule alionekana kuwa na kiu kubwa ya kufanya mapenzi kwa kutumia njia ya simu. Kila wakati alikuwa akiniambia wazi kwamba muda ulikuwa hauendi kabisa. Ilipofika saa tano, nikampigia kwa kutumia laini ya Vodacom, akakata simu na kisha kunipigia. Hakujua kama mimi ndiye nilikuwa mkali wa kufanya mapenzi kwa njia ya simu. Nilikuwa nikiufahamu sana mchezo ule ambao ulikuwa unachezwa sana na vijana kama sisi ambao tulikuwa tumekulia uswahilini, hasa huku Tandale.

MIMI: Upo tayari?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Uko peke yako chumbani?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Unaikumbuka sheria yetu ya kwanza?
MSICHANA: Ndio.
MIMI: Ilikuwa inasemaje?
MSICHANA: Nifanye kila utakachoniambia.
MIMI: Safi sana. Naomba uzime taa.

Nikaanza kumsikia akiinuka kitandani, baada ya muda, nikaisikia switch ikilia kuona kwamba tayari alikuwa amezima taa ya chumbani kwake na kisha kurudi kitandani.

Itaendelea

Saturday, April 6, 2013

RIWAYA: WASALIMIE KUZIMU========4

 

 

MTUNZI: Hussein Wamaywa

SIMU: 0755 697335


SEHEMU YA NNE


Saadan akamtazama Nasra na kuyafikia majibu yake, zilikuwa hoja za uhakika ambazo zingemgharimu muda mwingi kuziweka sawa ili kuondoa mashaka kwa Nasra, akajikuta akishusha pumzi za kukata tamaa na kusema.
“Sasa unataka kuniambia nini? Kwamba hunipendi na hutaki kuolewa na mimi?”
Ikawa zamu ya Nasra kumtazama Saadan kwa muda kabla hajayarudisha macho chini, kwa ujumla Saadan alikuwa amekata tamaa. Akaachia tabasamu dogo na kumuonea huruma.
“Sikiliza Saadan! Nikikwambia nakupenda, upendo kama huo ulionao wewe kwangu ninakuongopea! Baba wa watoto hawa ndiye haswa aliyeushika moyo wangu. Hata hivyo juhudi zako zimenifanya nigundue ni namna gani unavyonipenda.
Na wanadiplomasia, wanasaikolojia na hata wanaaikolojia wote wanakubali kwamba ni vizuri zaidi ukaishi na mtu anayekupenda sana kuliko wewe unavyompenda!
Kwa kuzingatia usemi huu na sababu nilizokueleza hapo nyuma, sioni kwa nini nikukatishe tamaa huenda nikakubali unioe, lakini kwanza unifanyie yafuatayo:-
“Kwanza nataka kuja Oman kama mtalii ili wazazi na ndugu zako wanione na pia unitambulishe kwao nione watanipokea vipi. Na labda ikiwezekana niishi nao kwa muda fulani nione tabia zao, waone tabia zangu. Baadae nafikiri nitakuwa nimeshajua nifanye nini!”
“That is good. Very good Nasra!” Saadan akishangilia. Nasra akamuonea huruma moyoni na kuendelea “Kwa sasa ningekushauri urudi Oman ukaendelee na shughuli zako. Acha umenikatia Pasport yangu na za wanangu pamoja na nauli sawa Saadan?”
Furaha ya Saadan ikazimika. “kwa nini tusiondoke wote Nasra?”
“We nenda tu, watoto wangu bado wanahitaji matunzo na wangalizi wa karibu. Sio busara kuwaanzisha mikimiki ya safari kwa sasa!” Saadan akaelewa.
“Sasa utakuja lini?”
“Munkari wa nini? Mawasiliano yapo, hali itakapokuwa shwari nitakufahamisha tu. Muhimu shughulikia Passport kwanza!”
“Nitashughulikia!” Saadan akasema akiwa ameridhika na kuongeza “Naomba uniruhusu nikuage kwa kukumbatia na kukubusu?”
Nasra akatabasamu na kuinua uso.
“Tuliza boli Saadan! Mambo yakiwa sawa, tutakuwa na karibuni robo karne ya kuishi pamoja! Katika kipindi chote hicho utanikumbatia, kunibusu na kukuruka nami tani yako!! Kwa sasa nione huruma, kumbuka mimi ni mzazi.
“Usijali Nasra!” Saadan akainuka na kuaga kabla hajaondoka, moyo na mwili ukiwa na furaha ambayo hakuwahi kuwa nayo kabla. Akamuaga pia mama Nasra alieyekuwa akimalizia kufua na kuondoka.
Mama Nasra akarudi wodini hima akiwa na mshawasha wa kutaka kujua kilichoongelewa. Akamuuliza Nasra juu juu hata kabla hajakaa chini.
“Ah! Nimeamua kumtosa tu ili arudi kwao salama. Vinginevyo angerudi ndani ya sanduku!” Nasra akamwambia.
“Una maana gani?” akauliza. Nasra akamsimulia kila kitu.
“Lakini hukufanya vizuri mwanagu kwa nini usimkatalie moja kwa moja ili akatafute Mwarabu mwenzake huko kwao? Unajua kama ni dhambi kumpa mtu matumaini ambayo hayapo?
“Dhamira mama! Ilinisuta. Alitaka kulia, tayari alishalengwa na machozi. Halafu vile alivyonisaidia pale ukumbini na fedha anazolipa hapa hospitali vimenifanya nisifanye hivyo!”
“Vizuri nilidhani utakaosa utu na kusahau fadhila. Sasa vipi utakwenda Oman? Manake ni lazima tu ataleta Passport kwani mie tayari ameniuliza juu ya cheti chako cha kuzaliwa!”
“Nitakwenda mama! Hii itakuwa ni fursa nyingine nzuri ya kwenda kutalii. Sikuwahi kufikiria kama nitakuja kufika Sultanate! Imetokea wacha niende, nitakwenda!”
“Angalia isije ikawa ile hadithi ya mwonja aslali…” Akatania
“Never mama!” Nasra akakataa kwa dhati “Haiwezi kutokea kwangu!” wakacheka kwa bashasha na kufurahi pamoja!
Jioni ya siku hiyo mama Nasra alikwenda kwake alikokutana na Alwatan Dafu. Akajua akianzisha madahalo hapo hawataelewana akajiandaa kwa mechi na kumwita ndani.
Dafu alipofika ndani, akakuta hali imebadilika mazingira yakamlazimisha afike kifuani kwa mkewe chezo la nguvu lakini la taratibu likaanza kuchezwa. Lilikuwa chezo la kiutu uzima!
Hapo ndipo mama Nasra alipopata nafasi ya kumlaumu mumewe kwa kitendo kilichotokea mchana kule hospitalini, Dafu akakiri kosa na kuahidi kutorudia. Lakini alipoelezwa azma ya Nasra ya kutaka kumuwekea wakili Promota Halfan, hamu ya uroda ikamtoweka ghafla akawa mbogo mfano hakuna.
Ilimlazimu mama Nasra kufanya kazi ya ziada kumrudisha tena kitandani, hali iliyopelekea mjadala wa Nasra kufungwa mara moja.
Hata hivyo tayari Alwatan Dafu alirudi akiwa na wazo moja na msimamo mmoja kwamba atadhibiti gari na akaunti ya Nasra isitolewe hata senti moja mbovu! Alipomueleza haya mkewe aliishia kutazamwa kwa mshangao kama anayemuhurumia.
Ni kweli mama Nasra alimuonea huruma mumewe ambaye hasira zake zilikuwa sawa na zile za mbogo aliyejeruhiwa ambaye hupambana hata na mti!. Mama Nasra hakutia neno tena, alizidi kunyonga nyonga kwa hasira! Huku mawazo yakiwa mengi kichwani. Alimsapoti sana mwanae Nasra, lakini pia alikuwa akimuheshimu na kumuogopa sana mumwewe Alwatan D!
Vitu hivi viwili vilimfanya ausubirie msuguano mwingine wa Nasra na baba yake kwa mshaka makubwa!
Ndivyo ilivyokuwa. Miezi mitatu baadae, watoto wa Nasra walikuwa na hali nzuri kiafya isipokuwa yule mdogo aliyeitwa Romota hali ya huyu haikuwa inaridhisha sana.
Miezi miwili baadae aliruhusiwa na kurudi kwao. Ulinzi wake uliongezeka mara dufu, sasa aliajiriwa mtu mwingine kwa ajili ya kumlinda Nasra tu! Hili halikuwa geti kali tena. Bali geti chungu hasa.
Bahati mbaya hali hii ambayo haikumfurahisha mama Nasra wala Nasra iliondoa amani iliyokuwa imetawala katika nyuma hiyo na kukaribisha machafuko. Nasra akazidisha kiburi na lugha mbaya.
Mara kwa mara Alwatan Dafu alikuwa akimpiga mwanae hasa pale Nasra alipomtamkia maneneo yasiyofaa.
Wakati huo Promota Halfan alishahukumiwa kifungo chake katika siku zote za kesi, Nasra hakuwa amepata nafasi ya walu hata ya kutoka nje ya nyumba yao wachilia mbali kuhudhuria kesi ya Halfan kule Mahakamani.
Gari lake la ushindi ‘Caddilac’ lilidhibitiwa vilivyo na hata siku moja hakuwahi kuiona funguo wala kadi yake. Mambo yote haya yalimuinamia Nasra na kumfanya aishi katika msongo mkuu wa mawazo pamoja na unyonge uliokithiri.
Mama yake alimuonea huruma sana na pengine ili kumpumzisha na madhila haya, akamshawishi aende Oman kwa Sadaam akabadilishe walau hali ya hewa. Wazo ambalo Nasra aliliafiki.
Lakini kabla wazo hilo halijafikishwa kwa Alwatan Dafu, Alwatan akaja na wazo jingine la kumpeleka Tanga kwa mdogo wake Dafu. Wazo ambalo pamoja na Nasra na mama yake kulipinga, bado Nasra alipelekwa Tanga kwa nguvu!
Mungu bariki mke na watoto wa baba yake mdogo walikuwa wakarimu hujaona, taabu ilikuja kwa huyo baba yake mdogo Mansoor! Alikuwa mkali na mkatili mara mbili ya Alwatan Dafu.
Ulinzi aliopata Tanga ulichusha na kuudhi na vile Alwatan Dafu alikuwa amemueleza kila kitu, hali ikawa mbaya zaidi. Nasra alivumilia kwa muda lakini aliposhindwa kabisa akamtolea uvivu na kuanza kumfanyia kama vile anavyomfanyia Alwatan Dafu, kipigo kikachukua nafasi.
Ni pale Nasra alipotishia kuingamiza familia nzima ya baba yake mdogo kwa sumu, ndipo Mansoor aliposalenda. Akainua mikono na kumrudisha Nasra Dar es Salaam.
Nasra akafurahia kwani alijua endapo atakuwa anaongea na mama yake, basi atapata mawazo na ushauri mzuri na hivyo kujipatia faraja ya pekee!
Jioni Alwatan Dafu alirudi akiwa mbogo vibaya akitataka kujua ni kwa nini Nasra ametishia kuangamiza familia ya mdogo wake kwa sumu.
“Ilinichosha baba. Na hata hapa naweza kufanya hivyo mkizidi kunifuatafuata!” Akajibu kijeuri.
“Eti?” Jibu la Nasra likaibua hasira kali iliyoamsha mvua ya kipigo kilichokuja kuamuliwa na mama Nasra. Usiku huo mama Nasra aliutumia muda wake mwingi akimfariji Nasra pamwe na kumkumbusha ‘wazo la Oman’ kabla hajamshauri la kufanya.
Nasra akapokea ushauri huo. Mpaka mama Nasra anaondoka kwenda kulala kwa Alwatan Dafu; Nasra alikuwa bado anatabasamu kwa furaha ya ushauri wa mama yake.
Unadhani walikosea walikosea walionena mtoto wa kike kwa mama yake? Hata kidogo!

* * *

“Baba naomba kuongea na wewe kabla hujaondoka!” Nasra alimfuata baba yake na kumueleza hayo muda mfupi kabla Alwatan Dafu hajaondoka kueleka katika shughuli zake.
Dafu akamtazama bintiye ambaye sasa amekuwa sugu na mwenye tabia za ajabu ajabu toka alipozaa mapacha, akatikisa kwa masikitiko.
Hapo kabla, Nasra hakuwahi kutaka kuongea na mzazi wake, tena kwa upole na heshima kama alivyofanya leo. Ushauri wa mama yake aliyeamini dawa ya moto ni maji ndio ulimfanya Nasra awe hivi.
“Hiyo ndiyo salaam Nasra?” Hasira zilificha nyuma ya swali hili.
“I am so sorry father!” Nasra akatahayari “Shikamoo!”
“Marhabaa! Enhe ulikuwa unataka kuongea na mimi kuhusu nini!”
“Mengi tu baba, mengi sana! Sidhani kama unaifurahia hii staili mpya ya maisha yetu ya paka na panya. Kumbuka wewe ndio baba yangu, nisipoongea na wewe juu ya shida zangu nani atafanya hivyo? Tafadhali nisikilize walau kwa dakika chache tu!”
“Wakati mwingine unakuwa binti mwenye busara Nasra. Nipo kwa ajili yako Mama, ninakusikiliza mwanangu!” Nasra akatabasamu, tayari alishamtoa mzee wake kunako uadui na kumfanya rafiki kitu ambacho kilikuwa kimeanza kuondoka katika kamusi za vichwa vyao.
“Ni kuhusu hili swala langu la kuolewa na Saadan!”
“Enhe, nakusikiliza endelea!”
“Samahani baba kama nitakuudhi kwa swali hili. Hivi baba ni kweli mimi ni mwanao kabisa kabisa?”
“Kwa nini unauliza hivyo mwanangu?!” Alwatan Dafu akamtazama vizuri.
“Nijibu kwanza baba, nijibu tafadhali”
“Of course! Wewe ni mwanangu wa kuzaa kabisa tena mtoto wangu wa pekee kwa nini unauliza swali kama hili Nasra?”
“Nina sababu baba! Nina sababu za kutosha. Kwanza mfumo wa maisha tunayokwenda nayo baada ya mimi kuzaa, ndio uliopelekea niulize swali hili. Kama mimi ni mwanao inaelekea hunipendi kabisa baba na uko tayari kunipoteza kama sitafanya kile ambacho unakitaka wewe.
Kitu ambacho wazazi wenye upendo wa dhati kwa watoto wao huwa hawathubutu. I think now you know kwa nini nimeuliza swali la aina hiyo”
“Sikiliza Nasra mwanangu, sio kwamba sikupendi la hasha! Nakupenda sana mwanangu tena nakupenda kuliko unavyoweza kufikiria! Unachojaribu kufanya wewe ni kupiga ngumi ukutani, kuuzia mkondo wa maji na wakati mwingine kujaribu kuyapandisha mlima! Kwa hili,huwezi kufanikiwa mwanangu!”
“Una maanisha nini baba?”
“Kwamba mimi ni baba yako mzazi niliyekuzaa, kukulea na kukusomesha. Mpaka sasa uko chini ya himaya yangu! Nimejaribu kukulea katika maadili mema kwa kadiri nilivyoweza, ili uje kuwa mke na mama mwema. Lakini yule khabith Halfan amenizidi ujanja na kuharibu kila kitu! Mungu amlaani atumikie kifungo kwa mateso makuu.
Tena inaonyesha amekujaza maneneo ya ajabu ajabu kiasi kwamba umeshindwa kupokea hata shauri wangu, umenidharau, kunidhalilisha na kuniona sifai! Umediriki hata…..!”
“Usiende mbali baba! Where are you going now?” Nasra akamuwahi alipoona ameanza kupandisha hasira ”Kwa hiyo endapo nitakubali kuolewa na Saadan amani itarejea baina yetu?”
“Bila shaka. Huo ndio ugonvi wetu mkubwa, Halfan sio mtu ni mnyama.”
“Oke, kukuonyesha ni kiasi gani ninakupenda baba yangu mimi nimekubali kuolewa na Saadan….”
Nasra akatua kwa muda kuangalia Alwatan Dafu anaipokeaje kauli hiyo. Dafu aliruka na kupiga ngumi hewani, akarukaruka na furahi mno. Akamkumbatia na kumbusu mwanae kwa fujo mpaka alipotosheka, akamuachia.
Nasra akaendelea “Lakini naomba uniambie kitu kimoja Daddy! Hivi ni kwa nini ukaamua kunitafutia mchumba toka mbali mbali hivi? Unataka kuniambia kuwa Tanzania nzima na nchi dada za Afrika mashariki amekosekana mtu wa kunioa hata uniletee Saadan toka Oman?”
“Inawezekana wapo! Lakini kwa jinsi nilivyokulea, nilitarajia upate mume mstaarabu kwa maana halisi ya neno hilo tena atakayekupenda kwa dhati. Oman ni nchi ya kiislam, nasi ni waislaam nilikuwa na yakini kabisa kule atapatikana kijana mstaarabu kama ninavyotaka. Na kweli, kama hutakuwa mnafiki utakubaliana na mimi kwamba Saadan ni mstaarabu!
Wangelikuwa wachumba wa kibongo na pengine wa kiafrika, hadithi ingekuwa nyingine pengine ningepigwa, ningetukanwa, ningedhalilishwa na kuwekwa katika daraja ambalo hata Matonya yule bingwa wa kuomba hastahili kwalo kuwako huko.
Lakini ilikuwa tofauti.
Ni Saadan aliyehisi tofauti toka mwanzo, akakukimbilia na kukudaka toka ulipojifungua, akawa bega kwa bega na sisi pamoja na mama yako kukupeleka hospitali ili kuokoa maisha yako na ya wanao. Kumbuka anafanya hivi akiwa hahusiki kabisa na mimba yako.
Hiyo tisa kumi ni pale alipokubali kukuoa hivyo hivyo ulivyo na watoto wako na kuahidi kuwalea na kuwatunza. Wachilia mbali kuwalipa gharama za matibabu na matunzo pale Agha Khan hospital! Tanzania ya leo nani anaweza kufanya kama yeye? Nani?!! Na ajitokeze tumuone.
Kwa yakini hakuna, hakuna kwa maana ya watu wanaojua kupenda, natumai ushujua naongelea nini!” Akahitimisha. Nasra akatikisa kichwa kukubaliana nae. Akasema.
“Ni kweli uyasemayo baba. Saadan ana moyo wa peke yake! Lakini mimi…..” Akasita na kumtupia jicho baba yake. Alitaka kusema ‘simpendi kabisa!’ macho ya Alwatan Dafu ndiyo yaliyombadilihia uelekeo wa maongezi.
“Lakini mimi simjui fika! Nahitaji kumjua kwanza baba pengine inawezekana yeye akawa mbaya zaidi kuliko wote uliowataja. Inawezekana anajifanya Simba mwenda pole ili ale nyama! Huwezi kujua baba!”
“Inawezekana wala sio uongo, wala sikatai utabiri wako. Lakini pamoja na yote bado sijaelewa unataka kuniambia nini? Ujue sitaki kabisa kuusikia upuuzi wa Halfan!”
“Swali zuri Daddy! Nataka kwenda Oman kwa Saadan. Nikakae walau mwezi mmoja, miwili au miattu! Nione hali halisi ya maisha ya kule, nimjue vilivyo, naamini nikirudi hapa nitakuwa nimerejea na tarehe ya harusi!”
“Good Nasra. Ndio sababu nakupenda Nasra. Wewe ni msichana wa ajabu. Ninajivunia hilo, I love you Nasra!” Baba Nasra akishangilia kwa vigelegele “Sasa umeamua jambo la busara kuliko yote


***NASRA anamuhadaa babake, naye ameingia mkenge.....
Je akienda OMAN atatoka hivi hivi ama ndo penzi litachipukia huko??

ITAENDELEA KESHO


Recent Posts